Bima gari ya Chenge ilikuwa ya mtu mwingine

Msharika

JF-Expert Member
May 15, 2009
947
69
'Bima gari ya Chenge ilikuwa ya mtu mwingine'
Na Hidaya Kivatwa



OFISA wa Kampuni moja ya Bima ya jijini Dar es Salaam, ameiambia Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni kuwa stakabdhi ya bima aliyekuwa nayo waziri wa zamani wa Miondombinu, Andrew Chenge, ilikuwa ni ya mtu mwingine.

Ofisa huyo wa Kampuni ya Scan Insurance and General Services Limited, Raygon Njeje alitoa madai hayo jana, alipokuwa akitoa ushahidi wake katika kesi kuhusu tuhuma kwamba Chenge, aliendesha gari bila kuzingatia sheria za usalama barabarani na hivyo kusababisha vifo vya watu wawili.

Njeje ambaye ni wakala wa kampuni hiyo, pia aliiambia mahakama kuwa Chenge hajawahi kuwa mteja wake kama inavyoonyeshwa katika stakabadhi hiyo.

Alidai kuwa stakabadhi hiyo iliyowasilishwa na Chenge, haikuwa ya gari lake na kwamba ilikuwa ya gari aina ya Toyota RAV4, iliyomesajiliwa kwa namba tofauti na ile ya kwake.

Kwa mujibu wa ofisa huyo, gari hilo ni mali ya Evarist Bigurumba Sesa.
Shahidi huyo alielezea kushangazwa kuhusu stakabadhi hiyo akielezea kuwa kumbukumbu za kampuni hiyo, iliyoko chini ya Kampuni Phoenix of Tanzania Insurance, zinaonyesha kuwa Chenge hayumo katika orodha ya watu waliowahi kukata bima.


"Stakabadhi namba 1919156 ilisainiwa na mimi, lakini ilikuwa ni bima ya gari la Evarist Bigurumba Sesa na si la Chenge. Niliitoa kwa ajili ya matumizi ya miezi mitatu, kati ya Juni 29 mwaka 2007 hadi Septemba 28 mwaka 2007,"alisema Njeje.

"Kamwe hatujawahi kuwa na mteja anayeitwa Chenge na hii stakabadhi siyo yake, ni ya mtu mwingine, kwani namba moja ya stakbadhi haiwezi kutumika mara mbili," alisisitiza.

Ushahidi huo ulitolewa na wakala huyo wakati ambapo Ofisa wa Shirika la Bima la Taifa alikuwa ameiambia mahakama kwamba gari la Chenge, lilikuwa halina bima na hata kampuni iliyokuwa imetoa bima awali ilikuwa ni feki.

Kesi hiyo iliharishwa hadi Septemba 7 mwaka huu, mahakama itakapotoa uamuzi wa ama mshtakiwa kuwa au kutokuwa na kesi ya kujibu.

Mapema, wakili Simon Mponda anayemtetea Chenge, alikuwa amekanusha vipengele tisa vilivyosomwa mahakamani wakati kesi iliposomwa kwa mara ya kwanza.

Chenge alishtakiwa kwa tuhuma za kutokuwa mwangalifu katika kufuata sheria za usalama barabarani na kusababisha vifo vya wanawake wawili, Victoria George na Beatrice Constatine, Machi 27, mwaka jana.
Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, Chenge alikuwa akiendesha gari aina ya Toyota Hillux Double Cabin na akawa amezidi upande wa njia ya magari ambayo alipaswa kupishana nayo.

Inadaiwa kuwa katika mazingira hayo, aliigonga pikipiki aina ya Bajaj na kusababisha vifo vya wanawake hao.



Source: Mwananchi
 
Mtu msomi aliyeshindwa kuonesha uzalendo wake kwa kutetea maslahi ya Taifa lake kwenye mikataba unadhani anaweza kuuonesha uzalendo huo kwa kampuni binafsi?!
 
Kwa hiyo aligushi hiyo bima aliokuwa anatemebelea? Na kugushi si kosa la jinai pia.
 
usomi(sheria) na hela alizonazo havijamsaidia kitu,!jamaa wa ajabu hawa
 
Mwananchi anayeikosesha serikali yake mapato, kwa kugushi hata bima za magari! Na bado anagombea ubunge akiahidi maendeleo kwa taifa!
 
