Bravo Chadema! Let's move on....

Nyambala

JF-Expert Member
Oct 10, 2007
4,465
1,170
Bravo Chadema! Let's move on....

Kama kuna kitu ambacho Chadema wamefanikiwa katika kipindi hiki basi ni kutimiza ile hamu ya watanzania tulio wengi kuhusu siasa. Chadema imetumbanulia haswaa kwamba pamoja na kwamba ni "official opposition" bungeni lakini pia hata mtaani. Ule utitiri wa vyama umeshakuwa kiasi fulani "obselete" na "irrelevant". It is now clear kwamba CHADEMA ndiyo chama cha upinzani na upinzani unaoishi. Hebu tuangalie yaliyojiri "in just some few months" kutoka uchaguzi uliopita.

1. Chadema imeionyesha CCM na wananchi kwa ujumla kwamba ni vyama vipi ni vya msimu kama alivyowahi kunukulia JK wakati wa kampeni kwamba "Vyama upinzani ni vya msimu" . Toka wakati huo hakuna hotuba iliyosemwa na JK bila walau kuitaja Chadema, directly or indirectly.

2. Chadema imeifanya CCM kusahau hata ilani yake ya uchaguzi na kujikuta iko bize kutekeleza yale yaliyokuwa kwenye ilani ya Chadema mfano katiba mpya. Hatujasikia tena ilani ile iliyokuwa ikinadiwa wakati wa uchaguzi ilipoishia.

3. Chadema imeilazimisha CCM, narudi "IMEILAZIMISHA" CCM kukubali kwamba ufisadi ni janga tena haswaa ndani ya CCM na serikali yake. CCM wamejikuta sasa nao eti wako bize kupambana na ufisadi.

4. Chadema imepelekea CCM kufika hatua ya kukubali kudhoofika na hatimaye kuamua eti kujivua gamba pia kufanyika upya kwa semina elekezi.

5. Ni Chadema inayoitikisa CCM kiasi kwamba inajikuta kila siku CCM inahangaika kujaribu aidha kutoa visingizio kwa tuhuma inazozikabili au kujaribu kulinganisha tuhuma hizo na za Chadema as if "two wrongs can make a right"

6. Ni Chadema tu inayozungumzwa na hii secretariat mpya ya CCM, nani amewahi kumsikia Nape au Mukama akizungumza kuhusu CUF au TLP.

7. Chadema imeonyesha kwamba ni alternative, inakubalika na inahitajika. Imepenetrate mpaka kule kusikotarajiwa, imesemwa kuhusu ukabila, udini, ukanda na alwayz imekuwa bigger than hizi tuhuma na propaganda zenye lengo moja tu ya kuidhoofisha Chadema.

8. Everywhere you go in Tz ni Chadema, Chadema........narudia tena Bravo! Chadema.

Kwa sasa Chadema inahitaji kwenda hatua mbele zaidi, hili limeshawahi kusemwa na kutolewa ushauri na watu mbalimbali. Hatua hiyo/ hizo ziada haimaanishi Chadema iache kuendelea ku-sensitize watanzania kuhusu haki zao na hatima yao kupitia maandamano na mikutano. Bali ni hatua za kufanya ili kuipambanua Chadema tofauti na chama chochote kile cha siasa.

a. Chadema waanze kubadili mfumo wa chama chao na ikiwezekana usifanane kabisa na ule wa CCM. Mfano namna ya kuchagua viongozi, kuongoza, kuachiana madaraka, kushirikisha wanawake (sio kwa upendeleo).

b. Ile sera ya Chadema kuhusu serikali za majimbo ambayo binafsi naamini ni mojawapo ya sera bora kabisa kuweza kutukwamua na umasikini ianze kufanyiwa kazi. Mfano mipaka ya majimbo, namna ya utawala wa hizo serikali za majimbo, Viongozi wa majimbo hayo namna watakavyopatikana, Uchumi katika majimbo - Vyanzo, uzalishaji umeme, viwanda. Kifupi ni picha halisi ya hayo majimbo iwe tayari na wananchi tupewe nafasi ya kuchangia mawazo.

