Biashara ya salon za kiume na kike

Umeweka huduma gani? Mfano scrub maana sinza saloon zimejaa tele
Habari zenu wakuu. Katika kupitia mawazo ya humu na research yangu ndogo nilofanya niliweza kufungua barbershop yangu maeneo ya Sinza Mori. Toka nimefungua hii ni wiki ya 2 nimeanza wiki ya tatu lkn kusema ukweli biashara imekuwa ya kawaida sana yani tofauti hata na malengo yangu. Ningependa kufaham je mwazo wa biashara hii ndivo unavokuwa au itafika mahali mambo yatabadilika na kuwa sawa.? Natanguliza shukrani zangu kwenu wakuu
 
Mkuu hapo kwanza ungetuambia kama umeajiri watu au unanyoa mwenyewe. Kwa ufahamu wangu mdogo ni kwamba vinyozi wengi wanapohama saloon huhama na wateja wao. Kama unanyoa mwenyewe tengeneza kwanza mtandao wako wa wateja ila kama umeajiri jaribu kuzungumza na vinyozi wako.
 
Mkuu hapo kwanza ungetuambia kama umeajiri watu au unanyoa mwenyewe. Kwa ufahamu wangu mdogo ni kwamba vinyozi wengi wanapohama saloon huhama na wateja wao. Kama unanyoa mwenyewe tengeneza kwanza mtandao wako wa wateja ila kama umeajiri jaribu kuzungumza na vinyozi wako.
Kaka nimeajiri watu wapo hapo wanaendesha ndio hvo kila siku napata hzo report za kawaida.
 
Siku hizi za mwanzo jitahidi kuwepo na ww ili ujue kinachoendelea binadamu hawaaminiki ndugu,wateja wanaweza kufika na kunyoa wala usigundue km umeme ulinunua wa kutosha wakahisi utawashitukia na wao wananunua unit kidogo wanajazia ukiuliza unaambiwa hamna wateja na ww ukicheck unit unakuta kweli zipo
 
Habari zenu wakuu. Katika kupitia mawazo ya humu na research yangu ndogo nilofanya niliweza kufungua barbershop yangu maeneo ya Sinza Mori. Toka nimefungua hii ni wiki ya 2 nimeanza wiki ya tatu lkn kusema ukweli biashara imekuwa ya kawaida sana yani tofauti hata na malengo yangu. Ningependa kufaham je mwazo wa biashara hii ndivo unavokuwa au itafika mahali mambo yatabadilika na kuwa sawa.? Natanguliza shukrani zangu kwenu wakuu
Kila mwanzo ni mgumu boss, biashara zaku subiri mteja aingiye zina changamoto sana. Ila kwa ushauri, kutokana vile saluni bado mpya, fanya uigawe Mara 2. Iwe upande wakunyowa na kaupande kadogo ka wakina Dada, kusuka na Kutengeneza Dread. Hapo utakuwa umepiga ndege wa 2 kwa jiwe 1. Mori nisehem nzuri sana kibiashara, nilisha wai kufunguwa saluni hapo hapo mori, maeneo ya Meeda Bar. kwa ushauri zaidi ni check PM.
 
Back
Top Bottom