Betting sio biashara halali

WELL SAID MKUU.

Na kwa kumsaidia huyu MAKRITA ni kwamba kwa Tanzania ili usajili kampuni ya Betting lazima uwe na mtaji wa Shilingi Bilioni MBILI au zaidi.
 
Katika orodha ya matajiri wakubwa duniani, africa na hata tanzania, hebu nitajie waliofika pale kwa kutumia betting, ili tuwatumie kama mfano kuwashawishi watoto wetu wakazane na kubet zaidi.
Tajiri gani atakwambia ukweli wa uhalali wa utajiri wake,yapo mengi haramu watu wamefanya kuwa matajiri ila hakuna atakayekwambia ukweli,miongoni mwa hao matajiri unaowajua wewe kuna wengine walishapita pita kwenye haramu ambazo kwa namna moja au nyingine zimewafikisha walipo na usitake kutuaminisha pesa za betting ndo haramu pombe,cocaine,sigara etc pia biashara haramu na ndo maana kuna nchi zingine km za kiarabu ukienda hivi vitu ni adimu kuvipata mm nilidhani ungeongelea kwa upande wa dini kila kidunia betting ni halali na ndo maana wanalipa kodi tena kampuni za betting ni miongoni mwa walipaji kodi wazuri tu
 
Dah! Wewe jamaa
 
Mnatupigia kelele tu humu wengine kazi yenu ni kuhonga malaya tu,harafu leo hii mnasema niache kubet!!! Kubet ni mchezo wala sio biashara kwamba kila cku lazima uifanye. Mimi naweka buku kwa wiki au kwa cku,hata nikiliwa wew inakuhusu? Wewe honga hao malaya wa buguruni,mim niache niitumie Nguvu ya Buku (1000) kwenye ubashiri.
 
Mkuu umemjibu vema. Kabla ya kuleta hayo mawazo yake alitakiwa kufanya uchunguzi kwa kina. Inaonyesha hata terms and conditions za betting hazijui.
 
Ni kweli kabisa,
Ila wao wanacheza kama sehemu ya burudani, na siyo mkakati wa kupata fedha, kama ambavyo vijana wengi wa kitanzania wanajidanganyw.
Unakuta mtu ana elfu 2 anapanga kwenda kubet apate elfu 20 ya kuendesha maisha yake, huu ndiyo ujinga unaoumiza vijana wengi.
 
Achana na maisha ya watu sio lazima tufuatishe mawazo yako ..
Hujalazimishwa kusoma wala kucoment mkuu,
Sijakuletea ulipo usome,
Nimejipa wajibu wa kutoa elimu sahihi kwa wale wanaoangamia kwa kukosa maarifa sahihi, huitaki elimu hii pita tu mkuu.
 
Hakika,
Wengi hawaoni madhara ya muda mrefu kwa huu mchezo wa hovyo.
Ni janga kwa taifa, pale ambapo vijana wanategemea kubahatisha kama njia ya kuingiza kipato.
 
Sasa mkuu kama 50cent anayeingiza dola laki 2 kwa kila SAA kutokana na Muziki pamoja na Investments zake anabet sembuse sisi ambao hatuna uwezo wa kuingiza hata Milioni 2 kwa siku...???
Kwahiyo akibet 50 cent ndo uhalali wa wewe kubet?
Kwanza umemfatilia huyo 50 vizuri au una habari za juu juu za kujishawishi ubet?
Unajua kwa nini alifile bankruptcy?
 
Endelea kujidsnganya hivyo hivyo,
Na endelea kubet,
Siku utakapozinduka, utaendelea kulaumu serikali kwa maisha yako magumu.
Kila la kheri.
 
Kwahiyo akibet 50 cent ndo uhalali wa wewe kubet?
Kwanza umemfatilia huyo 50 vizuri au una habari za juu juu za kujishawishi ubet?
Unajua kwa nini alifile bankruptcy?
Mimi nilijua uhalali wa jambo lolote unatokana na mamlaka husika.

Ckuwahi kujua kwamba ili biashara iwe halali lazima ihalalishwe na MAKRITA AMANI.
 
Endelea kujidsnganya hivyo hivyo,
Na endelea kubet,
Siku utakapozinduka, utaendelea kulaumu serikali kwa maisha yako magumu.
Kila la kheri.
Acha upumba hakuna biashara halali hapa mjini,labda ukalime mpunga ifakara waache watu wa beti

hata kubeti kwenyewe sio bure lazma ufanye kazi ndo upate hela ili ukabeti

na si utuambie biashara gani halali wewe unafanya so watu ndo wakusikilize
 
Wakipiga hela wanafura afu wanarudisha zote kwenye kubet, madhara ni long term huwezi ona leo. Kuna kitu kinaitwa pathological gambling ndo hatua ya mwisho, apo ukisha anza chomoa tairi ya gari ya mkeo na kwenda kuuza ili uka gamble
 
Mtoa mada utakuwa umeliwa sana kwa kubet hovyo hovyo mpaka umegeuka kuwa mwanaharakati. Me siwezi kuacha kubet kabisa aisee, na ikitokea serikali imezuia huu mchezo, naweza kuhama kwenda kuishi nchi ambayo mchezo huu upo.

Sijawahi kufanya biashara inayonipatia faida nyingi kama hii ktk maisha yangu. Me daily huwa natafuta 1.60 or 1.80 ya odds, naweka milioni moja, naondoka zangu. Nna mwezi wa kumi sasa mfululizo napata faida ya kati ya laki nne mpaka laki sita kila siku kwa mtaji wangu huo wa milioni moja.

Nakushangaa sana unavyoeneza uongo huo wa uharamu. Ni bora kwenye kujenga hoja yako labda ungetuhusia kiimani/kiroho walau ungetushawishi kwa kumuhofia mungu wetu.
 
Naunga hoja asilimia 100% ukiwakuta vijana ndiyo wamekaa wanabeti utafiki wapo shule wanajisomee kwa maandalizi ya NECTA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…