c. Itikadi ya Chadema iwekwe wazi na itetewe na viongozi wa Chadema na wanachama wake. Itikadi hii iwe ndiyo msingi wa kwa nini mtu ajiunge Chadema. Tofauti na CCM ambayo kwa sasa haileweki ina itikadi gani. Wao kila mahali wanajidai kuwapo.

d. Chadema ifanye harambee ya kujenga vitu flani flani ambavyo serikali ya CCM inaonekana kushindwa au kutojali mfano maktaba kubwa kuliko zote Tanzania (Of course baada ya hapo unaweza kuwapa TLS waendeshe). Bustani kubwa (Park) katikati ya mji Dodoma, Printing unit ya kisasa kwa ajili ya machapisho ya halmashauri za miji. Na mengine mengi!!!

Ni wakati muafaka sasa Chadema kusonga mbele maana inaonekana CCM kazi wameshindwa ila wako tayari kwa malumbano. Nawakilisha.
 
Haya, ndo mambo ambayo CDM, wanatakiwa kuyafanya ili kutofautiana na CHAMA CHA MAGAMBA
 
Umesomeka vyema mkuu. Ushauri wako ni mzuri na nadhani unatekelezeka sababu lengo ni kujenga msingi imara ili kuuthibitishia umma wa watz kwamba CDM inaweza hata bila ya kukadhiwa nchi.
 
Ni chama ambacho kimeonekana kuwa na mikakati ambayo hata CCM inawashangaza. Kila kukicha CCM wanaota CDM watafanya nini, maana kama acceptance wameshapata hivyo kilichobaki saizi ni kujaribu kuipoteza hiyo acceptance kabla 2015
 
Bravo Chadema! Let's move on....

Kama kuna kitu ambacho Chadema wamefanikiwa katika kipindi hiki basi ni kutimiza ile hamu ya watanzania tulio wengi kuhusu siasa. Chadema imetumbanulia haswaa kwamba pamoja na kwamba ni "official opposition" bungeni lakini pia hata mtaani. Ule utitiri wa vyama umeshakuwa kiasi fulani "obselete" na "irrelevant". It is now clear kwamba CHADEMA ndiyo chama cha upinzani na upinzani unaoishi. Hebu tuangalie yaliyojiri "in just some few months" kutoka uchaguzi uliopita.

1. Chadema imeionyesha CCM na wananchi kwa ujumla kwamba ni vyama vipi ni vya msimu kama alivyowahi kunukulia JK wakati wa kampeni kwamba "Vyama upinzani ni vya msimu" . Toka wakati huo hakuna hotuba iliyosemwa na JK bila walau kuitaja Chadema, directly or indirectly.

2. Chadema imeifanya CCM kusahau hata ilani yake ya uchaguzi na kujikuta iko bize kutekeleza yale yaliyokuwa kwenye ilani ya Chadema mfano katiba mpya. Hatujasikia tena ilani ile iliyokuwa ikinadiwa wakati wa uchaguzi ilipoishia.

3. Chadema imeilazimisha CCM, narudi "IMEILAZIMISHA" CCM kukubali kwamba ufisadi ni janga tena haswaa ndani ya CCM na serikali yake. CCM wamejikuta sasa nao eti wako bize kupambana na ufisadi.

4. Chadema imepelekea CCM kufika hatua ya kukubali kudhoofika na hatimaye kuamua eti kujivua gamba pia kufanyika upya kwa semina elekezi.

5. Ni Chadema inayoitikisa CCM kiasi kwamba inajikuta kila siku CCM inahangaika kujaribu aidha kutoa visingizio kwa tuhuma inazozikabili au kujaribu kulinganisha tuhuma hizo na za Chadema as if "two wrongs can make a right"

6. Ni Chadema tu inayozungumzwa na hii secretariat mpya ya CCM, nani amewahi kumsikia Nape au Mukama akizungumza kuhusu CUF au TLP.

