Bed Special needs.

Bed Special needs.

kacherema

Senior Member
Joined
Oct 3, 2017
Posts
127
Reaction score
65
Waalimu nipeni uzoefu juu ya hii kozi ya kuchukua shahada ya ualimu special needs, je unachukua teaching subjects kama waalimu wengine mfano Geography au chemistry? Pia ufundishaji unajikita kwa wenye shida ya usikivu na kuona au hata kwa wenye mtindio?Namaanisha majukumu ya kimsingi kwa huyu mwalimu wa mahitaji maalumu awapo shuleni ni yapi. Na vipi kipaumbele chake kwenye ajira za serikalini.
 
Kozi ipo chuo kikuu cha Dodoma na chuo Kikuu cha Kumbukukumbu ya Sebastian Kolowa (SEKOMU) japo kwa sababu za kisiasa kimefungwa, na wanafunzi wamehamishwa UDOM.

OK, kozi hii ni sehemu ya Kozi ya Psychology, Mwanafunzi atasoma Lugha ya ishara kwa ajili ya watu wenye shida ya Usikivu, lakini atasoma BRAIL COURSE (mashine ya Kuchapia kwa vipofu) wa ajili ya uono.


Kwa chuo kikuu cha Dodoma Utasoma Miaka Mitatu, ukiwa na somo moja la kufunzia. Kozi zitakazobaki ni zile za profession ya ualimu na saikolojia kwa watu wenye uhitaji maalum

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa chuo kikuu cha Dodoma Kozi hii ni Very Partial, na wala hau specify unasoma nini haswa (ulemavu gani)

Chuo kikuu cha SEKOMU kozi hii ilikuwa ni kozi kuu, na mwalimu husoma Kiundani ulemavu mmoja kati ya uono au usikivu. Majukumu makubwa ya mwalimu, baada ya kozi hii, ni kufundiasha watu wa namna hii, kuwasaidia kwa namna nje ya kufundisha, kutengeneza mitaala ya watu wenye uhitaji maalumu, kulea na kutunza watu hawa.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Suala la ajira linaambatana tuu na walimu wengine, japo kipaumbele chake ni kikubwa actually.

Changamoto ni kwamba vituo ni vichache.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante sana kiongozi.
Kozi ipo chuo kikuu cha Dodoma na chuo Kikuu cha Kumbukukumbu ya Sebastian Kolowa (SEKOMU) japo kwa sababu za kisiasa kimefungwa, na wanafunzi wamehamishwa UDOM.
OK, kozi hii ni sehemu ya Kozi ya Psychology, Mwanafunzi atasoma Lugha ya ishara kwa ajili ya watu wenye shida ya Usikivu, lakini atasoma BRAIL COURSE (mashine ya Kuchapia kwa vipofu) wa ajili ya uono.
Kwa chuo kikuu cha Dodoma Utasoma Miaka Mitatu, ukiwa na somo moja la kufunzia. Kozi zitakazobaki ni zile za profession ya ualimu na saikolojia kwa watu wenye uhitaji maalum
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shukrani ndugu. Ila naomba ufafanuzi unaposema hii kozi kwa Udom unasoma partially (hauchimbui kiundani)inamaanisha utasoma kufundisha aina zote walemavu bila kujikita mahsusi kwenye hizi kuu zinazohusiana na wasioona na kusikia au ni kwamba utahitimu bila kujua una weledi wa kufundisha walemavu wapi? unamaanisha nini hasawa?
Kwa chuo kikuu cha Dodoma Kozi hii ni Very Partial, na wala hau specify unasoma nini haswa (ulemavu gani)
Chuo kikuu cha SEKOMU kozi hii ilikuwa ni kozi kuu, na mwalimu husoma Kiundani ulemavu mmoja kati ya uono au usikivu. Majukumu makubwa ya mwalimu, baada ya kozi hii, ni kufundiasha watu wa namna hii, kuwasaidia kwa namna nje ya kufundisha, kutengeneza mitaala ya watu wenye uhitaji maalumu, kulea na kutunza watu hawa.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shukrani ndugu. Ila naomba ufafanuzi unaposema hii kozi kwa Udom unasoma partially (hauchimbui kiundani)inamaanisha utasoma kufundisha aina zote walemavu bila kujikita mahsusi kwenye hizi kuu zinazohusiana na wasioona na kusikia au ni kwamba utahitimu bila kujua una weledi wa kufundisha walemavu wapi? unamaanisha nini hasawa?
UDOM sio specialist institution ya walemavu kama ilivyo SEKOMU. Namna unavyojifunza ni kwamba unasoma General course bila ubobezi mahsusi kwenye aina gani ya ulemavu unasomea.

Yaani per semester unaweza kusoma kozi mbili za uono na usikivu, kwa hivyo unaiuwa sio mbobezi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pia tunaambiwa siku hizi madarasa yanafanywa mseto (walemavu na wasio na ulemavu darasa moja) kama ushawahi kuhudumia darasa kama hili nisaidie kujua ufundishaji unavyofanyika mfano labda darasa lina wanafunzi wasioona na kusikia na ambao hawana shida na waalimu mko wawili ndani ya darasa, mwalimu wa kawaida na wewe mwalimu wa wenye uhitaji maalumu,sasa hapo anayefundisha mada ni huyu mwalimu wa kawaida alafu wewe kazi yako tu ni kutafsiri anachofundisha kwenda kwenye lugha ya alama au kila mtu anafundisha kivyake?
 
