Bora nikate tamaa ili niwe salama

Bora nikate tamaa ili niwe salama

Daviie

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2016
Posts
1,292
Reaction score
1,482
Nlipokuwa mdogo (before 20yrs) ilikuwa kila nikitaka kitu nikapima na kuamini naweza kuwa ama kupata basi ilikuwa ni lazima nifanikishe ningeacha vyote nifocus na hicho tu mpaka ieleweke. Sasa nimekuwa mkubwa bado ni mtu wa strong desires yaani nikitaka nimetaka akili yangu itaumia kutafuta namna ya kufanikisha ninachotaka kwa nguvu zote lakini mambo yamekuwa magumu mno hayaji kirahisi na si tu kirahisi bali hata kwa nguvu zote ninazoapply ambazo nilipima nikaona inawezekana lakini mambo hayawezekani.

Maisha yangu ni kama yamesimama, mateso yanaongezeka , changamoto hazivumiliki (ugonjwa/ulemavu) nimeshindwa kufanikisha nilivyofikiri itawezekana lakini nashindwa kupotezea na kumuachia Mungu. Msemo wa Mungu hachelewi wala hawahi haufanyi kazi kwangu, siwezi kabisa vumilia zaidi kuendelea na maisha ya hivi lakini nifanye nini sielewi, nikweli ninayoyataka yapo nje ya uwezo wangu, mengine nje ya uwezo wa binadamu lakini napata machungu kuona kwanini isiwe yaani milango yote imefungwa sasa nitokee wapi, halafu kwanini iwe mimi tu?

Agrrrh... Nahisi kuchanganyikiwa! hii strong desire ya kuwa mtu fln kuishi katika level fln licha ya hali yangu sasa inanitesa vilivyo. Nikikaa kutwa nzima kichwa kinawaka moto nifanya nini na kila ninachoamini nikijaribu sifanikiwi, sitakiwi kuwa hapa nilipo, sitakiwi kuishi hivi, Huu ni mtihani mzito sana kwangu. Nawaza pengine uzito hasa unakuja kutokana na aina ya mtu niliye. Bora ningekuwa mtu nisiyeamini katika mafanikio, kama ningekuwa mtu wa kukubali kushindwa walahi nisingeteseka hivi pengine ningekuwa cool nimemwachia Mungu lakini kiukweli nimeshindwa kukata tamaa.

Nimejaribu kujiwekea miiko kwamba No social networks hasa hasa FB, whatsap groups labda zinaniongezea anxiety kwasababu kule wengi ninaowahamu naona ni kama wote wameridhika wanafurahia maisha yao. Nikiwaza hivi kweli namimi niridhike na hali hii BIG NO! Nikasema wacha niachane na mambo ya Inspirations, Motivations huko IG nikiingia watu wanafanya big moves, hata wauza sura wanaoshine kwa kufake life still wanaEnjoy life, wakina Ontario kila siku kutusema tunaosindikiza maisha, Quote yake moja anasema "Maisha hayajawahi kuwa selective, hayajui kama baba yako ni maskini au wewe ni kilema, kipofu, yatima. Maisha ni kama mvua ikinyeesha haiangalii kama kuna mtu kaanika mpunga, kuna mtu anajenga nyumba, kuna mtu anaanika nguo, haiangalii chochote same as life.

Ni jukumu lako kuwa na mwamvuli " Basi nikiona hivyo moyo unauma sana naona bora nihamie kwenye kushabikia udaku na story za kina Mondi kusogeza siku lakini nazo zinachosha big times. Sina rafiki, sina mpenzi wala sidhani kama nataka kuwa nao kwasasa maana hata marafiki niliokuwa nao hatumatch tena kama zamani na urafiki umefifia. Sifurahii kabisa kuishi hivi, bila kuwa ninavyotaka seriously sijioni kuumaliza mwaka 2020.

Nimekosa alternative ya vipi nibadili attitude niliyonayo, niiambie nini nafsi yangu ili iridhike akili yangu itulie just to be calm and patient nisisumbuke tena kujiwazia chochote. Kama kuhold endurance nimehold sana nimefika mwisho kabisa sasa nahisi hata naweza kujifanyia kitu kibaya. Two times this year nilichukua hatua kadhaa toward self suicide lakini nikaghairi na kuishia kutokwa na machozi, nilimfikiria mtu mmoja anayenipenda sana lakini hana namna ya kuweza kunisaidia. Nahisi nguvu kubwa inanivuta kwenye self suicide kwakuwa seriously sioni care wala love kutoka kwa watu wanaopaswa kunicare na mimi ni mzigo wao.