7. Chadema imeonyesha kwamba ni alternative, inakubalika na inahitajika. Imepenetrate mpaka kule kusikotarajiwa, imesemwa kuhusu ukabila, udini, ukanda na alwayz imekuwa bigger than hizi tuhuma na propaganda zenye lengo moja tu ya kuidhoofisha Chadema.

8. Everywhere you go in Tz ni Chadema, Chadema........narudia tena Bravo! Chadema.

Kwa sasa Chadema inahitaji kwenda hatua mbele zaidi, hili limeshawahi kusemwa na kutolewa ushauri na watu mbalimbali. Hatua hiyo/ hizo ziada haimaanishi Chadema iache kuendelea ku-sensite watanzania kuhusu haki zao na hatima yao kupitia maandamano na mikutano. Bali ni hatua za kufanya ili kuipambanua Chadema tofauti na chama chochote kile cha siasa.

a. Chadema waanze kubadili mfumo wa chama chao na ikiwezekana usifanane kabisa na ule wa CCM. Mfano namna ya kuchagua viongozi, kuongoza, kuachiana madaraka, kushirikisha wanawake (sio kwa upendeleo).

b. Ile sera ya Chadema kuhusu serikali za majimbo ambayo binafsi naamini ni mojawapo ya sera bora kabisa kuweza kutukwamua na umasikini ianze kufanyiwa kazi. Mfano mipaka ya majimbo, namna ya utawala wa hizo serikali za majimbo, Viongozi wa majimbo hayo namna watakavyopatikana, Uchumi katika majimbo - Vyanzo, uzalishaji umeme, viwanda. Kifupi ni picha halisi ya hayo majimbo iwe tayari na wananchi tupewe nafasi ya kuchangia mawazo.

c. Itikadi ya Chadema iwekwe wazi na itetewe na viongozi wa Chadema na wanachama wake. Itikadi hii iwe ndiyo msingi wa kwa nini mtu ajiunge Chadema. Tofauti na CCM ambayo kwa sasa haileweki ina itikadi gani. Wao kila mahali wanajidai kuwapo.

d. Chadema ifanye harambee ya kujenga vitu flani flani ambavyo serikali ya CCM inaonekana kushindwa au kutojali mfano maktaba kubwa kuliko zote Tanzania (Of course baada ya hapo unaweza kuwapa TLS waendeshe). Bustani kubwa (Park) katikati ya mji Dodoma, Printing unit ya kisasa kwa ajili ya machapisho ya halmashauri za miji. Na mengine mengi!!!

Ni wakati muafaka sasa Chadema kusonga mbele maana inaonekana CCM kazi wameshindwa ila wako tayari kwa malumbano. Nawakilisha.

Kwa haya uliosema hakika ndio uhai na maendeleo ya CDM,upinzani wa kweli sio ndoa ya mkeka na chama tawala. Bravo CDM.
 
Bravo Chadema! Let's move on....
8. Everywhere you go in Tz ni Chadema, Chadema........narudia tena Bravo! Chadema.

Kwa sasa Chadema inahitaji kwenda hatua mbele zaidi, hili limeshawahi kusemwa na kutolewa ushauri na watu mbalimbali. Hatua hiyo/ hizo ziada haimaanishi Chadema iache kuendelea ku-sensite watanzania kuhusu haki zao na hatima yao kupitia maandamano na mikutano. Bali ni hatua za kufanya ili kuipambanua Chadema tofauti na chama chochote kile cha siasa.

a. Chadema waanze kubadili mfumo wa chama chao na ikiwezekana usifanane kabisa na ule wa CCM. Mfano namna ya kuchagua viongozi, kuongoza, kuachiana madaraka, kushirikisha wanawake (sio kwa upendeleo).

