Beating the Drum on One Side: Confusing the People on Both Sides

nawe pia nakuuliza, kwa nini wakatae vitabu vyako? Sina hakika na MUM ambako mkuu ana mentality kama yako
Nyakageni,
Nimekujibu kuwa hilo swali unalileta sipo.

Hao wanaokataa kitabu changu ndiyo wa kuulizwa.

Mimi ninachoweza kukueleza ni kuwa kitabu changu kilipochapwa London
mwaka 1998 kilifanyiwa pitio na John Iliffe wa University of Cambridge na
kikapata heshima ya kutiwa kwenye Cambridge Journal of African History.

Hili ni journal linaloheshimiwa dunia nzima.

James Brenan wa London School of Oriental and African Studies na yeye
akafanya pitio na nikaingia tena kwenye journal lao na Jonathon Glassman
wa Nortwestern University na yeye akafanya pition na nikaingia tena kwenye
journal na kwingi nikawa maarufu.

Alhamdulilah.
Ni hayo tu.
 
Hilo nalo dogo?

Maji yakishamwagika hayazolekiii

Kwnye historia hii kamwe hawawez NA HAWATII MKONO HATA KAMA WAMENAWA.

 

hivi unajua hata lini Nyerere aliachia ofisi kweli?

MOU ilifanyika mwaka gani?

Unamlaumu Nyerere kwa lipi kuhusu fair treatment ya wachache kama wahindi na wazungu kuwa watanganyika bila ubaguzi?
 
Last edited by a moderator:

Matumbo,
hapana haja ya kutumia maneno makali, "ujinga," nk.

Prof. Hirji bahati mbaya hayupo hapa.
Juu ya hayo nimeweka maswali yangu hapa kwenye uzi ambayo angekuwapo
labda angenijibu.

Maswali na majibu ni njia mbili.
Hapa nipo mimi peke yangu Prof. Hirji hayupo.

Sasa tunafanyaje katika hali kama hii?

Unashindwa kunielewa.

Kabla ya kuandika kitabu cha Abdul Sykes ulijua kama ni yeye ndiye aliyeasisi
TANU?

Ulijua kama kadi yake ya TANU ni namba 3 na ya mdogo wake Ally ni namba 2?
Ulijua kama kadi ya Nyerere aliandikiwa na Ally Sykes?

Naamini kuna mengi hukuwa unayajua.
 

hujanielewa, swali ni kwa nini kitabu chako kimekataliwa UDSM?

Kuhusu kukubalika Uingereza Prof Hirji kasema academicians wa Tanzania mnakimbilia kwa donors kupata dollars, working for their interests

he who pays the piper chooses the song!
 

But what is a big deal hapa? Kwani kama walibeba mzigo waliubeba kwaajili ya dini yao au waliubeba kwaajili ya Taifa lao? Then why should one argue udini hapa kwani Tanganyika wakati huo kulikuwa na dini moja tu? Then for example wapagani wangeondoa ukoloni je ingewapa haki katika upagani wao in comparison to other belief ama tungewashukuru kama Taifa na muendelezo ungetegemea malengo yaliyowekwa na wanataifa?

Ndugu zangu hizi tabia za kushikilia historia bila kuweka objectivity ndicho kinacho tu cost mpaka leo; miaka 50+ baada ya uhuru bado tunalalamika wakoloni ndiyo sababu ya umasikini wetu.... Kuna nchi kadhaa duniani zilitawaliwa yet zingine ni amongst top three the richest. Kama ukoloni ni sababu tunazungumziaje hao wenzetu ambao kwao siyo tatizo?

Pia kwanini basi ss hatukutawala wengine bali tulitawaliwa? Namaanisha pia kuuliza je hao heroes tunaolazimisha historia zao walikuwa wapi mpaka waka surrender kwa hawa tunao walaumu leo?