Lakini siyo makosa yao pengine wanahisi I'm strong to handle the situation by myself. Should I tell them I need more love and care from them than this how they take me for granted now? Masculinity feelings stops me. Nahisi mwanaume sitakiwi kuomba mtu anipende wala siwezi kulazimisha mtu anijali. Is this right? How can I change this attitude. I feel worthless hilo halipingiki na tatizo langu hasa ni kutambua hilo. How can I fix this? Haya mawazo yasije kuniletea brain tumor ni bora nikubali kushindwa, nikate tamaa lakini nawezaje? Nitaweza kweli kujitenga na kila kitu, kila mtu? Si ndo mwisho wa siku nitajua mimi .

Lakini nitaweza kweli kuassociate na society katika hali tofauti nikiwa mtu wa chini ninayehisi kupoteza thamani niliyokuwa nayo mwanzo ? Sipendi kuwa looser, well nimekuwa looser lakini sipendi kuonekana kama looser, sipendi kuwa worthless hivi. Dah, masikini mimi... Bora nikate tamaa!
#badmood #disabilityfeelings #poverty
 
Daah pole sana mkuu..hicho kipind unachopitia wengi tunapitia..ila usikate tamaa cha muhimu wekaa mipango kwa muda...hata kama ni kidogo kidogo .iko siku utafikia malengo yako hata kama ni mzee..usipende kila kitu ufanikiwa on the spot..pia usimsahau mfariji wa kwel Mungu wako
 
umeandika kwa uchungu sana . kama nakuona masikini . pole sana . unawakilisha wengi wanaofikiria kukata tamaa au waliojikatia tamaa tayari. but take this from me , never give up . pambana mpaka mwisho na mungu yupo usichoke as long as una pumzi bado pambana mkuu. binadamu tumeumbiwa yote hayo unayopitia . dont feel you are worthless, u are a winner just never give up. angalia wapi pakurekebisha songa mbele usiangalie watu watakuchukuliaje hapo ndo utafeli .
 
Unahitaji Upendo na caring kubwa sana
Natamani nikusimulie story Fulani but I have changed someone's life aliyekua na same situation.
Na naamini atafika mbali Sana zaidi ya hapo
Kikubwa amini maisha ni zawadi na anayetupa Ana kusudi.
 
daah pole sana mkuu..hicho kipind unachopitia wengi tunapitia..ila usikate tamaa cha muhimu wekaa mipango kwa muda...hata kama ni kidogo kidogo .iko siku utafikia malengo yako hata kama ni mzee..usipende kila kitu ufanikiwa on the spot..pia usimsahau mfariji wa kwel Mungu wako
sawa mkuu nafahamu kanuni ya kidogo kwa kidogo lakini mipango yenyewe naipanga huku afya yangu inadhoofu nitafika kweli
 
Maisha hayatakaa yatosheleze. Hivyo ni budi na kushukuru kwa ulichonacho. Those who are the happiest never did have everything, but they are thankful for everything they do have.

When you learn to appreciate the little you have, then the big things are soon to happen. Please learn to be grateful.

Anza kwa kushukuru na kufurahia pumzi uliyonayo, shukuru kwa amani, shukuru kwa kila kitu huku ukijilinganisha na wasio nacho kabisa na utapata amani ya moyo sana.

Then, lower or have less expectations from someone and you will never be disappointed. If you love someone, then don't expect to be loved back. If you give, don't expect the return. If you help, don't expect a thankful hand. On whatever you do to others, have no expectations. You will have peace within you.
 