b. Ile sera ya Chadema kuhusu serikali za majimbo ambayo binafsi naamini ni mojawapo ya sera bora kabisa kuweza kutukwamua na umasikini ianze kufanyiwa kazi. Mfano mipaka ya majimbo, namna ya utawala wa hizo serikali za majimbo, Viongozi wa majimbo hayo namna watakavyopatikana, Uchumi katika majimbo - Vyanzo, uzalishaji umeme, viwanda. Kifupi ni picha halisi ya hayo majimbo iwe tayari na wananchi tupewe nafasi ya kuchangia mawazo.

c. Itikadi ya Chadema iwekwe wazi na itetewe na viongozi wa Chadema na wanachama wake. Itikadi hii iwe ndiyo msingi wa kwa nini mtu ajiunge Chadema. Tofauti na CCM ambayo kwa sasa haileweki ina itikadi gani. Wao kila mahali wanajidai kuwapo.

d. Chadema ifanye harambee ya kujenga vitu flani flani ambavyo serikali ya CCM inaonekana kushindwa au kutojali mfano maktaba kubwa kuliko zote Tanzania (Of course baada ya hapo unaweza kuwapa TLS waendeshe). Bustani kubwa (Park) katikati ya mji Dodoma, Printing unit ya kisasa kwa ajili ya machapisho ya halmashauri za miji. Na mengine mengi!!!

Ni wakati muafaka sasa Chadema kusonga mbele maana inaonekana CCM kazi wameshindwa ila wako tayari kwa malumbano. Nawakilisha.

Haya uliyo yapendekeza yana hitaji wewe na mimi kuwepo at frontline ndani ya CHADEMA kuyatekeleza. CHADEMA ni ya watanzania wenye maono yanayofanana so if you see fitting into these usitoe tu sugestion nenda hatua mbele seek position wewe ndani ya CHADEMA then toa pendekezo lako na thru agreement ulitekeleze ili kuifanya CHADEMA iwe jinsi tuipendavyo. nivigumu sana mtu mwingine ku implement idea ya third party maana kila tunacho kizungumza wenye akili sana wanaweza waka elewa to only not more than 50% of what you mean. Hiyo figure ni estimate tu the realy imenitoka kidogo ujue uzee nao unapiga hodi I guess!

Tukutane CHADEMA ili tuweze kuifanya i reflect our desires and wishes. CHADEMA VYEMA SANAAAAAAAAAA!
 
Kama chama pia,napendekeza tuwe na chombo cha habari aidhuru hata gazeti,radio ama Tv...tukiliweka hli sahv hakika hatutanyanyaswa tena na vyombo vyenye ubia na mafisadi,wenye kuzificha taharifa zetu na kudstort habari za chama chetu

sisi wanachama tuko tayari kuchangia kama tulivyofanya kipindi cha uchaguzi 2010 ilimradi tunapata chombo cha chama
 
Bravo Chadema! Let's move on....


a. Chadema waanze kubadili mfumo wa chama chao na ikiwezekana usifanane kabisa na ule wa CCM. Mfano namna ya kuchagua viongozi, kuongoza, kuachiana madaraka, kushirikisha wanawake (sio kwa upendeleo).

b. Ile sera ya Chadema kuhusu serikali za majimbo ambayo binafsi naamini ni mojawapo ya sera bora kabisa kuweza kutukwamua na umasikini ianze kufanyiwa kazi. Mfano mipaka ya majimbo, namna ya utawala wa hizo serikali za majimbo, Viongozi wa majimbo hayo namna watakavyopatikana, Uchumi katika majimbo - Vyanzo, uzalishaji umeme, viwanda. Kifupi ni picha halisi ya hayo majimbo iwe tayari na wananchi tupewe nafasi ya kuchangia mawazo.

c. Itikadi ya Chadema iwekwe wazi na itetewe na viongozi wa Chadema na wanachama wake. Itikadi hii iwe ndiyo msingi wa kwa nini mtu ajiunge Chadema. Tofauti na CCM ambayo kwa sasa haileweki ina itikadi gani. Wao kila mahali wanajidai kuwapo.

d. Chadema ifanye harambee ya kujenga vitu flani flani ambavyo serikali ya CCM inaonekana kushindwa au kutojali mfano maktaba kubwa kuliko zote Tanzania (Of course baada ya hapo unaweza kuwapa TLS waendeshe). Bustani kubwa (Park) katikati ya mji Dodoma, Printing unit ya kisasa kwa ajili ya machapisho ya halmashauri za miji. Na mengine mengi!!!

