kukumsela
JF-Expert Member
- Oct 13, 2018
- 721
- 907
Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa nchini TPBRC, imemfungia kwa muda wa mwaka mmoja bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo kufuatia kitendo chake kugomea kupanda ulingoni katika pambano lililoandaliwa na Kampuni ya PAF Promotion mwezi uliopita.
Mbali ya kumfungia kwa mwaka mmoja, TPBRC chini ya katibu wake George Silas imempiga faini ya shilingi milioni moja huku ikisisitiza adhabu hiyo haiwezi kuzuiwa PAF kwenda mahakamani kama walivyoeleza kwenye taarifa zao kwa waandishi wa habari.
Mbali ya kumfungia kwa mwaka mmoja, TPBRC chini ya katibu wake George Silas imempiga faini ya shilingi milioni moja huku ikisisitiza adhabu hiyo haiwezi kuzuiwa PAF kwenda mahakamani kama walivyoeleza kwenye taarifa zao kwa waandishi wa habari.