sammosses
JF-Expert Member
- Jan 24, 2011
- 1,743
- 1,164
CCM imechoka sasa kuliko wakati wote toka kuumbwa kwa dunia hii. Simba akizeeka hukimbilia kwenye vyanzo vya maji kuvizia wanyama wadogo wadogo, kutokana na kukosa nguvu ya kupambana katika mawindo yake.
CCM inavizia kwenye kurudisha fomu, kupora fomu na kupitisha wanaCCM bila kupingwa kuwa viongozi wa wananchi, na kuikanyaga mamlaka ya wananchi kwa mujibu wa katiba.
Imepoteza imani yake kwa wapiga kura kwa kushindwa kufanya siasa za ushindani wakitegemea mbeleko ya kupita bila kupingwa.
Ziko sababu zilizo pelekea kufanya yanayo fanyika katika uchaguzi huu wa serikali za mitaa kama ifuatavyo:
1. Pamoja na serikali kupitia mwenyekiti wa CCM Taifa kuzuia vyama vingine kufanya siasa za wazi ilihali wao wana fanya, mwitikio wa wananchi kupinga siasa za kibaguzi umekuwa mkubwa sana kuliko wakati wowote na kuviimarisha vyama vya siasa vya upinzani kuliko wakati wowote.
2. CCM na serikali yake kushindwa kuhimili mnyukano wa hoja ikitegemea zaidi kubebwa na nguvu ya dola jambo linaloiweka nchi kwenye hali tete.
Ndo maana mawaziri wake wamekuwa wapiga ramli kwa yanayotokea, wakifikirishwa zaidi kujihami katika kulinda dhamana zao.
Waziri mzima ana thubutu kutamka ole wao wapinzani walio amua kujitoa kwenye uchaguzi, wakitegemea kufanya vurugu. Serikali imejipanga kuwadhibiti kwa nguvu kubwa. Lakini amesahau kuwa walio paswa kushughulikiwa kwa nguvu kubwa ni wale walioitwa Ikulu na kupewa maelekezo ya kuvuruga uchaguzi wa kidemokrasia.
3. Pamoja na serikali kufanya matumizi yasiyo rasmi ya kununua madege kama wanavyoita wao, hali ya Watanzania kiuchumi, kijamii na kiusalama haiko sawa kabisa.
Tumeona deni la Taifa likipaa kila kukicha, lakini hospitali hazina dawa. Tumeaminishwa elimu bure lakini michango inazidi utayari wa elimu bure.
Mzunguko wa uchumi wa chini umepotea na serikali kuwatumia wataalamu kupika takwimu kwa malengo ya kuiaminisha dunia.
Hali ya usalama ni tete kwa maskini, na hata matajiri. Kama hujatekwa utafunguliwa kesi ya kutakatisha fedha ili tu kukodhoofisha uchumi katika kutimiza lengo la Watanzania waishi kama mashetani.
Usalama unaolinda uchumi wa mtu mmoja mmoja umepotezwa kwa makusudi.
4. Kwa kuwa mikutano ilizuiliwa kwa muda mrefu, uchaguzi ndiyo jukwaa pekee la kufanya mikutano ya hadhara, ambayo Watanzania wengi watasikia maovu ya serikali na kupata mrejesho wa yanayofanyika ndani ya serikali, bunge na Mahakama.
Kupitisha wagombea wa bila kupingwa wawe viongozi wa wananchi, ni zuio lingine la vyama vya siasa kufanya kampeni na mikutano ya hadhara.
Ndiyo maana mkakati huu ukiuchunguza kwa kina utaona hauna lengo zuri kwa mshikamano wa kitaifa. Haikijengi CCM zaidi cha kukifanya kuwa chama Cha Majambazi, maana wenye tabia ya kupora ni majambazi.