Characteristics ya failures wengi ni kuji console na kutafuta sababu za kushindwa kwao; mara nyingi wanapenda ku paint success za washindani kwakuzigeuza na kuzi demonise na hatimaye kuzitumia kama sababu za kushindwa kwao kumbe bila kujua wanaongea fear zao ambazo wakati mwingine wangeweza kuzi overcome zingekuwa opportunities za ku excel
 
The big , nadhani Mohamed anapoweka paper na mabandiko yake nikufahamisha, kuelewesha na kutoa ufafanuzi. Na katika hayo lazima kuwe na ‘critique'

Kisomi si lazima kila mtu aende kufanya tafiti. Kupitia ‘critique'ndipo mambo mengine yanapojitkeza.
Labda kama imekusudiwa kuwa anayoandikaMohamed ni ya kumeza tu


Nyuzi nyingi tumewahi kumwambia Mohamed kuwa historia anayoandika imejikita katika upande mmoja. Huwezi kusahihisha kosa kwa kufanya kosa.

Kwa bahati mbaya, mzee ni mgumu sana wa kuelewa. Mag3 aliwahi kumuuliza nani alianzisha TAA. Mohamed kasema ni Kleist Sykes . Mag3 katoa ushihidi wa Mwalimu C.Matola ambao Mohamed hakuupinga.Ndicho anachosema prof kuwa historiailiyokuwepo ilikuwa na matatizo, na matatizo hayo yameendelezwa na Mohamed kwakuficha ukweli akiegemea katika Imani.

Mohamed mara nyingi na hasa uzi wake wa mwisho amesema anaandika historia ili watu waelewe.
Ukisoma bandiko lake moja hapo, kwa kiwewe anajikuta anazungumzia Imani badala ya historia.
Halafu anataka vitabu vyake view katika mtaala. Unaona makosa ya mzee


Tuliwahi kumuuliza kama Abdul alikutana na Mwl mwaka 1950.Mohamed kasema ndivyo ilivyokuwa.
Tukamwekea ushahidi kuwa walikutana kabla yahapo. Leo anarudia kile kile alichowahi kukoselewa.
 
hivi unajua hata lini Nyerere aliachia ofisi kweli?

MOU ilifanyika mwaka gani?

Unamlaumu Nyerere kwa lipi kuhusu fair treatment ya wachache kama wahindi na wazungu kuwa watanganyika bila ubaguzi?
Muiteni huyo Prof hapa jamvini atueleze kwa nini Kambarage Nyerere, baada ya Uhuru wa Tanganyika aliwakatama Masheikh wetu na kuwaweka magerezani na wengine aliwafukuza Tanzania.
 

Muhasisi wa TANU ni Mwl Nyerere, hao kina Sykes walikuwa na kijiwe cha soga kinaitwa TAA .
 
hadi sasa hajajibu hoja zaidi ya kuweka malalamiko zaidi! Mara Mwembechai, mara Kitwana Kondo, namsubiri tu
Nyakageni,
Hakuna malalamiko.

Nimeweka takwimu za Mzee Kondo kuongezea zile zilizowekwa na Prof. Hirji
ili wanajamvi na wao wazione.

Kuna kitu kimoja tu ningependa kukutanabaisha.
Chunga lugha yako.

Andika kiungwana.
Huu mnakasha wengi watafaidika ila mimi huwa siwezi kujadiliana "kihuni.'

"Mara Mwembechai mara..." epuka staili hii.
Hiyo si staili ya wasomi wanapojadili.

Wasomi hawabughudhiani.

Sisi tuna lugha zetu.
Mimi sina sababu kukudhania vingine ila wewe ni msomi.

Usiniangushe.
 
Muteni huyo Prof hapa jamvini atueleze kwa nini baada ya Uhuru wa Tanganyika aliwakatama Masheikh wetu na kuwaweka magerezani na wengine aliwafukuza Tanzania.

Ingekuwa vema ungewataja kwa majina.
 
Matumbo,
Ikiwa kama usemavyo huenda wametuona wajinga hivyo wametupuuza hilo
vilevile sawa pia.
Mohamed, wewe unaandika historian a upo katika top 500 kwamujibu wako. Unaposema wametuona, ni dhidi ya nani? Maana somo hapa ni historia na vilivyototokea, sasa wametuna inaingiaje. Wametuona ni akina nani dhidi ya nani
 

Nadhani chapisho kukubalika inategemea malengo ya publisher vilevile mengine yakiwa nje ya kusudi la mwandishi....Pengine reviewer akaona inavutia wasomaji wengi na kusababisha debate kubwa na kwajinsi hiyo ni worthy for it to be published!

