Black Panther 2

Black Panther 2

Captain Donor

Member
Joined
Jul 24, 2022
Posts
13
Reaction score
19
Zimebaki siku 30 tu hadi kufikia siku ambayo muendelezo wa filamu ya Black Panther kuanza kuonyeshwa kwa mara ya kwanza. Kama alivyopata kusema Baba wa Taifa hili Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, "Elimu ni kujifunza kutokea kwenye vitabu, kutokea kwenye radio, kutokea kwenye filamu, kutokea kwenye mazungumzo kuhusiana na mambo ambayo yanaathiri maisha yetu".

Filamu ya Black Panther imenifunza mengi, binafsi nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu mazungumzo kuhusiana na vipi itakuwa muendelezo wake baada ya kifo cha Chadwick Boseman ambaye aliigiza kama King T'challa?

Nimejifunza kwamba mchango wa Chadwick kuanzia kwenye uandaaji wa filamu hiyo na uigizaji wake ndani ya filamu, ulikuwa ni wa kiwango cha juu sana katika kuuvaa uhusika wa King T'challa.

Jambo ambalo limewapa wakati mgumu Marvel Studio kwa ujumla wake kujua utakuwaje muendelezo wa Black Panther bila ya Chadwick Boseman hadi kufikia hatua ya kutaka kuurecast uhusika wa King T'challa kama ilivyofanyika kwenye uhusika wa Paul Walker ndani ya filamu ya Fast&Furious baada ya Paul kufariki.

Jambo ambalo lilipingwa na watu wengi lakini mwisho wa siku kilichokuja kufanyika kinaashiria ukubwa wa legacy aliyoiacha Bwana Chadwick Boseman.

Tarehe 11 mwezi ujao Black Panther 2 itaanza kuonyeshwa kwenye kumbi za Cinema. Kwa hapa kwetu Tanzania sijajua itaanza kuonyeshwa tarehe ngapi ila nitafurahi sana kama Century Cinemax watatupatia "Experience" ya kuuona muendelezo huo siku hiyo. Licha ya kutokujua itaonyeshwa tarehe ngapi hapa Tanzania, natumai nitakuwa miongoni mwa mamilioni ya waafrika watakaopata nafasi ya kuiangalia kwa mara ya kwanza itakapoonyeshwa kwenye nchi zao.

Urithi aliouacha Chadwick Boseman (King T'challa) utaenziwa kwa ukubwa mno siku hiyo, tangu alipoaga dunia mnamo tarehe 28 mwezi wa nane mwaka juzi akiwa na miaka 43.

Tutashuhudia "Experience" burudani ya kipekee itakayojawa na wakati wa furaha, huzuni, na shauku katika kila kipande cha filamu hiyo inayohusu maisha ya uhusika ndani na nje ya uigizaji. Nje ndani ya filamu hii kwangu binafsi inahusu maisha ya Chadwick kama King T'challa na ni ukweli usiopingika kwamba kuanzia muandaaji mkuu na wahusika wengine kwa pamoja wameamua kuuenzi mchango wa Chadwick Boseman kupitia muendelezo huu mara baada ya kipindi kirefu cha kufikiri ni kipi kifanyike.

Migogoro ya hapa na pale baina ya Marvel Studio na baadhi ya waigizaji katika mchakato wa kutengeneza muendelezo huu. Kiufupi ulikuwa ni wakati mgumu ambao hatimaye unaenda kuzaa matunda kutokana na kuupa kipaumbele urithi (legacy) wa Chadwick Boseman ambaye aliigiza kwa shauku na ukubwa wa kiwango cha juu katika sehemu ya kwanza.

Tasnia ya filamu ilimpoteza jemedari wakati ambapo alihitajika zaidi na wakati huohuo umma wa Wamarekani weusi pamoja na dunia kwa ujumla ukawa umepoteza shujaa wa aina yake ambaye safari yake ya maisha ilikatizwa na ugonjwa wa saratani ya utumbo mpana.

