Bring Back Our Money

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Watanzania wote kwa ujumla wetu,tujitokeze kuwaunga mkono vijana wazalendo wa nchi hii wakiongozwa na Ben Saanane,katika kushinikiza kurejeshwa kwa mabilioni yetu yaliyochotwa kiholela kupitia sakata la Kampuni ya IPTL. Ingaa imekuwa ikikanushwa kuwa mabilioni hayo si ya umma,bado tunaamini kuwa ni mabilioni yetu na yanatokana na kodi zetu kama watanzania.

Itoshe hata kupaza sauti zetu kukomesha uchotwaji huu wa mabilioni ya fedha nchini mwetu. Ya KAGODA,MEREMETA,RICHMOND na mengineyo nayo ni mifano ya mambo kama haya ya IPTL. Kijana, mzee na wengineo,tuunge mkono juhudi hizi za vijana wazalendo kupinga nchi yetu kuwa 'shamba la bibi'

Sajili kauli yako ya kukataa ufisadi nchini kwa kusema : Bring Back Our Money! Mimi nasema: BRING BACK OUR MONEY!


Mzee Tupatupa wa Lumumba (safarini Iringa-Morogoro)
 
Una akili timamu, lakini uwezo wako wa kufikiri ni mdogo sana dada angu. Sorry for this, but that's fact

Ulitaka upewe umeme wa bure?

Si uolewe tu kama mimi, sijui hata umeme unanunuliwa saa ngapi, utapata umeme wa bure.
 
si bora hata hizo zinaonekana zinafanya nini, anazotafuna Mshumbuzi na Mukya siyo ruzuku ambayo ni kodi ya wananchi?
 
Huyo faiza sijui kama mzima analeta habari za kujiuza barabarani huna la kuchangia nyamaza tumechoka kuibiwa nchi yetu sio masikini viongozi wetu ndo wabinafisi na wanakumbatia ufisadi na rushwa wizi wa pesa za iptl ni mkubwa mno kuliko epa haiwezekani pesa nyingi kiasi hicho kiibiwe arafu presidaa yupo kimia nina mashaka sana na viongozi wa nchi yetu tutamkumbuka mwl nyerere kwa mengi.
 
Ikiona mtu anatetea ujinga huu ujue kwa njia moja ama nyingine, yeye, baba yake, mjomba ama ndugu yake anafaidika na mfumo dhaifu uliopo.
 

Ben Saanae anasumbuliwa na msongo wa mawazo tu kutokana na kukosa cheo kwenye chama, tangu lini akaanza hiyo kazi yake zaidi ya ile ya kumuwekea ZIITO kitu kigumu
 

anzeni kwanza kuwsafisha viongozi wenu wenye ndoto ya kushika madaraka maana nao ni wachafu kupindukia.
 
Haya mambo ya ufisadi hayakuanza leo:
Mwenyekti wa kwanza wa CHADEMA, Mzee Edwin Mtei, alikuwa Gavana wa BoT.

Mwenyeti wa sasa wa CHADEMA, Mh. Freeman Mbowe, alikuwa mwajiriwa wa BoT.

Kabla ya kupata uenyeti wa CHADEMA, Mh. Freeman Mbowe, alimuoa mtoto wa Mwenyekiti wa kwanza wa CHADEMA, Mzee Edwin Mtei.

Mwenyekiti wa sasa wa CHADEMA, amekiri kwa maandishi kuwa anamiliki mabilioni ya shilingi pesa tasilimu na mali zisizohamishika yenye thamani ya mabilioni ya shilingi.

Hesabu za kiasi cha kodi alicholipa Mh. Freeman Mbowe kwa miaka kumi iliyopita hakiendani na utajiri huo mkubwa alio nao.

Mwenyekiti wa kwanza wa CHADEMA Mzee Edwin Mtei, hupenda kujitambulisha kama mkulima. Hata hivyo, utajiri wake ni mkubwa sana kuliko kiasi cha uzalishaji wa shamba lake lililopo Tengeru, Arusha.

Mzee Mtei amekuwa akitumia pesa zake binafsi kuendesha shughuli zote za CHADEMA tangu ilipoanzishwa mpaka ilipofikia hatua ya kupata wabunge na ruzuku. Huu ni utajiri wa hali ya juu. Sio mbaya kuwa tajiri, lakini utajiri wa mtu ni lazima uendane na kiasi cha kodi anacholipa. Mtu akiwa tajiri sana lakini katika orodha ya walipa kodi haonekani, ni ishara ya ufisadi.

Ukwasi huu wa wanasiasa hawa wawili walioitumikia BoT na kuamua kuunganisha familia zao kwa njia ya ndoa ya binti wa mmoja wao unatokana na chanzo gani?

Je, kuunganisha familia hizi ni njia ya kuongeza uaminifu wa "ushirikiano" waliokuwa nao tangu BoT? Je, "ushirikiano" wao waliouanza BoT unaendelea ndani ya Chadema? Je, hii ndio sababu ya Mzee Mtei kulazimisha Mbowe aendelee kuwa Mwenyekiti na kukataza wagombea "who are from nowhere"?.

Je, biashara ya ukumbi wa muziki inamuwezesha mtu kumiliki mabilioni nje ya nchi? Kiingilio bilicanas ni shilingi ngapi kila mtu? Kwa siku wanaingia watu wangapi? Je, zinatosha kununua nyumba Uingereza, Marekani, Afrika Kusini na Dubai?
 
Ufisadi haujaanza leo:
Walianza kutafuna akina EDWIN MTEI na MBOWE wakiwa BOT hadi leo wanatafuna fedha za ruzuku wenyewe.
 
Ulitaka upewe umeme wa bure?

Si uolewe tu kama mimi, sijui hata umeme unanunuliwa saa ngapi, utapata umeme wa bure.
Jitahidi kwanza basi ujue kinachoongelewa hapa, kama uko karibu na waliohusika na uchotaji huu si ukae kimya? Unaboa sana!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…