Biashara ya uji

noony

Member
Joined
Apr 6, 2018
Posts
65
Reaction score
52
Habari za majukumu wanajamvi, matumaini yangu mnachukua taadhari dhidi ya janga hili la Corona.

Niende moja kwa moja kwenye mada. Mimi ni binti miaka 25 nimemaliza chuo mwaka wa tatu sasa sijabahatika kupata ajira rasmi ila nnajishughulisha na shughuli za hapa na pale mradi mkono uende kinywani.

Ninatamani kuanzisha biashara ya kuuza uji katika sehemu zenye watu wengi. Kwa sasa naishi Iringa. Malengo yangu ni kuwa na sehemu kama 10 za kuuza uji (sio ofisi bali vijana wa kutembeza katika maeneo hayo 10) asubuhi na jioni kwa mtaji wa sh 300,000.

Naomba kwa mwenye ujuzi au uzoefu au hata mawazo bunifu au ushauri wowote juu ya biashara hii.

Asante.
 
Maamuzi yako ni mazuri nikupe hongera kwa hatua Hiyo
Sehemu ambazo ni nzuri kwa Hiyo biashara ni stand za mabus hizi huku ndiko naonaga Watu wengi wanakunywa uji
 
Fanya lakini sikushauri kuanza na pesa yote hiyo.

Anza hata na Themos 3 au 5 na utakuwa unaongeza kidogo kidogo kulingana na mwenendo wa biashara utakavyokuwa.
 
Asante. Ntakutafuta
 
Hizo vitenge sio Common? Kinacho kosekana ni Ubunifu na sio common
Tuseme za ukweli uji umekuwa common kwa sasa!....sijajua km kuna kipya!
Ningekuwa ndo mie Maathai ningeenda Katoro kuchukua vitenge vya bei chee!...kila kitenge sikosi 4000!.chukua kitenge kwa 18000uza kwa 25000

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…