fyddell
JF-Expert Member
- Dec 19, 2011
- 11,109
- 19,987
Hii ni barabara ya Uhuru soko la Karume, wafanyabiashara wanaotandaza bidhaa zao chini wamesogea mpaka usawa wa barabara na kusababisha usumbufu na foleni zisizotarajiwa kwa watumiaji wa njia hiyo kuelekea au kutoka katika ya jiji la Dar es Salaam.
Hakuna mamlaka ya kuzuia hili kwa usalama wa wafanyabiashara na magari yatumiayo barabara hiyo?
Au vitambilisho vya mjasiliamali vinawapa kinga wafanyabiashara kufanya biashara mahali popote pale?
Huko mjini maeneo ya Kisutu barabara ndogo zitokazo na ziingiazo zote zimejaa mama ntilie na wauza matunda. Tunaomba mamlaka husika irudie ule utaratibu wa zamani wakutenga maeneo maalumu ya biashara.
Tutajua kuwa hili lilipangwa kimkakati ili kuongeza mapato serikalini. Sasa tunaomba mamlaka iangalie madhara yanayosababishwa na ufanyaji biashara holela.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna mamlaka ya kuzuia hili kwa usalama wa wafanyabiashara na magari yatumiayo barabara hiyo?
Au vitambilisho vya mjasiliamali vinawapa kinga wafanyabiashara kufanya biashara mahali popote pale?
Huko mjini maeneo ya Kisutu barabara ndogo zitokazo na ziingiazo zote zimejaa mama ntilie na wauza matunda. Tunaomba mamlaka husika irudie ule utaratibu wa zamani wakutenga maeneo maalumu ya biashara.
Tutajua kuwa hili lilipangwa kimkakati ili kuongeza mapato serikalini. Sasa tunaomba mamlaka iangalie madhara yanayosababishwa na ufanyaji biashara holela.
Sent using Jamii Forums mobile app