Ni Arusha pekee mchele wa Kamsamba maarufu wa Mbeya kipindi cha mavuno na kipindi ambacho sio cha mavuno bei ni ile ile...hawashushi bei wao watakubadilishia Mchele tuu sijui wa Magugu au Kahama...mchele sasa hivi huko Mbeya kwa 20Kg ni Tsh 35,000 mpaka 45,000 ule uliokobolewa vizuri zaidi ila mchele ni ule ule ule bei tofauti...
Bei bado ziko juu ya miti. Tumejaribu kukata miti zishuke chini. tumeambia tunaharibu mazingira. Tunatakiwa tuote mbawa tuzifuate huko huko juu ya miti.
Bei bado ziko juu ya miti. Tumejaribu kukata miti zishuke chini. tumeambia tunaharibu mazingira. Tunatakiwa tuote mbawa tuzifuate huko huko juu ya miti.
Sasa nunueni akiba ya chakula kwa ajili ya familia yako kipindi hichi ambacho mazao yashuke bei , badae hatutaki lawama za kijinga dhidi ya bashe utadhani ndo aliwasaidia kuwazalisha wake zenu.
Mimi Mwanza nimenunua mchele kg 2000 nikashangaa, maana Bei ilikua 2900 nikahisi hiyo Bei ya sokoni tu, nimeulizia Jana dukani hapa mtaani Bei hiyohiyo 2000 per kg
Watu hawatanunua chakula cha kutosha afu wanataka bei zibaki hivohivo zikiwasubiri. Na hivi zimeshuka Hawaongei zikipanda tu wanaanza kelele.
Wakulima wanazalisha chakula cha kutosha kiuzwe na nchi jirani. Subir jirani waje uone.
Nchi hii ina chakula kingi sana sema serikali ni wapumbavu tu! Sasa hivi Wakenya wamezagaa vijijini wanakusanya mahindi kama hawana akili nzuri! Jamaa yangu yuko Hanang' anasema gunia limefika 80k muda si mrefu chakula kitaisha turudi kule kule! Huku kwetu sasa Mchele 1500 kwa kilo, mafuta ya alizeti 3500 kwa lita na mahindi 12k kwa debe!