Zaid ya 65% ya waTz wanapitia hii hali..
jikubali Mzee upigie life maana maisha ndo hayahaya ..
Pambana Mzee hiyo desire ya kupata unachotaka itumie as a tool , mafanikio hayata kuacha
Mzeebaba itakuwa hujanielewa tu, yaani natamani sana kupambana lakini kuna ugonjwa umeniweka ndani aisee daaah yaani nikiwaona wanaopambana huko nje nahisi kupasuka maana namimi ningekuwa mmoja wao na hakika ningetoboa lakini ugonjwa umenipiga kabali ndomaana hata nataka nikate tamaa nisifocus tena yanayoendelea huko nje just niwe kama sipo vile nikubali tu kuwa siwezi kuwa kama nyinyi wazima
 
Mkuu pole sana ...unaumwa nn labda unaweza pata msaada hata mawazo ya kutoka apo ulipo
 
Mzeebaba itakuwa hujanielewa tu, yaani natamani sana kupambana lakini kuna ugonjwa umeniweka ndani aisee daaah yaani nikiwaona wanaopambana huko nje nahisi kupasuka maana namimi ningekuwa mmoja wao na hakika ningetoboa lakini ugonjwa umenipiga kabali ndomaana hata nataka nikate tamaa nisifocus tena yanayoendelea huko nje just niwe kama sipo vile nikubali tu kuwa siwezi kuwa kama nyinyi wazima
Kama hutojali, waweza kuzungumza nasi kuhusu huo ugonjwa. Unaweza kupata msaada.
 
Mzeebaba itakuwa hujanielewa tu, yaani natamani sana kupambana lakini kuna ugonjwa umeniweka ndani aisee daaah yaani nikiwaona wanaopambana huko nje nahisi kupasuka maana namimi ningekuwa mmoja wao na hakika ningetoboa lakini ugonjwa umenipiga kabali ndomaana hata nataka nikate tamaa nisifocus tena yanayoendelea huko nje just niwe kama sipo vile nikubali tu kuwa siwezi kuwa kama nyinyi wazima

Maana nzima ya thread iko hapa, ila umetumia maneno mengi sana kuelezea kiasi cha kupoteza lengo.

Pole sana.
 
Maana nzima ya thread iko hapa, ila umetumia maneno mengi sana kuelezea kiasi cha kupoteza lengo.

Pole sana.
Dah kweli mkuu inawezekana naanza kuyumba stress zinaniendesha lakini najaribu tu kupunguza sumu pengine hata sijui kama nimeandika kutafuta msaada au nimeandika kwasababu gani mnisamehe bure kuwaandikia ujumbe mrefu usioeleweka
 
Nlipokuwa mdogo (before 20yrs) ilikuwa kila nikitaka kitu nikapima na kuamini naweza kuwa ama kupata basi ilikuwa ni lazima nifanikishe ningeacha vyote nifocus na hicho tu mpaka ieleweke. Sasa nimekuwa mkubwa bado ni mtu wa strong desires yaani nikitaka nimetaka akili yangu itaumia kutafuta namna ya kufanikisha ninachotaka kwa nguvu zote lakini mambo yamekuwa magumu mno hayaji kirahisi na si tu kirahisi bali hata kwa nguvu zote ninazoapply ambazo nilipima nikaona inawezekana lakini mambo hayawezekani.

Maisha yangu ni kama yamesimama, mateso yanaongezeka , changamoto hazivumiliki (ugonjwa/ulemavu) nimeshindwa kufanikisha nilivyofikiri itawezekana lakini nashindwa kupotezea na kumuachia Mungu. Msemo wa Mungu hachelewi wala hawahi haufanyi kazi kwangu, siwezi kabisa vumilia zaidi kuendelea na maisha ya hivi lakini nifanye nini sielewi, nikweli ninayoyataka yapo nje ya uwezo wangu, mengine nje ya uwezo wa binadamu lakini napata machungu kuona kwanini isiwe yaani milango yote imefungwa sasa nitokee wapi, halafu kwanini iwe mimi tu?

Agrrrh... Nahisi kuchanganyikiwa! hii strong desire ya kuwa mtu fln kuishi katika level fln licha ya hali yangu sasa inanitesa vilivyo. Nikikaa kutwa nzima kichwa kinawaka moto nifanya nini na kila ninachoamini nikijaribu sifanikiwi, sitakiwi kuwa hapa nilipo, sitakiwi kuishi hivi, Huu ni mtihani mzito sana kwangu. Nawaza pengine uzito hasa unakuja kutokana na aina ya mtu niliye. Bora ningekuwa mtu nisiyeamini katika mafanikio, kama ningekuwa mtu wa kukubali kushindwa walahi nisingeteseka hivi pengine ningekuwa cool nimemwachia Mungu lakini kiukweli nimeshindwa kukata tamaa.

