Bila katiba mpya kuandikwa na wananchi wenyewe CCM itapora haki za watanzania

dr. gracemary

Member
Jul 7, 2011
32
6
Kwa kweli inaumiza sana kuona taifa, majimbo na kata vinaongozwa na watu ambao hawakuchaguliwa kihalali na wananchi bali wamechaguliwa na CCM inayodhani ina haki ya kumiliki taifa hili. Chaguzi mbalimbali nchini na matokeo yake ni ushahidi wa kutosha unaoonyesha kuwa hali hii itaendelea kuwa hivi miaka yote kama hakuna katiba mya. CCM wanafanya mchezo na maisha ya watu na hawaoni shida.

Maoni yangu: Chadema ongozeni mapambano dhidi ya kuandikwa kwa katiba mpya, msisubiri uongo wa CCM kwani tutafika 2015 hakuna katiba mpya. Tunahitaji katiba mpya for our own future...kina mama wenzangu nao tusikubali kutumiwa na CCM. Tunahitaji ukombozi wa kweli na sasa tumechoka na utumwa wa jitu CCM.
 
Back
Top Bottom