Bingooo! Hatimaye Vodacom waahidi kurudisha vifurushi!

Bingooo! Hatimaye Vodacom waahidi kurudisha vifurushi!

kisugujira

JF-Expert Member
Joined
Aug 13, 2012
Posts
774
Reaction score
200
WanaJF,

Mkurugenzi wa kampuni ya Vodacom amesikia kilio cha wateja wake na kuahidi kurudisha vifurushi vyote vilivyonunuliwa siku ya Ijumaa tarehe 16/8/2013 kabla ya matatizo ya mawasiliano mtandaoni kutokea yaliyosababishwa na swichi ya mtandao kuungua!

Source:Star tv
 
Warudishe na time waliyopoteza kwani kama kifurushi kilikuwa kiishe tarehe kumi na tisa wao wakazingua hiyo 16th maana almost three days zimekwenda hapo!
 
Vodacom ni wezi tu unanunua kifurushi unaangalia video ya dakika moja YouTube kifurushi kimeisha sina hamu nao.!!
 
Warudishe na time waliyopoteza kwani kama kifurushi kilikuwa kiishe tarehe kumi na tisa wao wakazingua hiyo 16th maana almost three days zimekwenda hapo!

waswahili hatuna jema tumeambiwa tunarudishiwa bundle zetu munaanza kudai eti umepotezewa muda je isipo rudishwa unapakwenda kulalamika? Mswahili bana ukimpa kidole anataka na mkono.
 
warudishe na airtime yangu ! nyambafuuu...
 
WanaJF,

Mkurugenzi wa kampuni ya Vodacom amesikia kilio cha wateja wake na kuahidi kurudisha vifurushi vyote vilivyonunuliwa siku ya Ijumaa tarehe 16/8/2013 kabla ya matatizo ya mawasiliano mtandaoni kutokea yaliyosababishwa na swichi ya mtandao kuungua!

Source:Star tv

Mfano,ulinunua kifurushi cha Tsh 500 na ndicho utakachorudishiwa,hapa Bingo iko wapi?
 
Mfano,ulinunua kifurushi cha Tsh 500 na ndicho utakachorudishiwa,hapa Bingo iko wapi?
Mkuu Rogie,hicho kifurushi chako cha Tsh 500 kilichokuwa kinaelekea kupotea bila kutumika na kurudishwa ndiyo Bingo yenyewe!
 
Mi wanirudishie mpenzi wangu.......aliyepeperuka.........

Preta,ina maana hata baada ya Vodacom kurudisha mawasiliano jamaa bado anapeperuka na kutojulikana aliko? Pole sana. Nenda kwenye wodi za wagonjwa Airtel unaweza mkuta huko akitibiwa baada ya BP kumpanda kutokana na kupigwa chini na Vodacom kwa muda!
 
Bingoo!?!?..really?

what happened to 'companies need to have stable and reliable disaster recovery/business continuity plans in place to ensure that business objectives are met even in the most unexpected of natural calamities'?
 
waswahili hatuna jema tumeambiwa tunarudishiwa bundle zetu munaanza kudai eti umepotezewa muda je isipo rudishwa unapakwenda kulalamika? Mswahili bana ukimpa kidole anataka na mkono.

Tunatofautiana kuwaza mkuu wakati wewe unafurahia keki mpaka kwapa linalowa mimi nawaza kumiliki bakery!!!!!!
 
WanaJF,

Mkurugenzi wa kampuni ya Vodacom amesikia kilio cha wateja wake na kuahidi kurudisha vifurushi vyote vilivyonunuliwa siku ya Ijumaa tarehe 16/8/2013 kabla ya matatizo ya mawasiliano mtandaoni kutokea yaliyosababishwa na swichi ya mtandao kuungua!

Source:Star tv

Sasa bingo kivipi kwani tunapewa bure.Ifike point tufike point ya kutambua haki zetu na wajibu wetu.
 
Sasa bingo kivipi kwani tunapewa bure.Ifike point tufike point ya kutambua haki zetu na wajibu wetu.

Kwani Bingo maana yake ni nini? Mimi nafikiri ni ushindi fulani hivi ambao mtu anaupata baada ya kuweka jitihada fulani katika kuupata! Hii inaweza kutokea katika kesi,madai au mchezo. Kupitia JF Vodacom wanaweza wakawa wamesikia malalamiko yetu na kuona aibu ya kuturudishia vifurushi vyetu! Huo ni ushindi tosha kwani tumepiga kelele sana!

Tujaribu kutafakari kabla ya kukurupuka na kutoa kashfa kwa lugha zenye ukakasi! Pata ufahamu zaidi kwa kufungua kiunganishi hiki https://www.jamiiforums.com/habari-...vifurushi-vyetu-siyo-kuomba-radhi-wateja.html
 
Back
Top Bottom