Brexit na Paris climate viwe somo kwetu!

Barbarosa

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
22,584
27,782
Nchi zetu huingia Mikataba mingi ya Kimataifa, lkn kama kuna cha kujifunza hii Mikataba siyo rahisi kujitoa kama ambavyo wengi tunadhania!

Sasa hivi nchi ya Uingereza pmj na Wananchi wake kuikataa EU lkn bado ni ngumu sana kwa nchi hiyo kujiondoa EU mara moja, kuna mambo mengi sana kiasi kwamba wengine hata wanasema Brexit inaweza kukwama, Trump ameiondoa USA kwenye Paris Climate Agreement ambayo Obama aliingiza USA bila kuhusisha Seneti ya USA, sasa ingawaje wanasema ni hiari kuingia au kujitoa lkn bado USA anaweza kujiondoa moja kwa moja kuanzia 2020 huko!

Hivyo kwa maoni hii Mikataba tunayoiingia sijui AU, AM, EPA au hata tu Jumuiya ya Madola siyo hiari hivyo kama tunavyofikiri!

Mfano mzuri nchi ya AK imeshindwa kujiondoa ICC ingawaje Raisi Zuma alitaka hivyo na hata Bunge La AK limekubali lkn bado ineshindikana, mpaka sasa hivi!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom