Bongo Movie inaonekana hawajui Kiswahili

Bongo Movie inaonekana hawajui Kiswahili

michael western

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2014
Posts
544
Reaction score
259
Yaani kuandaa movie ni process ndefu, ila unakuta mpaka majina ya movie ya hovyo, mi nikiona jina la movie au wimbo siyo kiswahili sanifu sina hamu tena kuangalia najua tu walioandaa ni vilaza.

Kuna movie inaitwa "Milembe" ila maudhui ni Mirembe. Kuna moja "Chizi karogwa tena". Nadhani kiswahili sanifu ni "Chizi kalogwa tena".

Tuna waigizaji vilaza.
 
Mawani, karogwa yote ni maneno ya Kiswahili inategemea umetokea wapi.

Mawani ni neno la kizamani sana, na marehemu Bi Kidude akilitumia hilo neno kumaanisha miwani.

Na visiwani Unguja na Pemba tunatumia karogwa na siyo kalogwa.
 
Hlf sijui huwa hawawezi kuongea lugha moja mwanzo mwisho. Yaan utakuta wanachanganya changanya tu,mara kiswahili mara kingereza.
 
Yaani kuandaa movie ni process ndefu, ila unakuta mpaka majina ya movie ya hovyo, mi nikiona jina la movie au wimbo siyo kiswahili sanifu sina hamu tena kuangalia najua tu walioandaa ni vilaza.

Kuna movie inaitwa "Milembe" ila maudhui ni Mirembe. Kuna moja "Chizi karogwa tena". Nadhani kiswahili sanifu ni "Chizi kalogwa tena".

Tuna waigizaji vilaza.

n ww chiz kwny r unawek l,n vice vesa
tazam kwnz boriti kwny jicho kisha ndo umtoe kibanzi
 
Ukweli ni kwamba watanzania wengi hawajui kiswahili sanifu. Hata kwenye radio na tv zote tatizo ni hilo hilo. Hivi sasa tunashindwa na kenya na rwanda kwa kiswahili sanifu.
 
Ukweli ni kwamba watanzania wengi hawajui kiswahili sanifu. Hata kwenye radio na tv zote tatizo ni hilo hilo. Hivi sasa tunashindwa na kenya na rwanda kwa kiswahili sanifu.

Kila sehemu ni tatizo, hivi 'radio' ni kiswahili au kiingereza?
 
Kiukweli filamu za kitanzania hazivutii kuangalia wala hazikupi shauku ya kuendelea kutazama.....kila nikitazama hizi filamu hakuna ninachokiona zaidi ya mapaja ya wadada na chupi zao tu......
 
Mi tatizo langu kubwa ni pale jina la filamu ni 'FAMILY DISASTER' ila ndani ni kiswahili mwanzo mwisho, na mwisho kabisa utaona vile vikorombwezo viko kwa kiingereza mfano: director, producer, location manager, costume designer n.k, hivi hayo mambo hayapatikani kwa kiswahili? Hii ni tofauti na Kenya ambapo kama filamu ni ya kiswahili basi na vikorombwezo vyote vitakuwa kwa kiswahili.
Hitimisho: watanzania hatujui kiswahili wala kiingereza.
 
redio imetoholewa kutoka lugha ya kiingereza radio
 
Ukweli ni kwamba watanzania wengi hawajui kiswahili sanifu. Hata kwenye radio na tv zote tatizo ni hilo hilo. Hivi sasa tunashindwa na kenya na rwanda kwa kiswahili sanifu.

Hivi ni watanzania tu ndiyo wenye tatizo na lugha yao au kuna nchi zengine nazo pia zinatatizo kama kwenye lugha? Na nini kinasababisha hili tatizo?
 
Hivi ni watanzania tu ndiyo wenye tatizo na lugha yao au kuna nchi zengine nazo pia zinatatizo kama kwenye lugha? Na nini kinasababisha hili tatizo?

Nchi nyingi sana zina matatizo katika lugha haswa nchi zinazozungumza kiingereza.
Hii ni kutokana na muingiliano wa lugha ndogondogo kutoka maeneo tofauti tofauti pia kuna misimu ambayo nayo huchangia kujenga ama kuharibu lugha.
 
Nchi nyingi sana zina matatizo katika lugha haswa nchi zinazozungumza kiingereza.
Hii ni kutokana na muingiliano wa lugha ndogondogo kutoka maeneo tofauti tofauti pia kuna misimu ambayo nayo huchangia kujenga ama kuharibu lugha.

Je,kipi kinachowafanya kama Kenya au Rwanda kuwa na kiswahili Sanifu?
 
Nikimuona mtu anaangalia hizi film za kibongo najua ana upeo mdogo sana wa kufikiria bila hata ya kuongea nae au kumdadisi, ila zaidi waangaliaji naona ni wanawake sidhani kama kuna mwanamme. anaeangalia huu upumbavu.
 
Kuna sababu nyingi zinazofanya [ninaomba nizungumzie hapa nyumbani]
1.Kwa vile kiiswahili ni lugha mama, wengi hawaoni sababu ya kujifunza lugha hiyo kwani wanahisi kuwa wanaifahamu.
2. Radio, chombo hiki ndiyo kilikuwa ndiyo njia kuu ya kufahamu kiswahili sanifu hasa kwa vile watangazaji wake
walikuwa
wanazungumza kiswahili fasaha na hivyo kufanya kuwa rahisi kukifahamu vizuri
3 Hivi sasa waandishi wa magazeti, radio na hata baadhi ya TV hawafahamu kabisa kiswahili sanifu. wengi wao ndiyo wamekuwa virusi vya kusambaza lugha za mitaani hewani na hivyo kuambukiza vizazi vyetu.
 
Back
Top Bottom