[h=2] BAVICHA kuwatimua viongozi wake[/h] MTANZANIA, Alhamisi, Desemba 27, 2012 04:24 Na Benjamin Masese, Dar es Salaam
BARAZA la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA), limesema limewagundua wanachama na baadhi ya viongozi ambao ni virusi na litaanza operesheni nchi nzima ya kuwachukulia hatua za kinidhamu.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa BAVICHA, Deogratus Munishi, alisema hawapo tayari kulea kirusi ndani ya chama ambacho kipo kwa maslahi ya chama kingine na kuongeza kuwa, wameagiza kwa viongozi kuanzia ngazi ya mkoa na wilaya kuwadhibiti.
Kuna uvumi umekuwa ukienezwa kwamba ndani ya Bavicha Taifa kuna mgogoro, hili si kweli kwani viongozi wote wanafanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na tupo tayari kumfukuza mtu yeyote yule anayekwenda kinyume na malengo, dhima na dira yetu.
Kama tunavyofahamu Bavicha ndio nguzo kubwa ndani ya Chadema, kwani vijana wengi Tanzania ni wanachama wetu, hii inatokana na sera yetu ya kupigania ajira, mfumo wa elimu na matatizo yanayowakabili wananchi wote.
Kuendeleza Bavicha tunataka kuisafisha kwa kuwachukulia hatua za kinidhamu ila hatua zetu hatuzichukui katika majukwaa tutafanya vikao vya kisheria dhidi yao, tunaomba kama mtu anajijua ni kirusi ajiondokee mapema kabla ya kukumbwa na fagio linalokuja..
chanzo; mtanzania la leo tar 27/12.
MY TAKE: kwanini Katibu anasema hakuna mgogoro huku anasema kuna kirusi??? sasa wanaoenda kuwachukulia hatua za kinidhamu wana kosa gani??? inabidi tukubali kuwa kuna tatizo ili tulitibu.
Mkuu kuna tofauti kati ya mgogoro na kuwepo kwa wasaliti.
Mgogoro ni kwamba watu wameshindwa kuelewana na hata vikao Na juhudi za kusuluhisha zimeshindikana