BAVICHA Kujirudia ya 2009

BAVICHA Kujirudia ya 2009

TRUJILLO

Member
Joined
Jul 22, 2013
Posts
52
Reaction score
29
Kwa wasiokumbuka,uchaguzi wa bavicha mwaka 2009 ulifutwa baada ya kafulila kuchakachuliwa na kunyimwa ushindi kwa madai alikuwa anaungwa mkono na zitto, hatimaye akaondoka chadema akiitwa sisimizi. siku hizi ameongezeka kidogo anaitwa tumbili. ni wazi sisimizi aliauwa tembo kule kasulu.
uchaguzi wa mwaka huu una kila sura ya kupasua bavicha, kwani Mgombea wa uenyekiti toka kigoma,ameanza kusukiwa mizengwe ili aondolewe ama achakachuliwe kwa hisia kuwa ni mfuasi wa zitto.
lakini,kinyume na waraka wa katibu mkuu, daniel naftal amegharimia nauli,malazi na vyakula vya wajumbe toka bukoba,mbeya,zanzibar,mwanza na shinyanga,na amekuwa na vikao vya kampeni tangu tar 2 kabla ya muda. hatari ni kuwa john heche mwenyekiti anayemaliza muda wake amehudhuria vikao hivyo.kwa maslahi ya chama,nimewasilisha ushahidi wa video wa vikao hivyo.
mpaka sasa kimya,nafikiria kuumwaga hapa ili jamii ione unyamaziaji huu wa uvunjaji kanuni. labda kwa kuwa mhusika anabebwa na chama.
 
Eti ameongezeka amekuwa tumbili hatari sana
 
Huyo mgombea wa Kigoma anaitwa nani?Kanuni za chama na BAVICHA kuhusu malalamiko ya ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi zinasemaje?Nakushauri uwe na subira naamin tuhuma zinashughulikiwa kama umepeleka ktk ngazi husika kuliko kuja hapa jukwaani
 
wewe kama imeshawasilisha malalamiko kwa chama kwa nini usijiweke wazi ulajulikana mana hata kutokujitaja jina lako inaonekana huna habari za uwakika zaidi ya siasa chafu A kuchafuana

huyo mgombei w kigoma ni nan? na amewekewa mizengwe ipi? kua wazi hizi ni siasa chafu zidi ya kamanda naftal
 
Tuwe makini na watu wanaotaka kubomoa chama na wanaofanya siasa chafu...kama suala linashughulikiwa na chama hapa umelileta kwa manufaa yapi?Kwanza nna mashaka ww umetumwa kuvuruga co bure
 
NA ILI LI ACCOUNT LAKO FAKE UNAJARIBU KUPOTOSHA UMMA WAZI WAZI ......KAMA USHAIDI UNAO KWANINI USIWE MWAZI KWA KUTUMIA JINA LAKO KAMILI ??.

Tutahaminije Kama wewe Sio Habibu Mchange au Dotto Rangi Motto ??
 
Acha kumtafutia umaarufu mgombea dhaifu kisa tuu anatokea Kigoma, acha ujinga maswala ya chama yanamalizwa ktk chama siyo JF, mwanachama gani usiyeheshmu katiba ya chama?
 
Tatizo moja la vyama vya upinzani, wanachama wao hawana subira hata kidogo! Pia nidhamu kwa chama na viongozi wao ni ndogo sana, pia wanachama hawawaamini katika kanuni na taratibu walizojiwekea! Chama ni nidhamu, chama ni wanachama, na pia chama ni viongozi. Umesema umepeleka malalamiko na ushahidi, je kwa nini usisubiri? Je ukileta hapa jamvini mapema hivi unakivuruga chama!
 
Back
Top Bottom