BOT na pesa mpya vipi?

BOT na pesa mpya vipi?

Ni heri wabadilishe noti ya sh elfu kumi iwe ktk mfumo wa sarafu na sarafu ya sh 200 iwe ndo noti vivyo hivyo kwa noti ya sh elfu tano na elfu mbili natumai hapo uchakachuaji utakwisha.Kwa sababu haitakuwa rahisi kugushi sarafu ya sh elfu kumi na pia mtu hawezi kujiangaisha kwa ajili ya kugushi noti ya sh mia mbili. Ni mtazamo wangu.

Duh,Mkuu hii mpya.Lakini ulishawahi kusikia kuhusu shillingi mia za sarafu zilivyokuwa zinaghushiwa?
 
Mara nyingi tumekuwa wagumu kuelewa somo. Umeambiwa pesa hizi zina ubora zaidi na zina security features ambazo haziwezi kughushiwa kiurahisi lakini hatuelewi. Au mtu akivaa sarawili ya kitambaa kizito ndo anakuwa amevaa nguo yenye ubora. Hizi hela niza kisasa zaidi isipokuwa matumizi yetu ndo mabaya. Mfano; mnaenda kanisani kutoa sadaka mmekunja noti, mnaficha noti sehemu za siri zinapata ukungu, wengine wanachimbia pesa chini ya shimo, wengine wanazikunja kwenye pembe za kanga, hatutumii wallet, mikono yetu inakuwa na unyevu wa maji na jasho lakini tunashika pesa. Hayo ni baadhi tu ya matumizi mabaya ya pesa zetu. Ukiangalia American Dollar---huwezi kuikunja kwa sababu unajua inaweza kukataliwa either na benki au ikagoma kupita kwenye mashine ndo maana mnazitunza vizuri.
Mie nakubaliana na Ndullu kabisa kuwa hizo noti ni bora kabisa kuliko zote zilizowahi kutoka hapa TZ.

Kwa vigezo vipi mkuu?Watu wamekuonesha matatizo ya hizo noti wewe bado unakomaa ni bora,mbona hawaziondoi kwenye mzumnguko zile za zamani kama walivyoahidi ili zibaki hizo mpya tu?Inawezekana upo ughaibuni na haujawahi kuzishika hizi noti.
 
Kibaya zaidi hata mkuu wa nchi walimdanganya akaishia kushangaa mirangi ya kun'gaa bila ya kutambua si kila king'aacho ni dhahabu. Yaani fedha ni za kichovu mno hazina ubora....kwa nchi makini lazima mtu ang'oke.
 
Tumsubiri Beatrice Shelukindo aje na hili pia hapo Bungeni kabla ya Ijumaa 26th August 2011
 
Kwani lazima tutumie mpya! Wangeziacha hizo hzo za zamani.
 
Back
Top Bottom