Brazil to play Tanzania in a friendly

Kama kweli its good for though kuna watu watajifagilia apo wakati unaweza kuta ni njia tuu ya kwenda SA.
Chonde chonde T/Stars muwe wastaarabu rafu za kama akina salum kabinda ninja hazitakiwai as mtaaribu unaweza kuta UK nao wana mpango kama huo siku za usoni
MCHEZE FAIR GAME
 
Kama nawaona dada zetu kina Mboni Masimba na Mange waki strategise namna ya kumkamata Kaka na Robinho kimahaba!!

Kaeni mbali na Kaka jamani coz jamaa ni mlokole wa ukweli!!

Duh hawa kweli ni qualified kwenye kujiuza kwa mastaa??
 
Tutasikia muda si mrefu kuwa " ILE ZIARA WALIOKUWA WAFANYE REAL MADRID ILITANGAZWA KWA UTANI. UKWELI NI KWAMBA WATAKAOKUJA NI BRAZIL"
 
Ni bora niende kuangalia mazoezi ya abajalo ktk uwanja mashujaa sinza kuliko kwenda kuwaangalia brazil pasipo saint gaucho ambaye anaaminika kuwa ndiye balozi wa soka la mbinguni hapa duniani.

mbingu gani hiyo unayoifananisha, mbingu ya alah au ya Mungu wa Ibrahim Isaka na Yakobo? uyo ronaldinyo kakufanyia nini hadi ukazimika kiasi cha kumtukana Mungu na mbingu yake kwa kumfananisha na soka la Ronaldinyo? acha kufuru mkuu.
 
Brazil to play Zim & Tanzania

Brazil are to play friendly matches against Tanzania and Zimbabwe before heading into the World Cup in South Africa

The games are to be formally announced when all the required documents have been sent by the respective football federations.

The friendlies are set to take place on June 2 and 7 - ahead of the Samba Kings' opening encounter in the showpiece against North Korea on June 15.

The team is currently trainining in the southern Brazilian city of Curitiba and is to leave for South Africa on Wednesday.

Meanwhile, Zimbabwe captain Esrom Nyandoro has picked up a finger injury that could rule him out of the match against the five-time World Cup winners.

The Mamelodi Sundowns midfielder fractured his finger against AmaZulu in the semi-finals of the Nedbank Cup.

Source:Football365.co.za - All The News
 
Timu ya taifa ya Brasil (Samba Boys) inatarajiwa kucheza na Taifa Stars katika mchezo wa kirafiki utakaofanyika tarehe 7 June 2010. Mechi hiyo itakayokuwa ya mwisho kwa Brasil kabla ya kuanza kwa Kombe la Dunia, inatarajiwa kufanyika katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Hayo yamesemwa na balozi wa Brasil nchini Tanzania alipokuwa akizungumza na gazeti la The Citizen, ambapo alisema taarifa kamili na mipango mingine kuhusiana na hiyo mechi itatolewa na Rais wa TFF ndugu Tenga.

Source: The Citizen of 25 June, 2010

Mimi si support hii issue - Its too political, lakini ki ukweli kucheza na Brazil haitasaidia chochote timu yetu - Sisi tuhangaikie na hapa Africa Mashariki kwanza Rwanda, Kenya Uganda wanatuacha. sisi tunapenda kuongea ongea sana na kujikwaza. Juzi juzi eti tukaomba game na Misri kujipima nguvu tukapigwa 5-0 nini kimefanyika baada ya kipigo?

Haya timu zetu zote zimetolewa katika mashindano ya kimataifa, tunaambiwa ligi yetu legelege tumelifanyia kazi hilo? zingatia ligi hii ndiyo inatoa wachezaji wa taifa tegemea nini mazao yake?

Kwa hiyo kuwaleta Brazil ndiyo itakuwa perfomance ya kina tenga au? kama wameamua kuja kupitia kwetu thats fine - lakini si eti tujipme nguvu na wao - we're too far behind.
 
