Kulalamika si kujenga.
Hapa tutatizama video za wasanii wa Tanzania (hasa Bongo Fleva), ubora, upungufu na vyote ambavyo vinaweza kuonekana na ikiwezekana kushauri cha kufanya ili kuboresha tasnia hii ya video hapa nchini.
Kwa kuanza nimeichagua video ya wimbo 'Nivute Kwako" ulioimbwa na Dayna kwa kushirikiana na Barnaba, wote wakiwa wanatokea THT.
Video hii imefanywa na Adam Juma kupitia project ya Next Level.
Ni kati ya video ambazo zina sura ya Kiafrika ndani yake, imefanywa mahala fulani kwenye mazingira ya asili kabisa. Wahusika wamejitahidi kucheza na kamera vizuri isipokuwa huyu mwanaume ambaye ni mhusika mkuu, pozi zake zinamfanya aonekane kama 'sex machine', kitu ambacho kinatoa picha hasi hivi.
Wakaka na wadada wanaocheza wamependeza sana tu, na wamefanya group dancing nzuri sana.
Kuna kama idea mpya hivi, wasanii walioshirikiana si lazima wakaribiane-karibiane ndio video ya mapenzi ipendeze. Huu ni ubunifu wa pekee katika video za ki-Tanzania.
Cha mwisho nilichokipenda ni kuwa hakuna hali ya watu (wasichana) kujianika hovyo kama ilivyozoeleka (nudity), ni video ambayo watu wa marika yote wanaweza kutazama bila tatizo.
Video yenyewe ndio hiyo hapo juu, unaweza kuongeza uliyoyaona humu ambayo unahisi sijayazungumzia.
Ni wimbo huu.
Jamaa anaitwa Omari Dimples akishirikiana na Ali KIBA. Video yake ni nzuri sana,hasa kwa kuwa ni wimbo ambao umempatiaa tuzo mbili kwenye KTMA, ina pozi tofauti miksa costume za humo sio zile za ki-Cabo Snoop, something I like, pia Kiba na Omari wamecheza vizuri na kamera miksa vocals za hatari sana.
Dimpoz amependeza, kisasa zaidi na Ali Kiba kama kawaida yake, huwa haongozwi na hisia za fashion, anavaa vinavyompendeza siku zote, and he's good. Mercedez Benz za humu ni hatari sana, kama sio Bongo vile, plus pozi flani za kimamtoni za kutembea na 'pet dog' zimeifanya video ikae kimamtoni zaidi. Dancers wa mule, ambao nimeambiwa kuwa wanaitwa Dimpoz kwa Poz wametisha ile mbaya, kitu kinachoipa mvuto wa ziada video hii.
Tatizo langu lipo kwenye model wa video, hana kabisa viwango vya wimbo wenyewe, to be honest!
Ni demu wa kawaida, anaonekana ameenda umri kuliko kawaida, halafu amejichubua plus muonekano wa kikahaba, she ruined the video kwa kweli.
Tuishie hapo, next time nitawaeleza jinsi Hemed Ph.D alivyoboa kadiri ya uwezo wake.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.