Ni wakati muafaka sasa Chadema kusonga mbele maana inaonekana CCM kazi wameshindwa ila wako tayari kwa malumbano. Nawakilisha.

This is what I call great thinking..Ila inatuhitaji sote kuweza ku-impliment what you proposed, CDM has shown us a way, ni wakati muafaka sasa wa wewe, mimi na sote kutoka nyuma ya key boards zetu na kufanya kazi ya kulijenga taifa letu, ambalo limedidimizwa na hawa watawala...lets take charge, we will be there...:pound::director:
 
Dah,...
aisee mkuu nakupa heshima zako!
natamani ningekua kiongozi wa chadema,haya mapendekezo a-d ninge yachukua yoote
na kuanza namna hii:-

1.chadema wana pendekeza sera ya majimbo,kwa mda huu ambapo wao ndio
chama kikuu cha upinzani,na wana wabunge karibia kila "jimbo" au "kanda" basi wange
pewa majukumu katika majimbo/kanda zao ili kuiongezea chadema imani hata kwa majimbo
ambapo hawakushinda au hawa kusimamisha mgombea.

2.Hoja ya maktaba/liblary za mkoa,..
kama alivo sema Dr.Slaa kwenye kampeni zake,..huu ndo mda wa kuonesha kwamba
angefanya alicho ahidi mda ule kweli,...
alisema "raisi atakua anaenda kwenye maktaba za mkoa zitakazo jengwa na serikali kusoma na
watoto,na hii itawapa ari watoto kujijengea hamu ya kusoma".
now that hawajashika madaraka,pamoja na pendekezo lako la kufanya harambee ya kujenga maktba,bado
wanaweza kufanya walicho ahidi,kwa mfano!

wana weza kupanga,either kama group la wabunge wote,au viongozi au slaa
akaenda kuvisit maktaba ya mbeya pale kwa mfano,kuna watoto wanasoma maktaba,..na hiyo itakua
inaonesha how valid his promise was,...
atoe tangazo kwamba next month ntakua kwenye library ya mkoa dar,sio iwe kisiaaasa kujaza watu library,itaonekana unafanya siasa hadi library.

Hata wale wachache watakao kuwepo tu inatosha kwenda kuwapa moyo,...
of course,kipengele "d" chote nime kipenda sana
Dr.Slaa,you promised this,...you can do it now!

3.kuhusu uchaguzi ndani ya chama,
ufanyike uchaguzi huru na wa haki ambao ndio tunalia kuukosa NEC,
asibebwe mtu kwa sababu yoyote ile.
mchakato uwe wa uwazi,sio mtu akitokea kuchukua form kama enzi zile zitto,wazee wanakaa
kusema sijui nini,that is CCM's game,..
sikutaka zitto awe mwenyekiti,ila that time yeye kujiondoa akabaki mbowe peke yake
haikua demokrasia ndani ya chama kinacho jiita cha demokrasia!

Now,uchaguzi unaokuja wa vijana ni mda wa kuonesha kwamba chaguzi zote
zijazo ndani ya chadema zitakua za haki,..
kwa nyongeza tu,wekeni chachu ya midahalo ya wagombea,...
ili hata inapo fika mda wa uchaguzi mkuu,watu wawe wamezoe midahalo kwenye
uchaguzi na atakae kimbia mdahalo apimwe udhaifu wake tokea hapo!