Mboni Masimba MALAYA CLASS A Tender hiyoooooooooooo kama nakuona ukiopoa Kaka duh noma Kaka mlokole itabidi tu uruke na Lucio maana lazima Etoo atamtonya

MjasiliaMali huyu! Kazi kwenu dada zetu, Ruge kama kawaida walengeshe
 
Brazil to play Tanzania in pre-World Cup friendly

By Emmanuel Muga
BBC Sport, Dar es Salaam, Tanzania

999999.gif

_47406236_kaka.jpg
The likes of Kaka could line up against Tanzania in Dar es Salaam

Brazil are to play Tanzania on 7 June in a World Cup warm-up match ahead of this summer's finals in South Africa.
The Brazilians have become the first non-African team to schedule a friendly in Africa in the build-up to the tournament, which kicks off on 11 June.
Tanzanian Football Federation (TFF) spokesman Florian Kaijage told BBC Sport that a contract would be signed within the next two to three days.
Brazil also plan to play Zimbabwe but no date as yet has been set.
Regarding Brazil's friendly against Tanzania in Dar es Salaam, Kaijage said: "Brazil have already put this game in their plan, so obviously they are sure of coming, unless something unusual happens.

It's very exciting. Finally we've succeeded in attracting Brazil
TFF president Leodegar Tenga


"On our side, we were given some conditions to meet. The federation and the government have been meeting but chances are higher that the conditions will be met for the game to go ahead," he added.

The terms include an appearance fee requested by Brazil, which Kaijage described as being "several million dollars".

Tanzania have been eager to play a part in the World Cup build-up by hosting one of the finalists, and the TFF president Leodegar Tenga stated it would be an exciting prospect for the east African country.
"It's very exciting. Finally we've succeeded in attracting Brazil, who are obviously the biggest team in the world, to play our national team," Tenga commented.
The government earlier this year appointed a committee led by a minister and with a budget of about $6m (£4.17m) for the purpose, but most teams contacted by the TFF turned them down.
North Korea had planned to play two friendlies in Zimbabwe, but that was shelved after protests over Matabeleland, where rights groups say a North Korean-trained army unit killed thousands of people during the 1980s.
Brazil are currently training in the southern Brazilian city of Curitiba and are due to depart on 2 June.
Taifa Stars are currently in a training camp ready for an African Nations Championship (CHAN) final round, second leg qualifier against Rwanda, which will take place on 5 June in Kigali.




Hapo pekundu pameniacha hoi! Itatu-cost several million dollars! Yani hapo ni $2mil kwenda juu. Huu ni ujinga au vipi? Priorities zetu vipi wakuu? Je na Zimbabwe nao itawa-cost hivyo? Nchi ile si ina njaa?
 
Mimi si support hii issue - Its too political, lakini ki ukweli kucheza na Brazil haitasaidia chochote timu yetu - Sisi tuhangaikie na hapa Africa Mashariki kwanza Rwanda, Kenya Uganda wanatuacha. sisi tunapenda kuongea ongea sana na kujikwaza. Juzi juzi eti tukaomba game na Misri kujipima nguvu tukapigwa 5-0 nini kimefanyika baada ya kipigo?

Haya timu zetu zote zimetolewa katika mashindano ya kimataifa, tunaambiwa ligi yetu legelege tumelifanyia kazi hilo? zingatia ligi hii ndiyo inatoa wachezaji wa taifa tegemea nini mazao yake?

Kwa hiyo kuwaleta Brazil ndiyo itakuwa perfomance ya kina tenga au? kama wameamua kuja kupitia kwetu thats fine - lakini si eti tujipme nguvu na wao - we're too far behind.

Point za maana sana. Huu ni mlolongo wingine wa kutupa fedha mahala ambapo hakuna faida. Hii timu ya kwetu inafungwa mpaka na Somalia na Yemen, je unadhani kuwaleta Brazil kuja kucheza na sisi italeta manufaaa yoyote? Never in my life have I seen a sane individual or collection of paying for a whipping (sadomasochists excluded of course).
 
I can see a state dinner coming......Nsajigwa, Nadir na wenzenu msiwaumize wenzenu wanaenda WC
 
Halafu hii kitu imekaaje mi nasikia Brasil washafika Sauzi leo na hakuna habari hii ktk kambi yao so inakuwa vipi hapo wadau? Yaani wafike Sauzi halafu watoke waje Dar? Hii inawezekana kweli?

x2_1706bdb.jpg

x2_17062d4.jpg
 
usitie shaka RayB jamaa wanakuja kama umefuatilia vyombo vya habari leo vya duniani wamesema jamaa wanakuja
 
Hehehe, makubaliano ya wao kucheza Tanzania ni kuwa tuwalipe bilioni kadhaa. Kazi kweli kweli!
 