Da! Mzee chenge asipojiangalia lazima ale mvua hapo. Yani alishindwa kusolve issue ya Bima wakati issue za namna hiyo zikitokea unakimbia fasta kukata.:A S 100: ('' Haloo watu wa bima limenikuta mwenzenu, Kateni ya miezi miwili nishagonga huku'' halafu kumbukeni kuandika tarehe za nyuma)
 
Mwananchi anayeikosesha serikali yake mapato, kwa kugushi hata bima za magari! Na bado anagombea ubunge akiahidi maendeleo kwa taifa!
Yaani pamoja na kuwa na vijisenti mabenki abroad anaona shida akiweka kiasi kisichozidi laki 3 katika maendeleo ya nchi-bima? Sishangai mafisadi wamempitisha tena kugombea, kwani wote si mamoja tu? Ila najiuliza jimboni kwake hakuna mwingine mwingine mwenye hadhi ya kuleta maendeleo ya nchi yetu? Nchi inaelekea kuzimu:A S-danger:
 
Subiri hukumu itasema hivi " Baada ya kupitia vielelezo vyote na kuzingatia ushahidi, nimeona mtuhumiwa Andrew Chenge hana hatia na hivyo namwachia huru. Walalamikaji mnayo haki ya kukata rufaa ndani ya siku 30."
Hii ndio danganyika ilivyo bwana nyie subirini tu kama nasema uongo mtaniambia. Akiona noma hakimu atamwambia alipe faini shilingi milioni 1 na kwa sababu hilo ni kama tone katika bahari atalipa mara moja na kesi finished.
 
Subiri hukumu itasema hivi " Baada ya kupitia vielelezo vyote na kuzingatia ushahidi, nimeona mtuhumiwa Andrew Chenge hana hatia na hivyo namwachia huru. Walalamikaji mnayo haki ya kukata rufaa ndani ya siku 30."
Hii ndio danganyika ilivyo bwana nyie subirini tu kama nasema uongo mtaniambia. Akiona noma hakimu atamwambia alipe faini shilingi milioni 1 na kwa sababu hilo ni kama tone katika bahari atalipa mara moja na kesi finished.


Ndivyo itakayokuwa.
 
Mtu msomi aliyeshindwa kuonesha uzalendo wake kwa kutetea maslahi ya Taifa lake kwenye mikataba unadhani anaweza kuuonesha uzalendo huo kwa kampuni binafsi?!

Ni miongoni mwa watu ambao hawafai hata chembe kuwa viongozi wa nchi yetu. nasema hilo si tu kwa sababu ya kuwa na kesi ya kugonga, bali nikifuatilia mambo ambayo amefanya kuidhulumu nchi. zile bilioni katika kisiwa kule uingereza hajatolea maelezo ya kuridhisha. sasa sijui ni kawaida kwa watu wa ccMajambazi kuficha mijihela ughaibuni, ndo maana hata yeye chenge akaita vijisenti!!!!!?????
 
Subiri hukumu itasema hivi " Baada ya kupitia vielelezo vyote na kuzingatia ushahidi, nimeona mtuhumiwa Andrew Chenge hana hatia na hivyo namwachia huru. Walalamikaji mnayo haki ya kukata rufaa ndani ya siku 30."
Hii ndio danganyika ilivyo bwana nyie subirini tu kama nasema uongo mtaniambia. Akiona noma hakimu atamwambia alipe faini shilingi milioni 1 na kwa sababu hilo ni kama tone katika bahari atalipa mara moja na kesi finished.


Hivi ulisomea uhakimu nn maana naona unamajibu yote kabisa :becky::becky::becky::becky::becky::becky: ila hukumu itatoka baada ya uchaguzi kuisha ili ashinde kwa kishindo kikubwa
 
"Ushahidi huo ulitolewa na wakala huyo wakati ambapo Ofisa wa Shirika la Bima la Taifa alikuwa ameiambia mahakama kwamba gari la Chenge, lilikuwa halina bima na hata kampuni iliyokuwa imetoa bima awali ilikuwa ni feki."

sasa ikiwa mzee wa vijisenti anataka bima feki vipi kuhusu elimu yake ukute nayo ni feki ikiwa mwanasheria unapenda vitu feki basi ulakini wa taaluma yako nao nadhani ni feki kamwa feki hawezi kuwa orijino
 
Back
Top Bottom