Wanadam tumetofautiana sana kuhusu dhana ya kufanikiwa, bahati nzuri kuna mjumbe katoa angalizo kuwa kauli yako ni jumuishi sana nawe uka pin point Utajiri!. Sawa, kwako na baadhi ya walimwengu wanaamini kufanikiwa ni kuwa na Ukwasi wa Mali na Fedha, sisemi mnakosea, ila Dhana ya mafanikio kila mtu anaitafsiri kutokana na kuridhika kwa nafsi yake kwa kile anachojaaliwa kukipata baada ya kukitamani. Huko ndiko kufanikiwa kwa ujumla!. Kwangu mie naona sio tu Ndugai amefanikiwa bali hata Mangula na Kibajaji wamefanikiwa! Sijamsahau Msekwa(sijui ni mgogo yule
) wangapi wamezitamani nafasi zao na hajafanikiwa? Mie Mbondei na wala sijaoa Mgogo,hata kuwekeza chochote Ugogoni sijafikiria ila nawajua wagogo wengi wenye maisha ninayoyatamani.