Kiby
JF-Expert Member
- Nov 16, 2009
- 6,897
- 4,620
Ee bana eh! Nilikua nafuatilia mkutano wa mgombea urais wa jamhuri ya Tanzania kwa tiketi ya chadema, na macho yangu yakamwangukia sheikh mwaipopo akiwa amekaa kwenye viti vya wageni waalikwa. Hebu tusaidiane jamani na hasa kwa wale waliokaribu na protokali ya Chadema, amefikafikaje pale? Amealikwa tu kama kiongozi wa kidini ambayo ni haki yake au ni kwa maslahi ya kisiasa? Kama ni ya kisiasa basi chadema mkoa muwe macho huyu jamaa ni mtaalamu wa kula na mikono yote miwili tena bila hata kunawa. Yeye kwa mwezi mmoja anawezakuwa mwanachama wa vyama vinne tofauti. Ukija ugomvi wa matajiri kama wakati fulani huko nyuma kati ya Mengi na RA huyu mwaipopo alilamba mshiko kote kote. Kwenye sakata la mfanya biashara mmoja jijini na kiwanja cha waislamu alilamba toyota korolla. Hivyo watu wa namna hii ni wa kuwa nao makini kwani mwaka huu wa uchaguzi ni wa mavuno kwao.