VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Watanzania wote kwa ujumla wetu,tujitokeze kuwaunga mkono vijana wazalendo wa nchi hii wakiongozwa na Ben Saanane,katika kushinikiza kurejeshwa kwa mabilioni yetu yaliyochotwa kiholela kupitia sakata la Kampuni ya IPTL. Ingaa imekuwa ikikanushwa kuwa mabilioni hayo si ya umma,bado tunaamini kuwa ni mabilioni yetu na yanatokana na kodi zetu kama watanzania.
Itoshe hata kupaza sauti zetu kukomesha uchotwaji huu wa mabilioni ya fedha nchini mwetu. Ya KAGODA,MEREMETA,RICHMOND na mengineyo nayo ni mifano ya mambo kama haya ya IPTL. Kijana, mzee na wengineo,tuunge mkono juhudi hizi za vijana wazalendo kupinga nchi yetu kuwa 'shamba la bibi'
Sajili kauli yako ya kukataa ufisadi nchini kwa kusema : Bring Back Our Money! Mimi nasema: BRING BACK OUR MONEY!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (safarini Iringa-Morogoro)
Itoshe hata kupaza sauti zetu kukomesha uchotwaji huu wa mabilioni ya fedha nchini mwetu. Ya KAGODA,MEREMETA,RICHMOND na mengineyo nayo ni mifano ya mambo kama haya ya IPTL. Kijana, mzee na wengineo,tuunge mkono juhudi hizi za vijana wazalendo kupinga nchi yetu kuwa 'shamba la bibi'
Sajili kauli yako ya kukataa ufisadi nchini kwa kusema : Bring Back Our Money! Mimi nasema: BRING BACK OUR MONEY!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (safarini Iringa-Morogoro)