Bodi ya Mikopo kufanya msako nchi nzima kwa waajiri sugu wasiowasilisha makato na majina ya wadaiwa

TangataUnyakeWasu

JF-Expert Member
Dec 18, 2016
1,269
1,585
Kuanzia January Mosi 2017 bodi ya mikopo inakusudia kuchapisha sura za wadaiwa SUGU waliojinufaisha na mkopo wa Elimu ya juu.

BODI YA MIKOPO KUFANYA MSAKO WAAJIRI SUGU WOTE NCHINI WASIOWASILISHA MAKATO NA MAJINA YA WANUFAIKAJI

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), Abdul Razaq Badru ameunda kikosi maalumu (Task force) kwa ajili ya msako wa kuwanasa waajiri sugu wote nchini wasiowasilisha makato na majina ya wanufaikaji wa mikopo ya bodi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Badru amesema kikosi kazi hicho kitaanza kazi Januari 2, mwaka 2017 na kitafanya kazi hiyo kwa siku 14 mfululizo wakipita ofisi moja baada ya nyingine.


Chanzo: Mwananchi
 
SILALAMIKII WAO KUTOKUWEKA PICHA ILA NINA HAYA YA MSINGI KWAO:-
1. Kuna waliyoajiriwa kwenye serikali miaka mingi ila hadi sasa hivi wanawaacha hawaingilii mshahara wao kwa lazima wanawaomba walipe wenyewe, hasilan hili haliwezekani labda waingilie wenyewe kwenye halmashauri kuwa kila mwenye batchelor halmashauri au kwenye taasisis yoyote ile alete evidence ya alivyokuwa anasomeshwa hapo awali, endapo ataonekana amesomeshwa na bodi basi akatwe bila yeye kupenda
2. Endapo mdaiwa atakuwa amefikisha Two/third ya basic salary yake basi ni vyema wakamzuia kukopa na kwenye mshahara wake waweke asteric * kuonyesha kuwa huyu mtumishi hakopesheki kwenye mabenk hadi hapo loan board itakapoanza kumkata ndipo hapo mabenk yataruhusiwa kumkopesha maana, 87% ya kushuindwa kuchukua pesa yao ni kwa sababu wadaiwa wengi wa loarn board wamefikia 2/3 ya basic salary yao
3. kwahiyo kwanini nasema silalamikii wao kuweka picha, ni kwamba hakuna madhara maana hakuna aliyejua njia ya kulipa maana hakuna hata siku moja watumishi wameshapewa AC NO ya loarn board ya kuweka hela ya deni, na hakuna hamasa iliwahi kupita makazini kuhamasisha ulipaji so na wengi wanaamini kuwa ni haki yao maana ni pesa zao.
Mbona waliyosomeshwa zamani hawajalipa, why sisi
 
Naam si uungwana kutuanika...sina ajira na masomo yangu ya sanaa!huo ni uonezi kwetu siye akina pangu pakavu tia muchuzi(mchuzi).busara ni kuwanasa wahusika wa Escrow,richmond,lugumi....
 
Lazima niwe muwazi hiyo hela kunipa mlinisumbua sana na huku mnamkata mzazi wang kodi kubwa tu...sasa hyo hela silipi mpaka mnipe ajira na mkiendelea na interview zenu za kujuana basi ndo mmenipoteza jumla
.
.
.
Kyenekyaka mkighanile une
 
Huku mtaani wadaiwa wanaamini eti mtandao wenye data base ya wadaiwa ulichezewa maksudi na watu wa HESLB kwani walishiriki faulo nyingi ili kujipatia pesa.Mf kuna mtu ambaye anasema mwenyewe alikopeshwa ila jina lake halipo kwenye orodha ya wadaiwa.
 
BODI YA MIKOPO KUFANYA MSAKO WAAJIRI SUGU WOTE NCHINI WASIOWASILISHA MAKATO NA MAJINA YA WANUFAIKAJI

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), Abdul Razaq Badru ameunda kikosi maalumu (Task force) kwa ajili ya msako wa kuwanasa waajiri sugu wote nchini wasiowasilisha makato na majina ya wanufaikaji wa mikopo ya bodi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Badru amesema kikosi kazi hicho kitaanza kazi Januari 2, mwaka 2017 na kitafanya kazi hiyo kwa siku 14 mfululizo wakipita ofisi moja baada ya nyingine.



Chanzo: Mwananchi
 

Attachments

  • 20161228152102.jpeg
    20161228152102.jpeg
    9.6 KB · Views: 92
Back
Top Bottom