View attachment 1550294
Baada ya kumsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Bara,kamanda Bensoni Kigaila, nimepoteza hata hamu ya kufuatilia uzinduzi wa kampeni kwani kwa idadi ya wagombea wa ubunge wa CHADEMA walioenguliwa mpaka sasa, naweza kusema inatisha huku msemaji mwenyewe akiweka wazi kuwa idadi ya wanaogombea udiwani ndio kubwa zaidi na angesema aiongelee, basi angetumia muda mrefu sana.
Mazingira haya kwangu mimi yananiondolea kabisa hata ile hamu ya kufuatilia huo uzinduzi kwani naona hawa mabwana kwa sasa ni kama wanatuchora tu.
Ushauri wangu ni bora kupambana kwanza juu ya hili kabla hamjaendelea na huo uzinduzi kwani hai-make sense kufanya uzinduzi huku wagombea ubunge zaidi ya 50(kwa maelezo ya Kigaila) kwa tiketi ya CHADEMA wakiwa katika hatihati ya kukosa nafasi ya kuwa wagombea huku idadi ya wagombea udiwani nchi nzima ikiwa ni kubwa zaidi.
Ni bora uongozi wa CHADEMA Taifa mkalipa uzito jambo hili vinginevyo mtavunja moyo wenzenu ambao wako katika hatihati ya kukosa haki yao ya kikatiba ya kuchagua na kuchaguliwa.
Napata wasiwasi kuwa huenda hata huo uzinduzi nao ukahujumiwa kama wagombea wetu walivyohujumiwa.
Hata hivyo, naungana na Bensoni Kigaila kwa aliyoyasema na kwakweli ametoa onyo kali kuhusu hujuma hizi na ninaona kuna giza nene huko mbeleni iwapo busara itakosekana hasa kwa wenye mamlaka.
Tuombe Mungu kwani "tone" ya Kigaila haikuwa ya mchezo na ni wazi wamedhamiria kudai/kutafuta haki kwa gharama yoyote.