Betting Vs Forex Trading

Betting Vs Forex Trading

mbwadinho

Senior Member
Joined
Jun 29, 2016
Posts
180
Reaction score
102
Habari za majukumu jamani.

Samahani, naomba kwa wenye uzoefu na ujuzi na hivi vitu. Kipi kina risk kubwa kati ya betting nikimaanisha masuala ya soka na vitu kama hivyo ukilinganisha na Forex Trading?

Pili, kipi kinahitaji mtaji mdogo kwa siku angalau 50000 na faida isizidi 15000?
 
Samahan mkuu kuna namna ya kuepuka hizo risk au ipo hivyo tu
Forex ina risk kubwa sana, - Iwapo trades zitakuwa against positions zako.
KInyume chake pia ni sahihi, Ina faida kubwa iwapo utaenda kulingana na soko.

Hiki kipengele wengine watachangia
 
kuna namna ya kuepuka hizo risk au ipo hivyo tu
Ndio zipo njia za kuepukana na risk ya kupoteza fedha. Kama
- Tumia muda mwingi kujifunza/ kusoma kuliko kufanya trading.
- Tumia muda mwingi kusubiria setup sahihi, na ingia sokoni kwa wakati sahihi, na toka kwa wakati sahihi.
- Jiwekee kanuni na kuzifuata mfano, Hata kama zitapita siku kadhaa bila kuingia sokoni.
Ukipoteza mara moja, usiinie tena sekoni hadi siku inayofuata, na pia iwapo utapata big win pia jipe muda ndipo uingie tena ( Control your emotion unapopata au unapopoteza ).
- Tumia setup ya aina moja kwa muda wote, sio leo uko na hii kesho na hii.

- Wengine wataendelea kuna vingi vya kuzingatia.
 
Forex sio betting

Zingatia muktadha wa muuliza swali

Amehusisha Forex na betting sababu njia zote kwanza unaingiza fedha ili mwishoni upate fedha, Hivyo mleta mada anajaribu kuangazia hasara na faida. Ila sio kweli kwamba forex na betting ni sawa. La hasha.
Nilidhani hapo awali kuwa forex ni kibashiri kuwa currency fulani itapanda au kushuka ndipo upate faida kumbe huku hakuna kubashir km kwenye betting
 
Sawasawa mkuu ila samahani kwa maswali mengi hv hii forex kwa nchi za wenzetu ambapo masoko yapo huko mfano nchi km uk ,usa je kwann baadhi ya wananchi wao hulalamika ajira wkt fursa ni hii forex kwani ht masuala ya uchambuz ni rahisi kwao kwasababu matukio ya kiuchumi huhusu nchi zao
Hakuna kubashiri.
- Ni uchambuzi na ufuatiliaji wa matukio ya kiuchumi
- Kwa kutumia taarifa za chati husika za Mwezi/ wiki/ Siku hata masaa kadhaa basi waweza kupata picha ya mwelekeo wa soko na kujipanga wakati sahihi wa kuingia.
- Ukikosea ni hasara kwenda mbele
 
forex kwa nchi za wenzetu ambapo masoko yapo huko mfano nchi km uk ,usa je kwann baadhi ya wananchi wao hulalamika ajira wkt fursa ni hii forex
Sio rahisi kama ambavyo unafikiria/ tunafikiria, Au kama tulivyo aminishwa, wachache wenye uvumilivu wa kujifunza kwa bidii ndio hufanikiwa. Na wapo walio fanikiwa kupitia forex hata hapa JF.

Ni sawa na kilimo, sio kila anayeingia kwenye kilimo basi hufanikiwa au kwenye ufugaji kuna ambao hufanikiwa na kuna ambao hufeli, hivyo hata katika biashara ya forex, kama biashara zingine, wapo wanaofanikiwa na wapo wanaoshindwa kufanikiwa.
 
Sawasawa na ili mtu uwe mtaalamu haswa wa forex inachukua muda gani kujifunza mkuu
Sio rahisi kama ambavyo unafikiria/ tunafikiria, Au kama tulivyo aminishwa, wachache wenye uvumilivu wa kujifunza kwa bidii ndio hufanikiwa. Na wapo walio fanikiwa kupitia forex hata hapa JF.

Ni sawa na kilimo, sio kila anayeingia kwenye kilimo basi hufanikiwa au kwenye ufugaji kuna ambao hufanikiwa na kuna ambao hufeli, hivyo hata katika biashara ya forex, kama biashara zingine, wapo wanaofanikiwa na wapo wanaoshindwa kufanikiwa.
 