Licha ya hivyo urithi wake bado utaendelea kuishi kizazi baada ya kizazi na tarehe kama ya leo mwezi ujao utaenziwa mchango wake kwenye tasnia ya filamu akiwa kama baba, mume na mwanaharakati, kwa ule msemo maarufu wa "WAKANDA FOREVER". Binafsi nitamuenzi kwa ule usemi wa "YIBOMBE"!
FB_IMG_1664979604135.jpg
IMG_20221003_161009.jpg
image_a46223de-d869-40a4-b74e-ffa72e0207db20220412_180704.jpg
image_235a2080-6e6d-4b89-8eb4-c6a305ca02d820220204_204053.jpg
 
Mtoto wangu anaipenda Sana hii movie ya black panther niliweka hii movie kwenye flash kipindi cha likizo alikuwa hatoki ndani.
Nataka niende nae siku ya uzinduzi hapo cinemax Ila sijajua kama atakubaliwa kuingia maana ni darasa la tano maana Sisi enzi zetu tulikuwa tunaenda majumba ya cinema na ilikuwa haina shida
 
Mtoto wangu anaipenda Sana hii movie ya black panther niliweka hii movie kwenye flash kipindi cha likizo alikuwa hatoki ndani.
Nataka niende nae siku ya uzinduzi hapo cinemax Ila sijajua kama atakubaliwa kuingia maana ni darasa la tano maana Sisi enzi zetu tulikuwa tunaenda majumba ya cinema na ilikuwa haina shida

Nenda nae tu, Disney movie zao nyingi wanaziweka za kuangaliwa mpaka na watoto
 
Mtoto wangu anaipenda Sana hii movie ya black panther niliweka hii movie kwenye flash kipindi cha likizo alikuwa hatoki ndani.
Nataka niende nae siku ya uzinduzi hapo cinemax Ila sijajua kama atakubaliwa kuingia maana ni darasa la tano maana Sisi enzi zetu tulikuwa tunaenda majumba ya cinema na ilikuwa haina shida
Anaruhusiwa
 
Suluhisho la hii kitu ni kumle mtoto katika malezi ya dini maana dini zote zinakemea hili, hata asipokuogopa mzazi atamuogopa Muumba
Hakika, na pia uzuri kuna Parental Guidance (PG) rate ya umri kwenye kila movie huwa wanaweka. Lengo ni ili kile kinachoonyeshwa kiandane na uwezo wa mtu kupokea maudhui yaliyomo kwenye filamu. Ukiachana na kuwa siku hizi makampuni mengi yanayojihusisha na utengenezaji wa filamu yanaingiza sana hizo ajenda za ushoga na ulesbian ambazo zinakwenda kinyume na tamaduni zetu sisi waafrika kiujumla, pia suala la wazazi kuzingatia PG rate kwa watoto wao ni muhimu kwasababu kuna baadhi ya maudhui hayafai kutazamwa na rika fulani kutokana na matukio ya kinyama yaliyo ndani yake ambayo yanaweza kuathiri afya ya akili ya mtoto. Kwa hiyo as long as mtazamaji ana umaizi wa kutosha, atajua ni lipi na kuchukua na lipi la kupuuza kutokana na hizo ajenda mbaya kuwepo ndani ya filamu nyingi.
 
Hakika, na pia uzuri kuna Parental Guidance (PG) rate ya umri kwenye kila movie huwa wanaweka. Lengo ni ili kile kinachoonyeshwa kiandane na uwezo wa mtu kupokea maudhui yaliyomo kwenye filamu. Ukiachana na kuwa siku hizi makampuni mengi yanayojihusisha na utengenezaji wa filamu yanaingiza sana hizo ajenda za ushoga na ulesbian ambazo zinakwenda kinyume na tamaduni zetu sisi waafrika kiujumla, pia suala la wazazi kuzingatia PG rate kwa watoto wao ni muhimu kwasababu kuna baadhi ya maudhui hayafai kutazamwa na rika fulani kutokana na matukio ya kinyama yaliyo ndani yake ambayo yanaweza kuathiri afya ya akili ya mtoto. Kwa hiyo as long as mtazamaji ana umaizi wa kutosha, atajua ni lipi na kuchukua na lipi la kupuuza kutokana na hizo ajenda mbaya kuwepo ndani ya filamu nyingi.
PG guidance ni tatizo kubwa sana kwa sisi Watanzania, watoto wadogo wanaangalia hadi Horror movies.

as long as ni movie mzazi hajali then utakuta wazazi hawapo halafu Housemaid ndio yupo kwahiyo yeye anaweka movie yeyote maana wengi uelewa wao mdg
 
PG guidance ni tatizo kubwa sana kwa sisi Watanzania, watoto wadogo wanaangalia hadi Horror movies.

as long as ni movie mzazi hajali then utakuta wazazi hawapo halafu Housemaid ndio yupo kwahiyo yeye anaweka movie yeyote maana wengi uelewa wao mdg
Yeah PG guidance bado ni tatizo kibongo bongo.
 
Back
Top Bottom