KERO BoT Changamoto ya chenji na mzunguko wa Pesa za Sarafu, je kuna nini kinaendelea?

KERO BoT Changamoto ya chenji na mzunguko wa Pesa za Sarafu, je kuna nini kinaendelea?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

tzvicto.2014

New Member
Joined
Sep 15, 2014
Posts
2
Reaction score
2
Wadau, hivi karibuni nimeshuhudia changamoto kubwa ya fedha za sarafu hasa za Tshs 200, 100 na 50.

Biashara nyingi sasa hivi ni ugomvi kutorudishiwa chenji kwasababu ya kutokuwepo na sarafu.

Binafsi nimefuatilia maduka makubwa hadi sasa yanadiriki kujaza pipi na big G kwenye madroo ya fedha ambazo hutumika kama chenji

Nimeshajaribu kuomba sarafu mabenki ila wao pia hawana

Je, BoT wanaweza kufafanua hii changamoto kulikoni?

Kusema kweli ni kero kwenda dukani na kurudishiwa pipi au big G ambazo mtu hauzihitaji.

BoT tufafanulieni hii changamoto ni kero kwa wananchi.

IMG_7217.jpeg
 
Back
Top Bottom