Bilioni 42 Zamwagwa Kufuta Shida ya Maji Mji wa Ifakara

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
43,109
49,811
Rais Samia anaendelea Kupeleka matumaini Kwa Watanzania wa Ifakara.

Shilingi Bilioni 42 Zinatumika kujenga mradi mkubwa wa kuleta maji mjini Ifakara.

Mji wa Ifakara unapata maji Kwa Asilimia 34 tuu hivyo ujio.wa mradi huu utawezesha Wananchi kupata maji Kwa uhakika.

Hongera sana Rais Samia Kwa kumtua mama ndio kichwani.
---
Mkuu wa Mkoa Morogoro, Adam Malima ametembelea Mradi wa Maji wa Kiburubutu, Ifakara utakaogharimu kiasi cha shilingi Bilioni 42, ukitarajiwa kukamilika Oktoba 10, 2025.

RC Malima ameeleza kukerwa na baadhi ya watu wanaofanya shughuli za kibinadamu kandokando ya vyanzo vya maji na kueleza kuwa serikali inatumia fedha nyingi katika uendelezaji wa miradi hivyo ni wajibu wa kila mtu kutunza miradi hiyo.

Amesema mpango wa serikali ni kuwahudumia wananchi wa mijini na vijijini wote wapate kwa usawa huduma za kijamii na kwamba uharibifu huo umekua kikwazo kwenye miradi mingi ya maji na kushindwa kutoa huduma kwa wa sababu ya maslahi ya watu wachache.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Ifakara, Mhandisi Ahmad Mpambaike amesema hali ya sasa ya utoaji huduma ya maji katika Mji wa Ifakara ni asilimia 34 na kwamba mradi huo umefikia asilimia 7 ya ujenzi wake, ukisimamiwa na mkandarasi mshauri (Consultant), WAPCOS LIMITED INDIA na Mkandarasi Mjenzi (Contractor) Larsen &Toubro Limited India.

674265760.jpg
957914877.jpg
 
Ifakara watu wengi wanavisima vile vya kupampu,labda maeneo korofi km Kaporo kibaoni kule sababu ni mlimani.
Kuna Tanki lile pale V/60 karibu na Mato kwanini halifanyi kazi.
Zamani sana tulilitumia na mabomba ya serikali yaliwekwa mfano pale kwa Makwemla kulikuwa na bomba la serikali.Kila la heri idara ya maji Ifoza
 
Sasa kwanini wamekata hiyo miti na kutandaza nondo na Zege? Wakati hiyo miti ni chemichemi ya maji?

Wastage of money, resources and labour.

Haki ya nani kama mdau wa mazingira sijafurahishwa.
957914877.jpg
674265760.jpg
 
Ifakara watu wengi wanavisima vile vya kupampu,labda maeneo korofi km Kaporo kibaoni kule sababu ni mlimani.
Kuna Tanki lile pale V/60 karibu na Mato kwanini halifanyi kazi.
Zamani sana tulilitumia na mabomba ya serikali yaliwekwa mfano pale kwa Makwemla kulikuwa na bomba la serikali.Kila la heri idara ya maji Ifoza
Hivyo sio visima salama sana ndio maana unaona mamlaka inasema water supply Iko 34 % tuu.
 
Rais Samia anaendelea Kupeleka matumaini Kwa Watanzania wa Ifakara.

Shilingi Bilioni 42 Zinatumika kujenga mradi mkubwa wa kuleta maji mjini Ifakara.

Mji wa Ifakara unapata maji Kwa Asilimia 34 tuu hivyo ujio.wa mradi huu utawezesha Wananchi kupata maji Kwa uhakika.

Hongera sana Rais Samia Kwa kumtua mama ndio kichwani.
---
Mkuu wa Mkoa Morogoro, Adam Malima ametembelea Mradi wa Maji wa Kiburubutu, Ifakara utakaogharimu kiasi cha shilingi Bilioni 42, ukitarajiwa kukamilika Oktoba 10, 2025.

RC Malima ameeleza kukerwa na baadhi ya watu wanaofanya shughuli za kibinadamu kandokando ya vyanzo vya maji na kueleza kuwa serikali inatumia fedha nyingi katika uendelezaji wa miradi hivyo ni wajibu wa kila mtu kutunza miradi hiyo.

Amesema mpango wa serikali ni kuwahudumia wananchi wa mijini na vijijini wote wapate kwa usawa huduma za kijamii na kwamba uharibifu huo umekua kikwazo kwenye miradi mingi ya maji na kushindwa kutoa huduma kwa wa sababu ya maslahi ya watu wachache.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Ifakara, Mhandisi Ahmad Mpambaike amesema hali ya sasa ya utoaji huduma ya maji katika Mji wa Ifakara ni asilimia 34 na kwamba mradi huo umefikia asilimia 7 ya ujenzi wake, ukisimamiwa na mkandarasi mshauri (Consultant), WAPCOS LIMITED INDIA na Mkandarasi Mjenzi (Contractor) Larsen &Toubro Limited India.

Injinia!!!!
Soma hiyo!!!!
 
Ni kweli ila mmechelewa sana, kwanini lile Tanki la pale V/60 halitumiki?
Waulize watu wa Ruwasa huko uliko Mimi natoa taarifa ya Jumla sio specific info.

Chelewa ila fika,Samia amewafikia labda hao wengine ndio walichelewa.
 
Back
Top Bottom