TANZIA Bondia George Foreman afariki dunia

Hata hivyo aliwaweka kwenye ramani ya dunia ya masumbwi watu wengi sana... Kiufupi aliwapa maishaπŸ˜…πŸ˜…πŸ˜… kwahiyo wacha aendelee kuvuta pumzi kwanza
Yeah ila alimpiga za macho Mike Tyson,

Tyson angekuwa Bilionea akiwa chalii mdogo sana akiwa na Don
 
Ungeliweka na historia yake ya kuzaliwa.
Tujue mwaka na uraia, pia nini kimemsibu kupelekea kifo chake?
 
Yeah ila alimpiga za macho Mike Tyson,

Tyson angekuwa Bilionea akiwa chalii mdogo sana akiwa na Don
Yeah uko sahihi, Don alikua muhuni muhuni fulani hiviπŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…
 
Narekebisha mambo mawili Tu kwenye post yako:
1.Ali aliwaambia Wacongoman kuwa George ni kibaraka wa wazungu na sio wabelgiji
2.kwenye picha uliotumia hapo juu ni pambano la pili Kati ya Mohammed Ali na Sony Liston, unaweza kuona Ali akiwa bado kijana mbichi kabisa. Kwenye Rumble in the jungle Big George alivalia bukta nyekundu ambayo aliivaa tena alipouchukua tena ubingwa wa dunia dhidi ya Michael Moorer.
Mengine yote upo sahihi sina shida nayoπŸ™πŸ™
 
Ungeliweka na historia yake ya kuzaliwa.
Tujue mwaka na uraia, pia nini kimemsibu kupelekea kifo chake?
George Foreman aka the Big George alizaliwa huko Marshall Texas tarehe 10 Jan 1949 ni mmarekani mweusi.
Jumla alupigana mapambano takriban 81 kama professional boxer alishinda 76 na Kati ya hayo 68 ni Kwa knockout. Halafu Leo anakuja mjinga mmoja anapigana Mapambano 50 Tu tena ya kujichagulia wapinzani halafu uzito ndogo wa light weight anataka aonekane mkubwa kuliko hawa miamba.
Hapa namzungumzia Floyd Mayweather jr.
Huyu mwamba baada ya kupigwa bila kutarajia na Mohammed Ali akataka rematch Ali akawa anamkwepa, ili kuuaminisha umma kuwa bado ni wa Moto akawa Anandaa mapambano ya kupigana na mabondia Hadi 4 Kwa wakati mmoja na wote aliwachenyenta. Ila politics za ngumi kipindi kile zilimkataa na hazikumpa nafasi ya kugombea tena ubingwa wa dunia. Akawa frustrated na mwishoe akaishia kupigwa Kwa point na Jimmy Young na baada ya pambano Hilo la 1977 akatangaza kuokoka na kustaafu rasmi masumbwi na akaamua kumtumikia Mungu kama mhubiri. Miaka kumi baadae 1987 akarudi tena ulingoni na 1997 akawa bingwa tena wa dunia kabla ya kustaafu rasmi na kuendelea na uinjilisti wake. Ujasiliamali pamoja na uandishi wa vitabu na comedy kidogo.
Sababu za kifo chake bado hazijawekwa wazi ila familia yake imesema alifariki Kwa Amani huku akiwa amezungukwa na familia yake.
RIP the Big puncher George.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…