Hapa tusilaumu mtu, wa kulaumiwa watu wajua kiswahili na pia wataalam wa Kiswahili kwani makosa kama haya hawayakosoi. Wanakaa kimyaa tu.
Pia kuna tatizo kubwa kwa Watanzania kutotaka kujituma na kuomba kazi sehemu kama BBC na kazi nyingi za kimataifa.
Mnajua majirani zetu wanajituma sana na pia ni wachapa kazi zaidi ya wa Tz.
Ingawa mimi ni Mjamaa na napenda siasa ya ujamaa nadhani dosari yake na madhara yake ndo hayo kama haikutumika vizuri. Kutokana na utafiti wangu binafsi nadhani siasa ya Ujamaa ilichangia sana watu kuwa wazembe wazembe na kupenda kuunganishiwa kazi, siyo kuomba na kuchakarika mwenyewe.