Lakini swali langu ni objective ya wewe kuiandika hiyo history upya nini? Ku promote hiyo category ya waleta uhuru, kuleta umoja wa kitaifa ama ku create academic debates? Ama ni for personal benefits, kama academic recognition, kutetea imani ama tu ni kufurahia religious debates?
 
Muhasisi wa TANU ni Mwl Nyerere, hao kina Sykes walikuwa na kijiwe cha soga kinaitwa TAA .

Matumbo,
Unakusudia "muasisi" umeandika "muhasisi."

Hayo unayosema ndiyo ulikuwa msimamo wa miaka mingi hadi nilipoandika
kitabu cha Abdul Sykes.

Iwe itakavyokuwa hakuna sababu ya mimi na wewe tukabishana kuhusu hili.
Ukweli sasa uko wazi watu wamesoma kitabu changu na wana uhuru wa kuamini
kile wanachoona kina ukweli.

Mimi nakuomba kitu kimoja tu.
Andika kwa adabu.

Naona staha kidogo inakutoka umehamaki na kuita TAA "kijiwe."
Hapana AA (1929) na TAA na vyama vingine walivyoanzisha wazee wetu
kama Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (1933), TANU (1954) na Tanganyika
Railway African Union (1955) (TRAU) havikupata kuwa "kijiwe.''

Babu yangu Salum Abdallah ndiye alikuwa rais muasisi wa TRAU katibu akiwa
Kassanga Tumbo.

Uongozi wa TANU wa mwanzo pamoja na wanachama wake walitoka Al Jamiatul
Islamiyya.

TRAU ilipigana bega kwa bega na TANU dhidi ya Waingereza.
Yako mengi lakini na tuishie hapa.
 
hujanielewa, swali ni kwa nini kitabu chako kimekataliwa UDSM?

Kuhusu kukubalika Uingereza Prof Hirji kasema academicians wa Tanzania mnakimbilia kwa donors kupata dollars, working for their interests

he who pays the piper chooses the song!
Kwani prof Hirji ni mtume kila atakachosema ni kweli watu wakifuate Hirji ni binadamu kama wewe ana mapenzi yake pia na fikra zake.
 
Muiteni huyo Prof hapa jamvini atueleze kwa nini Kambarage Nyerere, baada ya Uhuru wa Tanganyika aliwakatama Masheikh wetu na kuwaweka magerezani na wengine aliwafukuza Tanzania.

ni masheikh tu hakukuwa na wanaharakati wengine? Prof Hirji anasema Nyerere bado alipata upinzani hata baada ya uhuru toka kwa wanaharakati

Prof Hirji anasema Mohamed Said hakueleza sababu za makundi yote kuungana bila kujali dini wala kabila

Zaidi ya hapo kuna masheikh wamo ndani hadi wanalawitiwa na marais wote watano wa pande mbili za muungano ni "ndugu katika iimaan"
 
Kwani prof Hirji ni mtume kila atakachosema ni kweli watu wakifuate Hirji ni binadamu kama wewe ana mapenzi yake pia na fikra zake.

kwani Mohamed Said ni mtume hadi hutaki akoselewe?

Prof Karim Hirji is a well established guru with objective opinion lakini si Mohamed Said a subjective islamic extremist
 
Muiteni huyo Prof hapa jamvini atueleze kwa nini Kambarage Nyerere, baada ya Uhuru wa Tanganyika aliwakatama Masheikh wetu na kuwaweka magerezani na wengine aliwafukuza Tanzania.

Lakini historia anayoiandika mzee inasema wao ndiyo walikuwa wenye chama sasa kwanini hawakumwondoa kabla ya kusababisha ubaya wote huo?

What went wrong mpaka Nyerere akawazidi ma unjanja? Imetuchukua miaka takribani 30+ kuki weaken chama chake kinachotawala hadi leo vipi wao waliweza kuwa weakened ndani ya miaka isiyozidi 10 tena na mtu waliye meonyesha mji? Kwa maelezo hayohayo hata kama hatutaki kusema inabidi tu tukubali Nyerere is a history by himself isiyohitaji msanii wa kuiandika.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…