Brazil inakuja Tanzania na inatarajiwa kucheza na timu ya taifa Taifa Stars katika Uwanja wa Taifa hapo Juni 7 wakati wa usiku. Brazil inapanga kutua Dar es salaam usiku wa Juni 6.

Mipango ya kuja Brazil pengine ni ya muda mrefu, kwa vile Tanzania ilikuwa na kiu ya kujiweka katika jukwaa la kimataifa la soka kwa kutumia fainali za Kombe la Dunia za huko Afrika Kusini.

Inaeleweka Tanzania imeunda kikosi kikubwa cha watu maarufu na wenye fedha ili kutafuta fursa mbali mbali za kuitangaza Tanzania. Katika hilo Tanzania imetengeneza machapisho yenye taarifa za vivutio vya kitalii ambayo yatasambazwa Afrika Kusini kuanzia wakati huu.

Lakini ilikuwa ni kiu ya Tanzania kupata timu ya kuja kucheza Dar es salaam au kufanya mazoezi. Zilijaribiwa nyingi, nyengine zikiwa zimewahi kucheza Dar es salaam kama Cameroon na Ivory Coast kwa upande wa Afrika na nyengine za Ulaya.

Ila hakuna aliyeitupia jicho kwa mfano Korea Kaskazini, ambao hadi sasa wanashikilia kwa kasi msimamo wao wa Ujamaa, kwa sababu ingawa ingekuwa rahisi kuwapata, lakini wasingeleta sifa na ujiko ambao Tanzania inautafuta.

Brazil, Brazil, Brazil ndio ikawa lengo, ila ingepatikana vipi. Kocha wa Tanzania Marcio Maximo akaruka mpaka nchini kwao katika likizo yake na akajaribu kuifanya kazi hiyo. Mguu hapa na mguu kule.

Akasema ingekuwa vigumu na haiwezekani hasa. Alitoa sababu za kiufundi ambazo sote tulikubali. Maana timu kama Brazil kwenda pahala hata urefu wa majani ya kiwanja cha mazoezi hupimwa seuze mahitaji mengine mengi.

Alichosema Maximo ni kuwa Brazil wasingeweza kuja maana hali ya hewa ya Dar es salaam haitafanana na ile ya kituo chao katika kundi lao huko Afrika Kusini.

Nikakutana na Maximo uso kwa uso, na akaniambia hay ohayo, na kunihakikishia kabisa haitawezekana.

Ila aliniambia jengine pia. Kuwaleta Brazil ni gharama kubwa sana na hakuwa na hakika kama Tanzania ingeweza kuthubutu kufanya hivyo.

Na mimi nilikubali hilo kwa sababu huko nyuma nilijaribu kuileta Brazil. Nina maajenti walioko Austria ambao wana viungo muhimu katika ulimwengu wa soka na walinipa ofa hiyo na mie nikaitupa kwa Shirikisho la Soka la Tanzania TFF.

Brazil walidai kulipwa dola milioni moja kwa kucheza mechi moja. Hiyo ni mbali ya tiketi za wachezaji na maafisa lakini pia watu wengine kadhaa. Kwa ujumla kawaida msafara wa Brazil huwa watu 60 hivi.

Leodgar Tenga Rais wa TFF akaanza kuhesabu vidole. La haitawezekana aliniambia. Kabisa haiwezekani. Maana kwa maana hiyo ya gharama zitazohusika basi ni wazi kuwa kiingilia cha chini kitabidi kiwe kikubwa kiasi ambacho cha kutisha na kiingilio cha juu kitakuwa kikubwa kiasi cha kuwa kufuru.

Na Tenga ameshaanza kusema hivyo hivi sasa. Kuwa wadau wa soka wajue kuileta Brazil ni gharama ambayo mzigo wake watabidi waubebe wao.

Huko nyuma Tenga na TFF pia walikataa ofa zangu kadhaa kuleta timu za Amerika Kusini hasa na sababu siku zote ikiwa ni gharama- yaani vipi mchezo utalipa. Nitakupeni mifano ya timu kama hizo.