#Ukimsikiliza waziri mwenye dhamana na TAMISEMI utasema wana nia njema, lakini kinacho fanyika na watendaji walio chini yake (WEO 's) ambao ndiyo wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ambao waliitwa ikulu na mwenyekiti wa CCM,kwa dhamana ya urais ambao TAMISEMI iko chini ya ofisi hiyo, na ukimya wa serikali kwa uhuni unaofanywa na watendaji hao, utaona wazi huu ni mkakati toka ikulu.
Waziri kuwataka waliokatwa kupeleka rufaa zao kwa waliowakata ni matumizi mabaya ya rasilimali muda, huo ni uhuni kama ulivyo uhuni unaofanywa kukandamiza demokrasia nchini.
Chokochoko hizi haziisaidi serikali zaidi ya kuzidisha hali tete ya usalama nchini. Kwa kuwa wenye mamlaka ya kuziweka serikali kwenye madaraka (wananchi) wameporwa haki yao ya kikatiba, wamepewa watendaji wa kata.
History inatueleza chokochoko zote kwenye mataifa mengi husababishwa na ukosefu wa huduma bora na chaguzi za kihuni kama huu wa TAMISEMI, ambazo husababisha serikali nyingi kuondolewa madarakani, kwa hali hii sasa rasmi CCM imechoka kutawala.
Mwalimu Nyerere alisema "bila CCM madhubuti nchi itayumba " ni kweli nchi inayumba, chaguzi si za haki wala huru. Matumizi mabovu ya fedha za walipa kodi haziakisi maisha ya Watanzania.
Umadhubuti wa CCM aliyoifikiria Mwalimu ni ile yenye kuheshimu demokrasia, yenye kuwasikiliza Watanzania wanataka nini, si unataka nini ,ni ile yenye kuheshimu na kuitumia katiba kama mwongozo. Lakini leo imepoteza ideology yake kabisa, chama hakiamini katika ustaarabu tena, ndo maana nchi inayumba.
Kauli hii ya Mwalimu imegeuka fumbo la imani, linawatesa kutafuta uhalali wa kubaki madarakani kwa njia yeyote ile. Lakini wameshindwa kuheshimu kuwa Tanzania ni ya Watanzania, vyama vitapita nchi itabaki.
CCM inavizia kwenye kurudisha fomu, kupora fomu na kupitisha wanaCCM bila kupingwa kuwa viongozi wa wananchi, na kuikanyaga mamlaka ya wananchi kwa mujibu wa katiba.
Imepoteza imani yake kwa wapiga kura kwa kushindwa kufanya siasa za ushindani wakitegemea mbeleko ya kupita bila kupingwa.
Ziko sababu zilizo pelekea kufanya yanayo fanyika katika uchaguzi huu wa serikali za mitaa kama ifuatavyo:
1. Pamoja na serikali kupitia mwenyekiti wa CCM Taifa kuzuia vyama vingine kufanya siasa za wazi ilihali wao wana fanya, mwitikio wa wananchi kupinga siasa za kibaguzi umekuwa mkubwa sana kuliko wakati wowote na kuviimarisha vyama vya siasa vya upinzani kuliko wakati wowote.
2. CCM na serikali yake kushindwa kuhimili mnyukano wa hoja ikitegemea zaidi kubebwa na nguvu ya dola jambo linaloiweka nchi kwenye hali tete.
Ndo maana mawaziri wake wamekuwa wapiga ramli kwa yanayotokea, wakifikirishwa zaidi kujihami katika kulinda dhamana zao.
Waziri mzima ana thubutu kutamka ole wao wapinzani walio amua kujitoa kwenye uchaguzi, wakitegemea kufanya vurugu. Serikali imejipanga kuwadhibiti kwa nguvu kubwa. Lakini amesahau kuwa walio paswa kushughulikiwa kwa nguvu kubwa ni wale walioitwa Ikulu na kupewa maelekezo ya kuvuruga uchaguzi wa kidemokrasia.
