kamanyani
Member
- Jan 2, 2015
- 65
- 110
Habarini wanajamvi,
Hivi karibuni nimegundua bei za vifurushi vya data zimepanda tena licha ya kupunguzwa takribani miezi 4 iliyopita baada ya wananchi kupiga kelele.
Bei za vifirushi hivi zimepandishwa kinyemela baada ya kushushwa kwa kelele za wananchi. Sasa najiuliza ni ile mbinu ya "waache baada ya muda watajisahau tupandishe tena hawatapiga kelele"?.
Mfumuko wa bei za bidhaa mbalimbali umeshika kasi, tozo lukuki zimeongezwa, ninajiuliza na kujipa tafakuli mwenyewe, hivi imeshidikana kukusanya kodi kwa Mabeberu au kunani kinachoendelea.. Mzigo wa maisha ya mwananchi wa chini "wanyonge" pamoja na wananchi wa kati umezidi kuwa mzito na kwakifupi siku zinavyozidi kwnd punda atakufa kabla ya kifukisha mzigo.
Niwatakie Kazi njema na nangoja maoni yenu wajuvi wa mambo.
Hivi karibuni nimegundua bei za vifurushi vya data zimepanda tena licha ya kupunguzwa takribani miezi 4 iliyopita baada ya wananchi kupiga kelele.
Bei za vifirushi hivi zimepandishwa kinyemela baada ya kushushwa kwa kelele za wananchi. Sasa najiuliza ni ile mbinu ya "waache baada ya muda watajisahau tupandishe tena hawatapiga kelele"?.
Mfumuko wa bei za bidhaa mbalimbali umeshika kasi, tozo lukuki zimeongezwa, ninajiuliza na kujipa tafakuli mwenyewe, hivi imeshidikana kukusanya kodi kwa Mabeberu au kunani kinachoendelea.. Mzigo wa maisha ya mwananchi wa chini "wanyonge" pamoja na wananchi wa kati umezidi kuwa mzito na kwakifupi siku zinavyozidi kwnd punda atakufa kabla ya kifukisha mzigo.
Niwatakie Kazi njema na nangoja maoni yenu wajuvi wa mambo.