Bomoa bomoa imeanza Kurasini Matankini

hizi nchi zetu za dunia ya tatu bila kuwa kadikteta na ukatili kidogo mambo hayaendi,utakuta wamelipwa siku nyingi lakini kuhama hawahami hadi waje kubomoa ndio watu wataanza kulaumu kwa nini wanabomolewa...mfano yule mzee wa greenacres pale victoria....hawawezi kuja kubomoa tu bila taarifa au kuwalipa
 
Tunakuwa wakimbizi kwenye nchi yetu!
 
Lakini hao si ndiyo wapenzi wa ccm? Kwa nini Kikwete asiagize wajengewe nyumba kama wale wa Bwagamoyo wanaopisha ujenzi wa bandari/bomba la gesi?

Thubutuuuuu hivyo viwanja vyenyewe walivyoandaliwa kimbiji wanatakiwa walipe mil 6......
 

Wanapozungumza wakazi hao wanasema ya kuwa pesa walizolipwa zilikuwa chini ya kiwango. Kuna mama mmoja alisikika akisema alilipwa shilingi milioni 27, na hajapewa kiwanja. Maana yake ni kwamba katika hiyo milioni 27 anunue kiwanja na ajenge nyumba ya kuishi yeye na familia yake. Halafu wiki iliyopita wakapewa siku saba wawe wamehama, wakati huenda hata hiyo milioni 27 wameshaitumia hata kama si yote kwa matumizi mengine. Kweli kama sio kuwapa watu ufukara wa kudumu ni nini?

Ama kweli maisha bora kwa kila mtanzania tunayaona. Naona ccm imeamua kama alivyosema Pinda, Liwalo na Liwe!
 
Kwahiyo hapo wapo kinyume na sheria

haswaaa! Toka 2009 walitakiwa wahame na walishapewa stahili zao sasa hapo nadhani walijisahau ndo yamewakuta haya. Si kitu kizuri ila hawajafanyiwa uvamizi ni kwamba ilikuwa iko waz na wangehama mapema dhahama hii isingewakuta.
 

Unacheza na maisha eeeeh?hivi umelipwa milion 20 alafu unasikia wenzio wanalipwa mil 300 utaona raha.
Unaweza hata ukafa....wameongezewa pesa mwaka huu mara laki2,wenye nyumba nzur mpaka mil1.Hali za wananchi ni mbaya huko,nawaonea huruma sana.
 
Unacheza na maisha eeeeh?hivi umelipwa milion 20 alafu unasikia wenzio wanalipwa mil 300 utaona raha.
Unaweza hata ukafa....wameongezewa pesa mwaka huu mara laki2,wenye nyumba nzur mpaka mil1.Hali za wananchi ni mbaya huko,nawaonea huruma sana.

kwanini ulipokea??
 
haswaaa! Toka 2009 walitakiwa wahame na walishapewa stahili zao sasa hapo nadhani walijisahau ndo yamewakuta haya. Si kitu kizuri ila hawajafanyiwa uvamizi ni kwamba ilikuwa iko waz na wangehama mapema dhahama hii isingewakuta.

Ni muda gani mtu anastahili alipwe toka tathimini imefanywa carter?
 
kwanini ulipokea??

Mimi si mkazi wa huko ingawa najua historia ya hilo eneo vizur sana tu.
Hizo pesa watu walipokea tu wafanyeje lakin w pesa zilipigwa sana watendaj wa serikal wa mtaa.
Wazir walimrekodi akisema kuwa tathimin iliyofanyika kipind hicho tunaifuta na kuanza upya,watu walifurahia sana lakin kabla yakufika kwa wananchi akaekwa mtu kati nakutoa tamko lingine kuwa hataongeza pesa zaid wale waliokataa kupokea pesa kipind kile ndo watalipwa pesa nzur hizo mil300.
 

ok ndio maana nikauliza kwanini ulipokea??kama unaona haitoshi unagoma kama hao waliogoma wakalipwa 300m...lkn sio unapokea hela then baadae unagoma kuhama unasema hela ndogo baada ya kuimaliza....kama hela ndogo usipokee weka pingamizi mahakamani
 
dah..kinacho wakuta wenzetu basi jua kina weza kutukuta ata sisi..system haijali wanachi wakat bila ya wanainchi hakuna system
 

Kiwi,

Hapo sasa ndio kuna tatizo, kwa nini walikubali kupokea hiyo hela kama ilikuwa ni kidogo? Na je kwenye makubaliano na serikali ilikuwa wapewe viwanja pamoja na malipo? Hii inabidi iwekwe wazi hapa kabla ya kukimbilia kuilaumu serikali kwa inachokifanya kwa sasa. Unaweza kukuta hiyo hela walilipwa miaka kadhaa iliyopita na wakaila na sasa wanaona kama wanaonewa.

Tiba
 
[/B]

Basi acha wakome maana wakazi wa DSM ndiyo wanajifanya wana mahaba na CCM!!!!!!!!!!!!!!

Umeona eeeeh.......yani CCM wanaipenda kama chakula,ndo wakome sasa.Ingawa wanatia huruma na mijimba yenye mingi ya urith ndo watakoma
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…