Kulikuwa na jaribio nilofanya ya kuileta timu ya Paraguay ikashindikana. Nikajaribu Bolivia ikawa hivyo hivyo. Pia nimejaribu timu za Ulaya Mashariki.

Niliwahi kuwaambia TFF kuwa hata siku moja hatutaweza kuipata timu ya Ulaya kuja kucheza bila ya mchango wa makampuni. Kwa kutarajia viingilio tu hatutaweza kupata fedha za kutosha kulileta kundi la nyota ambao huunda timu za taifa za Ulaya.

Wakati huo pengine walikuwa na sababu kwa pembeni kukataa ofa hizo kwa kuwa sikuwa wakala rasmi wa mambo ya soka. lakini sasa nina kibali rasmi cha fifa kufanya kazi kama hizo.

Sasa tunaambiwa Brazil inakuja. Inakuja kwa kupitia Afrika Kusini.Hapa inabidi tujiulize suala moja kubwa sana. Inakuaje timu ishafika Afrika Kusini ambako ndio lengo lake kisha tuitoe huko na kuileta huku.

Tunaambiwa Brazil inakusudia kucheza Tanzania na baadae Zimbabwe katika programu ambayo hatukuwa tumeisikia mapema. Timu zote takriban tumejua mapema zinacheza mechi gani, na hakuna hata timu moja iliyopanga kwenda Afrika Kusini kisha ndio itoke kwenda kucheza mechi za kirafiki.

Lakini hayo ni maalesh…tuseme naiwe hivyo. Hebu tutizame basi imekwendaje mpaka Brazil ikaja Tanzania? Hilo limetokezea baada ya Tanzania kwa njia moja au nyengine kukutana au kuijua kampuni inayoitwa kentaro na tembelea Kentaro - Home utapata mengi.

Kwa ufupi tu Kentaro ni kampuni ya mawasiliano au public relations na ni moja ya zile kubwa duniani na wateja wake ni wale wenye fedha za kupukutika.

Na mimi sikujajua hayo mpaka nilipoona Philippe Huber ndipo akili ilionigonga kwa sababu huyu bwana niliwahi kusoma habari zake kadhaa wa kadhaa katika medani ya soka na ni mmoja ya watu maarufu kama vile wakala wa Kiisrael Pini Zahavi.

Sifa za watu hawa katika mipango ni kubwa sana. Marafiki zao ni marais, mawaziri wakuu na wanasiasa wakubwa wakubwa. Hunywa chai Ikulu na kwenye majumba ya watu wenye ulwa na vyao.

Mwili wangu unatetemeka kama tumba la uvi nikifikiri kiasi gani Phillipe Huber na kampuni yake wamelipwa ili kuwezesha kuipata Brazil kuja kucheza Dar es salaam? Kiasi gani nasubiri watu wengine waniambie kama angalau wanaweza kukisia?

Inaaminika katika dunia ya soka haiwezekani kitu akitake Phillepe Huber Mswisi anayemiliki makampuni kadhaa au huyu Zahavi na kitu hicho kishindikane. Na Huber alipewa kazi na Tanzania na haingewezekana kabisa kushinda kuileta Brazil ukitizama kazi ambazo kampuni yake imezifanya.

Sawa Brazil itakuja itacheza. Mpira wa Tanzania hautapanda kwa kuwa imecheza na Brazil. Wala wachezaji wa Bongo hawatachukuliwa kwenye timu za Ulaya kwa kuwa usiku mmoja wamecheza na Brazil. Wala mimi siamini kuwa Tanzania itakuwa imejitangaza hivyo kwa mechi ya siku moja ambayo nayo imekuja mwishoni mwishoni.

Pengine mtu angejiuliza lipi lingekuwa bora. Kuwekeza kiasi kikubwa cha fedha kwenye soka yetu au kuwaalika watu kuja kucheza usiku mmoja. Hapa ndipo ninapopiga jicho katika sababu halisi ya kuileta Brazil.

Jee si kwa sababu ni mwaka wa uchaguzi?

makala na Ally Saleh "Alberto" wa BBC
 
Brazil wameshatua South Africa ili kuizoea hali ya hewa ya huko, hivi wataweza kusafiri tena ili wacheze Dar na Taifa Stars June 7, 2010? Mimi naona hii mechi kama haitakuwepo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom