Nilimpata mwanamke tu nilipomaliza masomo yangu tumekuwa wote kwenye mahusiano Kwa muda wa mwez mmoja sasa
Lakin nimechoka kabisa huyu mwanamke tukitoka labda kwenda sehemu muda wote kaniganda kama tumefungwa kamba hata nikimwambia subir hapa nikojoe lazima anifuate aangalie kwel mkojo unatoka? Akipita dukan kununua kitu hata vocha hatak utangulie umsubir ukitangulia kidogo tu kelele nyuma ohh my mbona unaniacha my simama my simama jamani mimacho ya watu njian yote kwangu mpaka naogopa hapo maswal bado hajakuuliza kwann umeniacha ananishika begani mara kiunoni kero sasa huu mzigo nitautuaje me
Hata kama mapenzi siyo haya najuta akija ghetto nikitoka kidogo tu simu inapigwa usipopokea au upokee then uchelewe kuongea utamkuta macho mekundu amelia weeeee mpaka bhas akikuhitaji hata saa nane za usiku uende usipoenda atatuma sms mpaka asbh analalamika et anaumia........
Nisaidie naona kama mapenzi yapo hivi bora niachane nayo niondoe visababishi vya mambo yote haya
Mkuu ngoja nikwambie kitu Cha kuzingatia sana.
Yaani jinsi ulivyoelezea nimekuelewa vzr sana kwa sababu situation Kama hiyo iliwahi kunikuta miaka ya nyuma.
Unatakiwa utumie akili nyingi sana na busara,ukifuata ushauri wa vijiweni unakwenda na maji.
Ni hivi huyo mwanamke amekupenda kupitiliza ndio maana anatumia kila namna ili kukulinda usichukuliwe na watu wengine.
Na kukupenda kwake kunatokana na moja Kati ya mambo yafuatayo.
1.Imetokea tu moyo wake amekutunuku au
2.Ameangalia future yako na amegundua kuwa utakuja kuwa ni mtu mwenye viwango vya juu vya maisha Kama bado hujafikia viwango hivyo kwa hiyo anaamini wewe ndio utakuja kuwa msaada wa pekee kwake.
Sasa kawaida ya watu Kama huyo huwa wakiachwa hawawezi kuvumilia hiyo situation na huamua kujiua.
Kwa hiyo hata Kama utamuacha Basi iwe kwa pole pole Hadi akusahau ila isiwe ghafla.
Ukikosea hizo hesabu utakuja kupata kesi usiyoitarajia.
Mimi nishawah kutokewa na watu wawili tofauti Kama hao wote walikunywa sumu lkn bahati nzuri ndugu zao waliwawahi wakapona.