Sawasawa na ili mtu uwe mtaalamu haswa wa forex inachukua muda gani kujifunza mkuu
- Basics inachukua miezi mitatu (3)
- Ila swala la kujifunza ni endelevu, utaendelea kujifunza kipindi chote ambacho utakuwa unajihusisha na hii biashara.
- Mimi binafsi huu ni mwaka wa tatu (3) tangu nianze kujifunza na naendelea kujifunza.
=====
Update
- Hata walio fanikiwa kwenye forex pia hupata mabalaa/ majanga kwenye biashara hii naa kupoteza mtaji
- Soma hili badniko: https://www.jamiiforums.com/threads...-anadaiwa-pesa-nyingi-polisi-wamsaka.1582528/
 
Mkuu nn ushauri wako kwa mtu anayetaka kujihusisha na hii biashara ambaye anataka forex iwe ni km ajira kwake
- Basics inachukua miezi mitatu (3)
- Ila swala la kujifunza ni endelevu, utaendelea kujifunza kipindi chote ambacho utakuwa unajihusisha na hii biashara.
- Mimi binafsi huu ni mwaka wa tatu (3) tangu nianze kujifunza na naendelea kujifunza.
=====
Update
- Hata walio fanikiwa kwenye forex pia hupata mabalaa/ majanga kwenye biashara hii naa kupoteza mtaji
- Soma hili badniko: https://www.jamiiforums.com/threads...-anadaiwa-pesa-nyingi-polisi-wamsaka.1582528/
 
Asante mkuu kwa muda wako ubarikiwe
- Atumie muda mwingi kujifunza.
- Afanye majaribio ya biashara, DEMO trading kwa muda usio pungua miezi sita au zaidi.
- Anza na mtaji mdogo kadri iwezekanavyo, na ukuze huo mtaji.
 
Sijawahi kubet ila natrade forex zaidi kwenye stocks( 6 years in a row tangu nimemalize chuo mi ofisi yangu ni chumbani kwangu) kama leo asubuhi nimefungua positions za kubuy uber. Nikifungua position yoyote either a buy/sell huwa na analyse mda mwingine hata mwezi kwa small cap stocks na miezi miwili kwa large cap sasa sijui kama kwenye kubet huwa wanafanya hivyo.

Alafu forex imegawanyika katika vipisi pisi vingi tu, kuna wanao trade currencies, indices, indexes, stocks na commoities. Naamini katika Forex kila mtu anakuwa na style yake unique ambayo huwa anaitumia ambayo ipo suitable kwake yeye, hayo mambo ya mentors na kununua signals tupilia mbali kabisa asilimia 90% ya mentors wabongo ni matapeli. Kama unataka kuzama kwenye forex ntakupa ushauri wa bure ufuatao.

1. Anza kutrade Demo account kwa atleast mieze minne, hii itakupa picha ya jinsi masoko yanavyoenda na kama kweli umeamua kuinvest mda wako wote kwenye hili then ndani ya mwaka ni lazima uwe umefanikiwa. Hakikisha hiyo demo account utakayo fungua balance yake ni ile ile utakayo deposit, sio unafungua demo account ya usd 1 mil then unakuja deposit 100$.

2. Soma, narudia tena soma. Knowledge is power. Kuna pdf kibao online fanya research yako, telegram kuna magroup mengi tu ya traders library unaweza pata vitabu vya bure huko ambavyo vitakusaidia mbeleni. Fuatilia habari sana tu kama huna tabia hiyo ndo uanze lipia dstv angalia Bloomberg masaa yote kuna insights za kutosha sana .

3. Wakati ukiwa unatrade hiyo demo account andika each and every single position utakayo fungua na kufunga, kuanzia mda uliofungua mpaka uliofunga pamoja pips ulizopata ama ulizopoteza na hii tabia usiache hata uje ufanikiwe vipi. Na ili ujue na uweze kufuatilia vizuri inabidi hizo notes zako zicover 24 hours kwa siku tano kwa mda wa miezi mitatu ambayo ni Q1 hii itakusaidia kujua ni mda upi ambao upo most volatile na mda gani masoko hayatembei.

Pia hili litakusaidia kujua ni pairs zipi zina hela na pairs zipi ni kimeo na pair zipi zenye correlation pia itakupa mwanga mpana zaidi wa kutengeneza trading plan yako ambayo usijethubutu ukaenda against nayo ikija kukamilika, Plan your trade, Trade your plan always.

4. Patience na emotion elimination. Kwakuwa unaanza na demo hivi vitu hutavijua, ila siku ukifungua real account ukaweka pesa zako then ukafungua positions hii ndo utakuja kujua maana yake ni nini. You have to experience this on your own ili uweze kujicontrol. Naweza andika mpaka mwaka ujao ila hivi vitu viwili vipo damuni kwa kila binadamu na kuviacha huwezi ila tunachofanyaga ni kuji fine tune tu.

