makoye2009
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,638
- 1,219
Muda mfupi tu uliopita nilikuwa nasikiliza BBC Swahili mahojiano ya moja kwa moja kati ya BBC na Benson Kigaila Mkurugenzi wa mafunzo wa CHADEMA na Nnape Nauye wa CCM. Kigaila ameweka wazi msimamo wa CDM/UKAWA kuwa hawatambui Urais wa Magufuli na hawako tayari kushirikiana na serkali ya Magufuli!
Benson Magufuli amehoji kufutwa kwa Uchaguzi Zanzibar kuwa CCM wamefanya hivo baada ya kushindwa vibaya lakini CCM hiyohiyo ikasema kura za Rais wa JMT na hauna kasoro.Kigaila ametoa mfano mmoja ambao umeniacha sina mbavu.Kwamba wanachofanya CCM Bara kukubali kura za kutoka Zanzibar ni sawa na mtu aliyepika nyama ya Kuku na ya Kitimoto kwenye sufuria moja na mlaji wa nyama akawa ni Mwislamu ambaye inabidi achague nyama za kuku toka sufuria lenye mchanganyiko na Kitimoto huku akisema nyama za kuku ni halal!
Benson Magufuli amehoji kufutwa kwa Uchaguzi Zanzibar kuwa CCM wamefanya hivo baada ya kushindwa vibaya lakini CCM hiyohiyo ikasema kura za Rais wa JMT na hauna kasoro.Kigaila ametoa mfano mmoja ambao umeniacha sina mbavu.Kwamba wanachofanya CCM Bara kukubali kura za kutoka Zanzibar ni sawa na mtu aliyepika nyama ya Kuku na ya Kitimoto kwenye sufuria moja na mlaji wa nyama akawa ni Mwislamu ambaye inabidi achague nyama za kuku toka sufuria lenye mchanganyiko na Kitimoto huku akisema nyama za kuku ni halal!