Nimejaribu kujiwekea miiko kwamba No social networks hasa hasa FB, whatsap groups labda zinaniongezea anxiety kwasababu kule wengi ninaowahamu naona ni kama wote wameridhika wanafurahia maisha yao. Nikiwaza hivi kweli namimi niridhike na hali hii BIG NO! Nikasema wacha niachane na mambo ya Inspirations, Motivations huko IG nikiingia watu wanafanya big moves, hata wauza sura wanaoshine kwa kufake life still wanaEnjoy life, wakina Ontario kila siku kutusema tunaosindikiza maisha, Quote yake moja anasema "Maisha hayajawahi kuwa selective, hayajui kama baba yako ni maskini au wewe ni kilema, kipofu, yatima. Maisha ni kama mvua ikinyeesha haiangalii kama kuna mtu kaanika mpunga, kuna mtu anajenga nyumba, kuna mtu anaanika nguo, haiangalii chochote same as life.

Ni jukumu lako kuwa na mwamvuli " Basi nikiona hivyo moyo unauma sana naona bora nihamie kwenye kushabikia udaku na story za kina Mondi kusogeza siku lakini nazo zinachosha big times. Sina rafiki, sina mpenzi wala sidhani kama nataka kuwa nao kwasasa maana hata marafiki niliokuwa nao hatumatch tena kama zamani na urafiki umefifia. Sifurahii kabisa kuishi hivi, bila kuwa ninavyotaka seriously sijioni kuumaliza mwaka 2020.

Nimekosa alternative ya vipi nibadili attitude niliyonayo, niiambie nini nafsi yangu ili iridhike akili yangu itulie just to be calm and patient nisisumbuke tena kujiwazia chochote. Kama kuhold endurance nimehold sana nimefika mwisho kabisa sasa nahisi hata naweza kujifanyia kitu kibaya. Two times this year nilichukua hatua kadhaa toward self suicide lakini nikaghairi na kuishia kutokwa na machozi, nilimfikiria mtu mmoja anayenipenda sana lakini hana namna ya kuweza kunisaidia. Nahisi nguvu kubwa inanivuta kwenye self suicide kwakuwa seriously sioni care wala love kutoka kwa watu wanaopaswa kunicare na mimi ni mzigo wao.

Lakini siyo makosa yao pengine wanahisi I'm strong to handle the situation by myself. Should I tell them I need more love and care from them than this how they take me for granted now? Masculinity feelings stops me. Nahisi mwanaume sitakiwi kuomba mtu anipende wala siwezi kulazimisha mtu anijali. Is this right? How can I change this attitude. I feel worthless hilo halipingiki na tatizo langu hasa ni kutambua hilo. How can I fix this? Haya mawazo yasije kuniletea brain tumor ni bora nikubali kushindwa, nikate tamaa lakini nawezaje? Nitaweza kweli kujitenga na kila kitu, kila mtu? Si ndo mwisho wa siku nitajua mimi .

Lakini nitaweza kweli kuassociate na society katika hali tofauti nikiwa mtu wa chini ninayehisi kupoteza thamani niliyokuwa nayo mwanzo ? Sipendi kuwa looser, well nimekuwa looser lakini sipendi kuonekana kama looser, sipendi kuwa worthless hivi. Dah, masikini mimi... Bora nikate tamaa!
#badmood #disabilityfeelings #poverty
Kuna mdau mmoja huku alichangia uzi wa kifo cha Ali Mufuruki kwa kusema nanukuu “Kuna nyakati maisha yanakosa maana”. Ni kweli kabisa maisha ni zaidi ya tunavyofikiria kama wanadamu kwa imani yangu. Maisha ya kila mtu yamepangwa kabla kabisa na Mungu. Baada ya wewe kutekeleza lile lililokuleta hapa duniani unaondoka. Hizi stori za kwamba nitafute pesa,nijenge nyumba nzuri ni mipango yetu sisi wanadamu ila kwa Mungu halipo hivyo. Pia sijui unatumia kipimo gani kusema wewe upo situation mbaya,kuna watu wako vibaya achaa. Ushauri acha kuona huishi mpaka upate pesa,shukuru Mungu kwa kila jambo,kwani hamna mwanadamu mwenye uwezo katika haya maisha zaidi yake
 
Back
Top Bottom