Mwanafunzi bora wa kidato cha nne kwa mwaka 2009, Imaculate Mosha kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana Marian ya mjini Bagamoyo, akipongezwa na kaka yake Eng. Dominic Mosha baada ya kupokea taarifa za matokeo hayo jana akiwa mjini Bagamoyo alipokwenda kufanya usaili wa kidato cha tano katika shule ya Marian.
Hata mimi sijaelewa maana ya heading yako Kuwa Mungu hakunyimi vyote. Maana kwa mtazamo wangu ni kuwa kutokana na heading yako ninaweza kunyongoloa kuwa au Imakulata na kasoro ya kimaumbile, au sura yake mbaya, au mapungufu yoyote katika mwili wake, hivyo basi pamoja na kuwa na kasoro hizo lakini bado alikuwa anafanya vizuri sana darasani hivyo kupelekea kuwa mwanafunzi bora katika mtihani yake ya kuhitimu.
Huu ni mtizamo wangu pengine mwenye mada atatufafanulia zaidi. kama hana ufafanuzi basi awe anaangali "heading" inayoendana na thread.
Pamoja na hayo Hongera sana IMACULATE Mungu akujalie na akutangulie katika safari mpya unayoianza ya elimu dunia.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.