BAVICHA Wapiga Tatu Kwa Mpigo Kujiimarisha

BAVICHA Wapiga Tatu Kwa Mpigo Kujiimarisha

Chademakwanza

JF-Expert Member
Joined
Jun 11, 2014
Posts
6,346
Reaction score
1,873
Baraza la vijana wa CHADEMA (BAVICHA ) Leo wanafanya mashambulizi katika sehemu tatu tofauti katika kuhakikisha wanaendelea kuliimairisha Baraza hilo na kukiandalia Chama mazingira mazuri zaidi ya kushika dola 2015.

Wakati Makamu M/kiti bara Patrick Sosopi,akiwa Kigamboni leo kukagua uhai wa Baraza na jioni mkutano mkubwa wa hadhara utakao andaliwa na BAVICHA Kigamboni kwa kushirikiana na viongozi wa Chama,wakati huohuo kuanzia saa9 jioni Makamu M/kiti Zanzibar Zeud Mvano atakuwa katika chuo cha TIA kufungua Tawi jipya la CHASO.Jioni atazindua Ofisi na hatimae atafanya mkutano mkubwa wa hadhara maeneo Mtoni mtongani majira ya saa 10 jioni.

Upande wa Kanda ya kati,Mkoa wa morogoro mamlaka ya mji mdogo wa Ifakara,Katibu Mkuu wa BAVICHA Juliusi Mwita akiwa na Katibu Mwenezi wa BAVICHA Taifa watakuwa na Semina na CHASO katika chuo cha St.Francis Ifakara mjini na hatimae uchaguzi wa Viongozi wa CHASO.

Baada ya hapo jioni ya saa10 kutakuwa na mkutano mkubwa wa hadhara,katika viwanja vya Yongo Ifakara mjini.

Hakuna kulala mpaka kieleweke...,Viva BAVICHA viva CHADEMA.
 
Asanteni Sana Vijana wangu wa Bavicha Mnafanya kazi iliyo TUKUKA
 
Habari za ngoma ya msanja usitusumbue nazo Habari ya mujini ni Sheikh Amri Abeid Kaluta.
 
Kamanda habari ya Mujini ni Arusha mgesubiri kwanza hizi habari zenu za Bavicha.

Kilichokuleta mbiombio hapa ni nini? sema unaikubali cdm ila tatizo ni njaa tu.
 
Kamanda habari ya Mujini ni Arusha mgesubiri kwanza hizi habari zenu za Bavicha.

Mkuu ona na wewe ulivyoipuuza habari hiyo na kuja kwenye uzi wa Bavicha..!!!

Unajisikiaje..? Feel at home Comrade..!!!!

BACK TANGANYIKA
 
Back
Top Bottom