5. Tafuta strategy. Usinunue kwa mtu utauziwa utumbo uliooza (wakati naanza nilipigwa karibia 2000$ kununua strategies that never worked na robots zilizochoma account tu).

6. Forex si kwa watu wenye roho nyepesi, ila ukisha kamilisha hivyo vitu vyote na ukaona upo fresh fungua cent account deposit dola 4 nadhani ni kama buku 10 tu ambayo itakuwa kama cent 400 hii itakusaidia kukujenga kwenye point zangu za number 4.

Forex unaweza anza na 1$
 
Nilidhani hapo awali kuwa forex ni kibashiri kuwa currency fulani itapanda au kushuka ndipo upate faida kumbe huku hakuna kubashir km kwenye betting
Dah hata mm kwa haraka haraka nilifikir hii ndio maana ya forex
 
sijawahi kubet ila natrade forex zaidi kwenye stocks( 6 years in a row tangu nimemalize chuo mi ofisi yangu ni chumbani kwangu) kama leo asubuhi nimefungua positions za kubuy uber. Nikifungua position yoyote either a buy/sell huwa na analyse mda mwingine hata mwezi kwa small cap stocks na miezi miwili kwa large cap sasa sijui kama kwenye kubet huwa wanafanya hivyo. Alafu forex imegawanyika katika vipisi pisi vingi tu, kuna wanao trade currencies, indices, indexes, stocks na commoities. Naamini katika Forex kila mtu anakuwa na style yake unique ambayo huwa anaitumia ambayo ipo suitable kwake yeye, hayo mambo ya mentors na kununua signals tupilia mbali kabisa asilimia 90% ya mentors wabongo ni matapeli. Kama unataka kuzama kwenye forex ntakupa ushauri wa bure ufuatao.
1. Anza kutrade Demo account kwa atleast mieze minne, hii itakupa picha ya jinsi masoko yanavyoenda na kama kweli umeamua kuinvest mda wako wote kwenye hili then ndani ya mwaka ni lazima uwe umefanikiwa. Hakikisha hiyo demo account utakayo fungua balance yake ni ile ile utakayo deposit, sio unafungua demo account ya usd 1 mil then unakuja deposit 100$.
2. Soma, narudia tena soma. Knowledge is power. Kuna pdf kibao online fanya research yako, telegram kuna magroup mengi tu ya traders library unaweza pata vitabu vya bure huko ambavyo vitakusaidia mbeleni. Fuatilia habari sana tu kama huna tabia hiyo ndo uanze lipia dstv angalia Bloomberg masaa yote kuna insights za kutosha sana .
3. Wakati ukiwa unatrade hiyo demo account andika each and every single position utakayo fungua na kufunga, kuanzia mda uliofungua mpaka uliofunga pamoja pips ulizopata ama ulizopoteza na hii tabia usiache hata uje ufanikiwe vipi. Na ili ujue na uweze kufuatilia vizuri inabidi hizo notes zako zicover 24 hours kwa siku tano kwa mda wa miezi mitatu ambayo ni Q1 hii itakusaidia kujua ni mda upi ambao upo most volatile na mda gani masoko hayatembei. Pia hili litakusaidia kujua ni pairs zipi zina hela na pairs zipi ni kimeo na pair zipi zenye correlation pia itakupa mwanga mpana zaidi wa kutengeneza trading plan yako ambayo usijethubutu ukaenda against nayo ikija kukamilika, Plan your trade, Trade your plan always.
4. Patience na emotion elimination. Kwakuwa unaanza na demo hivi vitu hutavijua, ila siku ukifungua real account ukaweka pesa zako then ukafungua positions hii ndo utakuja kujua maana yake ni nini. You have to experience this on your own ili uweze kujicontrol. Naweza andika mpaka mwaka ujao ila hivi vitu viwili vipo damuni kwa kila binadamu na kuviacha huwezi ila tunachofanyaga ni kuji fine tune tu.
5. Tafuta strategy. Usinunue kwa mtu utauziwa utumbo uliooza (wakati naanza nilipigwa karibia 2000$ kununua strategies that never worked na robots zilizochoma account tu).
6. Forex si kwa watu wenye roho nyepesi, ila ukisha kamilisha hivyo vitu vyote na ukaona upo fresh fungua cent account deposit dola 4 nadhani ni kama buku 10 tu ambayo itakuwa kama cent 400 hii itakusaidia kukujenga kwenye point zangu za number 4.
Forex unaweza anza na 1$
Powerful information.
 
Back
Top Bottom