BEN SAANANE KATIKA DURU ZA KIMATAIFA.
Hatimaye kelele zetu zimefikia kwenye duru za kimataifa. Baada ya idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Ujerumani (Radio DW) kumhoji Mhe.Mbowe kuhusu suala la kupotea kwa Ben, jarida la kimataifa la All Africa (online tabloid) linaloandika habari za nchi zote 52 za Afrika, na kusomwa na mamilioni ya watu duniani kote limeandika habari ya kupotea kwa Ben-Rabiu Saanane na juhudi zinazofanywa na UTG kumtafuta.
Hadi sasa habari ya Ben imesomwa na zaidi ya watu milioni 2 na still inaendelea kupata wasomaji kila siku. Hili ni doa kwa nchi yetu. Hii ina maana kwamba kuna watu milioni 2 wamesoma kwamba TZ sio nchi salama sana kwa raia wake. Tafsiri yake ni kwamba wageni wanaokuja nchini wanaweza kuhofia usalama wao ikiwa raia wetu wenyewe wanapotea zaidi ya mwezi bila kujulikana walipo.
Wageni wanaotarajia kuja kwa ajili ya uwekezaji, utalii, biashara, masomo etc wanaweza kuopt kwenda nchi nyingine badala ya kuja kwetu. Tunaweza kudhani tunamkomoa Ben lakini kumbe tunajikomoa wenyewe kama nchi. Tutakapoanza kuona idadi ya watalii inapungua, uwekezaji wa nje unapungua, na biashara ya kimataifa inadorora ndio tutajua anayekomolewa ni Ben au sisi wenyewe. Hakuna mtalii, mfanyabiashara au mwekezaji anayependa kwenda mahali penye doa kuhusu usalama wa watu.
Natoa pongezi kwa jarida la All Africa kwa kuona umuhimu na uzito wa habari hii na kuamua kuipublish. Pia napongeza gazeti la The Citizen ambalo ndio chimbuko la habari hii. Pongezi zaidi kwa UTG kwa hatua wanazoendelea kuchukua hadi sasa.[HASHTAG]#BringBackBenAlive[/HASHTAG]
Ukitaka kusoma habari hii ingia hapa
http://allafrica.com/stories/201612120626.