Bila Kadi kwa mtu mzima hupandi mwendokasi

Bila Kadi kwa mtu mzima hupandi mwendokasi

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
Kuanzia leo Julai 1, 2025, huduma ya Mabasi ya Mwendokasi jijini Dar es Salaam imesitisha rasmi matumizi ya tiketi za karatasi kwa abiria wa kawaida na kuanza kutumia mfumo wa kadi maalum zenye salio.

Abiria sasa wanatakiwa kuwa na kadi hizo, zitakazopatikana katika kwa shilingi elfu moja na kujazwa salio katika vituo mbalimbali vilivyokuwa vikitoa tiketi.

Hali hiyo imeibua mtazamo tofauti kwa baadhi ya abiria, hususan maeneo ya Morogoro Road, ambao wamedai hawakufahamu kuhusu mabadiliko hayo mapya. Wengine wamesema mfumo huo mpya unaweza kuwa changamoto kwa wananchi wa kipato cha chini.

Wafanyakazi wa vituo vya Mwendokasi wameeleza kuwa tiketi za karatasi zitaendelea kutumika kwa wanafunzi pekee. Vituo kama Mbezi Mwisho, Kibanda cha Mkaa, Kwa Msuguli, Temboni, Suka na Stop Over vimewekewa mashine maalum za kuskani kadi.
1751348332930.png
1751348332930.png

Chanzo:Nipashe
 
Hii inaenda kuwauwa njaa wale wakata tickets ambao walikuwa siyo waaminifuu... Mtu mzima walikuwa wanamkatia tickets ya mwanafunzi Halafu wanabana chenji..

Halafu wanampanga yule mpokea tickets aipokee na kumruhusu abiria apite faster halafu tickets inachanwa na kutupwa... Ama kweli Teknolojia inalaza watu njaaa..
 
Ndio serikali ya ccm ilishindwa kufanya hivi mpaka walete waarabu wa oman!😁😁😁🚮
^Eti sisi milioni 61 ni mandondocha kuliko Waarabu wa Dubai!^ ~alisikika John Heche
 
Kuanzia leo Julai 1, 2025, huduma ya Mabasi ya Mwendokasi jijini Dar es Salaam imesitisha rasmi matumizi ya tiketi za karatasi kwa abiria wa kawaida na kuanza kutumia mfumo wa kadi maalum zenye salio.

Abiria sasa wanatakiwa kuwa na kadi hizo, zitakazopatikana katika kwa shilingi elfu moja na kujazwa salio katika vituo mbalimbali vilivyokuwa vikitoa tiketi.

Hali hiyo imeibua mtazamo tofauti kwa baadhi ya abiria, hususan maeneo ya Morogoro Road, ambao wamedai hawakufahamu kuhusu mabadiliko hayo mapya. Wengine wamesema mfumo huo mpya unaweza kuwa changamoto kwa wananchi wa kipato cha chini.

Wafanyakazi wa vituo vya Mwendokasi wameeleza kuwa tiketi za karatasi zitaendelea kutumika kwa wanafunzi pekee. Vituo kama Mbezi Mwisho, Kibanda cha Mkaa, Kwa Msuguli, Temboni, Suka na Stop Over vimewekewa mashine maalum za kuskani kadi.
Ila wabongo wanadeka sana. Eti matumizi ya kadi yanaweza kuwa changamoto kwa watu wa vipato vya chini. Kwani wamepandisha nauli? Mi naona imebaki buku ile ile…

Kwa nini tunaogopa matumizi ya teknolojia ?
 
Kuanzia leo Julai 1, 2025, huduma ya Mabasi ya Mwendokasi jijini Dar es Salaam imesitisha rasmi matumizi ya tiketi za karatasi kwa abiria wa kawaida na kuanza kutumia mfumo wa kadi maalum zenye salio.

Abiria sasa wanatakiwa kuwa na kadi hizo, zitakazopatikana katika kwa shilingi elfu moja na kujazwa salio katika vituo mbalimbali vilivyokuwa vikitoa tiketi.

Hali hiyo imeibua mtazamo tofauti kwa baadhi ya abiria, hususan maeneo ya Morogoro Road, ambao wamedai hawakufahamu kuhusu mabadiliko hayo mapya. Wengine wamesema mfumo huo mpya unaweza kuwa changamoto kwa wananchi wa kipato cha chini.

Wafanyakazi wa vituo vya Mwendokasi wameeleza kuwa tiketi za karatasi zitaendelea kutumika kwa wanafunzi pekee. Vituo kama Mbezi Mwisho, Kibanda cha Mkaa, Kwa Msuguli, Temboni, Suka na Stop Over vimewekewa mashine maalum za kuskani kadi.
Yani nilinunua kadi kwa elfu tano leo hii wanauziwa buku wanasema wanakipato cha chini.
 
Mabasi ni mapya au yale yale?

Kwenye kituo wanakaa dakika ngapi? Au wameboresha
 
Back
Top Bottom