UDOM sio specialist institution ya walemavu kama ilivyo SEKOMU. Namna unavyojifunza ni kwamba unasoma General course bila ubobezi mahsusi kwenye aina gani ya ulemavu unasomea.

Yaani per semester unaweza kusoma kozi mbili za uono na usikivu, kwa hivyo unaiuwa sio mbobezi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kwa sasa course hii iko vizuri UDOM imefanyiwa marekebisho makubwa ni kweli kwa UDOM hakuna kwamba unakua spesho kwa kipofu au kiziwi nafikiri hii ni bora sababu ukipelekwa kwenye viziwi utamudu pia kipofu utamudu huu ndio uzuri wa UDOM,nilisoma hii course hapo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pia tunaambiwa siku hizi madarasa yanafanywa mseto (walemavu na wasio na ulemavu darasa moja) kama ushawahi kuhudumia darasa kama hili nisaidie kujua ufundishaji unavyofanyika mfano labda darasa lina wanafunzi wasioona na kusikia na ambao hawana shida na waalimu mko wawili ndani ya darasa, mwalimu wa kawaida na wewe mwalimu wa wenye uhitaji maalumu,sasa hapo anayefundisha mada ni huyu mwalimu wa kawaida alafu wewe kazi yako tu ni kutafsiri anachofundisha kwenda kwenye lugha ya alama au kila mtu anafundisha kivyake?
Hizo ni Classroom management skills ambapo ujuzi huu unapelekwa kwa walimu wote bila kujali anasomea watu wenye uhitaji maalumu

Inclusive education lazima iambatane na walimu wa SPED jambo ambalo ni msaada, kumbuka kwamba..........Shule za Mseto hazihusiani na TOTAL Impairment.

Kwa mfano, kuna aina za Kiwango cha usikivu.

1. Deaf
2. Low
3. Total

Inclusive haiwahusishi Total. Hao ni kwenye vituo maalumu tu
Hao wengine wanasikia japo kidogo lakini unaweza kufundisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kwa sasa course hii iko vizuri UDOM imefanyiwa marekebisho makubwa ni kweli kwa UDOM hakuna kwamba unakua spesho kwa kipofu au kiziwi nafikiri hii ni bora sababu ukipelekwa kwenye viziwi utamudu pia kipofu utamudu huu ndio uzuri wa UDOM,nilisoma hii course hapo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hali ya kumudu hizo zote kwa wakati mmoja ni ngumu sana, japo lengo lao ni zuri lakini hawajaliwekea mikakati dhabiti ya kumjenga mwalimu aweze mudu watu wote hao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ooh sawa. Nadhani hapa ni swala la chuo husika kujiboresha zaidi kukidhi uhitaji wote wa kada hii au hata kuiga yaliyokuwa yanatolewa na sekomu kule lushoto japo mpaka leo sijajua TCU waliwakuta sekomu na mapungufu gani ambayo hayarekebishiki na chuo kikafunguliwa ili kiendelee kuzalisha walimu wa kuhudumia kundi hili la kipekee kwenye jamii yetu na ambalo mara nyingi limekosa fursa ya elimu hasa elimu ya secondary na ngazi za juu. Kwa jitihada za sekomu kuwa chuo cha kwanza kutoa taaluma hii kwa ngazi ya shahada ingefaa kuwatia moyo na si kuwafungia.
UDOM sio specialist institution ya walemavu kama ilivyo SEKOMU. Namna unavyojifunza ni kwamba unasoma General course bila ubobezi mahsusi kwenye aina gani ya ulemavu unasomea.
Yaani per semester unaweza kusoma kozi mbili za uono na usikivu, kwa hivyo unaiuwa sio mbobezi.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ooh sawa. Nadhani hapa ni swala la chuo husika kujiboresha zaidi kukidhi uhitaji wote wa kada hii au hata kuiga yaliyokuwa yanatolewa na sekomu kule lushoto japo mpaka leo sijajua TCU waliwakuta sekomu na mapungufu gani ambayo hayarekebishiki na chuo kikafunguliwa ili kiendelee kuzalisha walimu wa kuhudumia kundi hili la kipekee kwenye jamii yetu na ambalo mara nyingi limekosa fursa ya elimu hasa elimu ya secondary na ngazi za juu. Kwa jitihada za sekomu kuwa chuo cha kwanza kutoa taaluma hii kwa ngazi ya shahada ingefaa kuwatia moyo na si kuwafungia.
Sababu za usimamizi wa chuo, rushwa n.k zilisababisha chuo kufungwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vipi Mkuu wakati unasoma field ulipelekwa kwenye vituo vya uhitaji maalumu au shule za mchanganyiko? Au field inagawanywa labda mwaka wa kwanza kituo na wa pili shule mchanganyiko? Na vipi sasa baada ya kuhitimu maisha yalivyo umepata pa kufundisha
Mkuu kwa sasa course hii iko vizuri UDOM imefanyiwa marekebisho makubwa ni kweli kwa UDOM hakuna kwamba unakua spesho kwa kipofu au kiziwi nafikiri hii ni bora sababu ukipelekwa kwenye viziwi utamudu pia kipofu utamudu huu ndio uzuri wa UDOM,nilisoma hii course hapo.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watanzania wagumu sana kuelewa someni kozi mnazoweza kujiajiri huu ualimu wenu utawatokea puani
 
Back
Top Bottom