3. Pamoja na serikali kufanya matumizi yasiyo rasmi ya kununua madege kama wanavyoita wao, hali ya Watanzania kiuchumi, kijamii na kiusalama haiko sawa kabisa.
Tumeona deni la Taifa likipaa kila kukicha, lakini hospitali hazina dawa. Tumeaminishwa elimu bure lakini michango inazidi utayari wa elimu bure.
Mzunguko wa uchumi wa chini umepotea na serikali kuwatumia wataalamu kupika takwimu kwa malengo ya kuiaminisha dunia.
Hali ya usalama ni tete kwa maskini, na hata matajiri. Kama hujatekwa utafunguliwa kesi ya kutakatisha fedha ili tu kukodhoofisha uchumi katika kutimiza lengo la Watanzania waishi kama mashetani.
Usalama unaolinda uchumi wa mtu mmoja mmoja umepotezwa kwa makusudi.
4. Kwa kuwa mikutano ilizuiliwa kwa muda mrefu, uchaguzi ndiyo jukwaa pekee la kufanya mikutano ya hadhara, ambayo Watanzania wengi watasikia maovu ya serikali na kupata mrejesho wa yanayofanyika ndani ya serikali, bunge na Mahakama.
Kupitisha wagombea wa bila kupingwa wawe viongozi wa wananchi, ni zuio lingine la vyama vya siasa kufanya kampeni na mikutano ya hadhara.
Ndiyo maana mkakati huu ukiuchunguza kwa kina utaona hauna lengo zuri kwa mshikamano wa kitaifa. Haikijengi CCM zaidi cha kukifanya kuwa chama Cha Majambazi, maana wenye tabia ya kupora ni majambazi.
#Ukimsikiliza waziri mwenye dhamana na TAMISEMI utasema wana nia njema, lakini kinacho fanyika na watendaji walio chini yake (WEO 's) ambao ndiyo wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ambao waliitwa ikulu na mwenyekiti wa CCM,kwa dhamana ya urais ambao TAMISEMI iko chini ya ofisi hiyo, na ukimya wa serikali kwa uhuni unaofanywa na watendaji hao, utaona wazi huu ni mkakati toka ikulu.
Waziri kuwataka waliokatwa kupeleka rufaa zao kwa waliowakata ni matumizi mabaya ya rasilimali muda, huo ni uhuni kama ulivyo uhuni unaofanywa kukandamiza demokrasia nchini.
Chokochoko hizi haziisaidi serikali zaidi ya kuzidisha hali tete ya usalama nchini. Kwa kuwa wenye mamlaka ya kuziweka serikali kwenye madaraka (wananchi) wameporwa haki yao ya kikatiba, wamepewa watendaji wa kata.
History inatueleza chokochoko zote kwenye mataifa mengi husababishwa na ukosefu wa huduma bora na chaguzi za kihuni kama huu wa TAMISEMI, ambazo husababisha serikali nyingi kuondolewa madarakani, kwa hali hii sasa rasmi CCM imechoka kutawala.
Mwalimu Nyerere alisema "bila CCM madhubuti nchi itayumba " ni kweli nchi inayumba, chaguzi si za haki wala huru. Matumizi mabovu ya fedha za walipa kodi haziakisi maisha ya Watanzania.
Umadhubuti wa CCM aliyoifikiria Mwalimu ni ile yenye kuheshimu demokrasia, yenye kuwasikiliza Watanzania wanataka nini, si unataka nini ,ni ile yenye kuheshimu na kuitumia katiba kama mwongozo. Lakini leo imepoteza ideology yake kabisa, chama hakiamini katika ustaarabu tena, ndo maana nchi inayumba.
Kauli hii ya Mwalimu imegeuka fumbo la imani, linawatesa kutafuta uhalali wa kubaki madarakani kwa njia yeyote ile. Lakini wameshindwa kuheshimu kuwa Tanzania ni ya Watanzania, vyama vitapita nchi itabaki.