BE WARNED:this is for all mmu female members

BE WARNED:this is for all mmu female members

Nakadori

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2011
Posts
8,779
Reaction score
21,048
Happy Valentine all,

Poleni na mzunguko wa maisha wa miaka nenda miaka rudi.

Naomba kuwasilisha swala lifuatalo.......Huu sio utani ni swala muhimu sana.

Kuna kijana ni tapeli wa mapenzi/muongo sana yuko hapa JF na huwa ana ID nyingi sana. Huyu kaka amekuwa akitumia kigezo cha kufiwa na mchumba wake kama kigezo cha kupata huruma ya wadada na hivyo kuwarubuni kimapenzi. Sio kweli kwamba amefiwa na mchumba, ukweli ni kwamba ameoa na ana familia yake (mke tena mzuri tu na watoto wawili). Ni mtu ambae basi tu anapenda tabia ya udanganyifu online kwa warembo mbalimbali hadi kufikia hatua ya kuwa kwenye mahusiano. Ni mkazi wa mikoa ya kaskazini.

Yakikufika ya kukufika usije sema hukuambiwa, kuweni makini sana na hawa the so called online lovers, friends n.k. Wengi wao sio, wengi wao ni waongo tu wanaojaribu kucheza na psychology za watu.

Asanteni.
 
Dada zangu, muwe makini, wapo na wanyonya damu humu wanatafuta wa kuwatoa kafara. Ombeni sana Mungu nae atawaepusha na kuwalinda.
 
Duh! Haya wadada mwenzenu tayari yamemkuta. Mapenzi ya mtandao bana wengi wanaliwa wengine wanakula yaani vurugu tupu. Wadada mlio serious na maisha tambueni kwamba hakuna wapenzi wa kweli mtandaoni!
 
Huyu jamaa kweli ana mambo ya kizamani.., Sasa kwanini hasiwe muwazi kwamba anatafuta no strings attached..?, matokeo yake uongo wake anapata watu ambao hawamfai na anatuchukulia ambao wanatufaa sisi 🙁,

Heshima kitu cha bure, humu kuna watu wa aina tofauti kuwa muwazi upate anayekufaa na sio uroho unaopelekea kuumiza watu na kujenga maadui
 
Loooooh! wapo wengi sana siyo huyo tuuuuuuu. Pia embu ninong'oneze kakutenda au vipi.
 
Ashindwe na alegee kama bamia lakuchemsha...

duuuuuuuuuuuuuuuuh!!!!!!!!!!!!! mna matusi ya nguoni kweli, ila washauri wanaoliwa nao wawe makini isijekuwa nao ni katabia kao kujilengesha kwa bazazi.
 
Killing your wife for a fling, that is very low of such a person.
Anyway, gals l am sure kama mtu anakuja ki-uchumba hamtoi tundi; na akija kimapenzi na kama nawe unataka mapenzi basi ukubali hiyo romance ila jua commitment ndio haipo. Usiseme umechezewa wakati amekuomba mapenzi nawe ukaruhusu!
 
Happy Valentine all,

Poleni na mzunguko wa maisha wa miaka nenda miaka rudi.

Naomba kuwasilisha swala lifuatalo.......Huu sio utani ni swala muhimu sana.

Kuna kijana ni tapeli wa mapenzi/muongo sana yuko hapa JF na huwa ana ID nyingi sana. Huyu kaka amekuwa akitumia kigezo cha kufiwa na mchumba wake kama kigezo cha kupata huruma ya wadada na hivyo kuwarubuni kimapenzi. Sio kweli kwamba amefiwa na mchumba, ukweli ni kwamba ameoa na ana familia yake (mke tena mzuri tu na watoto wawili). Ni mtu ambae basi tu anapenda tabia ya udanganyifu online kwa warembo mbalimbali hadi kufikia hatua ya kuwa kwenye mahusiano. Ni mkazi wa mikoa ya kaskazini.

Yakikufika ya kukufika usije sema hukuambiwa, kuweni makini sana na hawa the so called online lovers, friends n.k. Wengi wao sio, wengi wao ni waongo tu wanaojaribu kucheza na psychology za watu.

Asanteni.

Huko ni kupenda "Avatar"..
Yalinikuta zamaani.. Passport photo, macho yamelegea, shingo ya upanga, ngozi nyoroooro.
Tukapanga appointment.. tukakutana live..:smiling:
...Tooba..!! Lahaula.!!!:eek2::eek2:... Miguu haitizamiki.!! yote miwili ya kushoto..!!! Na kuna mwanadada ninayemfahamu aliingia kichwa kichwa kwa Mzambia, akatumiwa nauli ya kwenda Zambia... Amerudi na 'miwaya".

Lesson : Avoid rushing into so called "online dating" or check background first. Ya nini yote hayo? Mbona mjumbe wa nyumba kumi ana watoto wazuri tu?
 
Uuuuwiii. asije akamkwangua Erotica wangu jamani! Ila nina imani kabisa kwamba huyo kijana ndie atakwanguliwa na lady makini Erotica! Usimchezee huyu mama aisee. Utajuta!
 
Last edited by a moderator:
Dii

Wonders shall never end oooooo!

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
hiyo ni kweli mtoa mada....watu wamejikuta wakidate na majini na kushindwa kujinasua...umakini unahitajika humu mtandaoni.
 
Dah! Habari ndio hio! Taarifa hii sijui keshaipata muhusuka!?! Lakini reporters wetu wapo kila sehemu usijali ujumbe utamfikia tu! Atajiju! Lol
 
kweli kbs,yaan usikae ukaamini hawa watu wa mitandaoni....ni full mizengwe.
 
Pole sana kwa yaliyo kukuta...Mpaka alikuambia ameoa na ana watoto wawili...?Pole sana..
 
Back
Top Bottom