Asante sana kwa topic mkuu
 
Great analysis, Chadema now rules Tanzania ndio maana wapinzani wake wanazidi kuongezeka kama jana naye Dovutwa kaingia kuipinga cdm, swali ninalojiuliza mbona Dovutwa, Lipumba, Mrema, Aliyefulia, Nape, nk wote wanaiandama cdm? Wanazidi kuipa cdm nguvu ya kujiandaa 2015 viva CDM
 
Haya uliyo yapendekeza yana hitaji wewe na mimi kuwepo at frontline ndani ya CHADEMA kuyatekeleza. CHADEMA ni ya watanzania wenye maono yanayofanana so if you see fitting into these usitoe tu sugestion nenda hatua mbele seek position wewe ndani ya CHADEMA then toa pendekezo lako na thru agreement ulitekeleze ili kuifanya CHADEMA iwe jinsi tuipendavyo. nivigumu sana mtu mwingine ku implement idea ya third party maana kila tunacho kizungumza wenye akili sana wanaweza waka elewa to only not more than 50% of what you mean. Hiyo figure ni estimate tu the realy imenitoka kidogo ujue uzee nao unapiga hodi I guess!

Tukutane CHADEMA ili tuweze kuifanya i reflect our desires and wishes. CHADEMA VYEMA SANAAAAAAAAAA!

Mkuu shukrani for ur comment, ila wazo la kuseek position ndani ya Chadema kwa sasa nadhani umeenda mbali kidogo kwanza kwa kudhani au kuamini mimi ni mwanachama wa Chadema lakini fact mimi si mwanachama wa chama chochote na pia sidhani kama Chadema wana "position" nyingi kiasi hicho kiasi kwamba kila anayetoa wazo kuhusu wao basi apewe position kuimplement. Mimi ni mpenda mabadiliko na siyo siri siipendi CCM.

Nna uhakika kuna viongozi wa CDM humu wanaweza kuwasiliana nami kama wanahitaji maelezo ya ziada kuhusu my proposals!
 
Great analysis, Chadema now rules Tanzania ndio maana wapinzani wake wanazidi kuongezeka kama jana naye Dovutwa kaingia kuipinga cdm, swali ninalojiuliza mbona Dovutwa, Lipumba, Mrema, Aliyefulia, Nape, nk wote wanaiandama cdm? Wanazidi kuipa cdm nguvu ya kujiandaa 2015 viva CDM

wanatafuta kupanda mjuu kwa mgongo wa chadema,

historia inaonesha watashindwa maana:-
walikuja kina kafulila wakafulia kweli,..
kina hamad nao walianza sijui wamepotelea lamadi?
lipumba nae alijitahidi kuzunguka nchi kutema pumba,watu wakamuona pumba,...
mbatia alianza kufuka kama moshi,saivi kabanwa mbavu yuko kimya,..
mrema alilopoka mda mlani,saivi sijui analima nini,..
mtatiro alilia lia,saivi yupo kwenye mitaro tu,..
na huyu dovutwa nae,haha kesho ataanza kutoka povu!
 
Mkuu shukrani for ur comment, ila wazo la kuseek position ndani ya Chadema kwa sasa nadhani umeenda mbali kidogo kwanza kwa kudhani au kuamini mimi ni mwanachaa wa Chadema lakini fact mimi si mwanachama wa chama chochote na pia sidhani kama Chadema wana "position" nyingi kiasi hicho kiasi kwamba kila anayetoa wazo kuhusu wao basi apewe position kuimplement. Mimi ni mpenda mabadiliko na siyo siri siipendi CCM.

Nna uhakika kuna viongozi wa CDM humu wanaweza kuwasiliana nami kama wanahitaji maelezo ya ziada kuhusu my proposals!

Hawa jamaa wako makini sana,mda mwingi wana kuwa hapa kuchukua maoni,..
sina uhakika sana wa jinsi yanavo fanyiwa kazi,ngoja niwapime kwa mawazo yako niwajue
 
Hivi kwanini watu kama wewe CCM hawakujaaliwa! Ungekuwa unapenda na Ka-Ufisadi kidogo, ningekushauri uende CCM ukawaamshe lakini ndio hivyo tena, bila kuwa fisadi wewe hawakutaki kwani si mmoja wa Magamba.
 
Back
Top Bottom