BAVICHA kuitisha maandamano ya kitaifa kumg'oa Dr. Slaa!

Status
Not open for further replies.
CHADEMA haiwezi kuvurugwa na watu wachache wenye njaa binafsi CHADEMA ni kilio cha pamoja cha watanzania waliochoshwa na ubadhilifu wa rasilimali zao na kundi la watu wanaojiita CCM... waacheni wafanye hiyo press conf. ila HAATUUDDAANGAAANYIKIIII!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kwani DR Slaa angesema kadi aliichoma moto, nini kingetokea? Si yangekuwa yamekwisha? Au ni nani anayemtunzia kadi yake mpaka CCM wajue kuwa physically anayo ameiweka kwenye sanduku? Aliulizwa swali ameilipia hadi lini lakini majibu bado hajatoa, alisema tu anayo. Binafsi napata shida kidogo na hili suala. Ni jepesi ila DR mwenyewe analicomplicate.

I still believe, CDM kufa ni swala la muda tu.
 
CHADEMA wanazidi kutapatapa ovyo tu kila mmoja anakuja la na wazo lake...ukweli utabaki kuwa ukweli Dr Slaa ni pandikizi la CCM ndani ya CHADEMA.
 
BAVICHA Mwanza mmetumwa sasa naona mnatangaza vita ya maituni na hisia za vijana wa Kitanzania. Sasa ww wa mwz na huyo wa mbeya omba usikutane nasi maake wajinga jama nyie ni kuwapotea mabwepande ndo sehemu yenu. au kafara kwa jambia. Yaani ww kwa akili ya kawaida kadi ya CCM mbona mi ninayo na kiongozi wa chama sina muda wakuipeleka Lumunba wala kuichoma.

Slaa alikuwa na uwezo wa kusema hana kadi na kuizchoma moto ungeongea nn mpumbavu ww. Vitu vingine havina tija mnapewa vijisenti mnaitisha conference za ksenge eti tutaitisha maandamano.

Itisha uone utapita wapi kama hatujakutoa macho mchana kweupe na hao magamba wasikusaidie chochote watabaki wanawacheka kwa kuwachonganisha kama watoto.

JARIBU UONE HII NCHI ILIVYO NA VUJANA WA UKWELI WAPENDA MAENDELEO.
 
mkuu jamaa anasema eddo (yule aliyefanya press conf. Pale mic ubungo) na vija wenzake wapo mwanza wameungana na chagulani wanang'ang'ania kuhoji suala la dr. Kumiliki kadi ya ccm!

CHADEMA hawana sera ndo mana wanahaha, wanahofia CCM kuendelea kushika dola
walianza na operesheni sangara, sasa M4C mwisho watakuja na perege
 
HAPO KWENYE RED nadhani unaweza kuwa sahihi,Lakini si kwamba eti Dr.slaa hawezi kung'oka yeye ni nani?NI KWAMBA DR.SLAA AMESHAKUWA NA SHUTUMA KIBAO NDANI YA CHADEMA ZA KUKIDHALILISHA CHAMA KIASI KWAMBA ANAVUNJA MIOYO YA WATANZANIA WENYE KIU YA MABADILIKO

Umaarufu wa dr unakua kwa kasi ya ajabu,dr ni kichwa hakuna kama yeye kwenye medani za siasa,magamba wataangaika sana mwaka huu
 
Mimi ninayo shilingi hamsini ile ya zamani(ya noti),naweza kuitumia kwenye maduka ya Ccm,Fikiri kabla ya kusema,hatudanganywi na propaganda za marehemu watarajiwa(MAGAMBA)chali.
 
Mkuu mbona unaandika habari nusu nusu au unamuogopa Dr Slaa. Bavicha Mwanza wanasema Dr Slaa ni pandikizi la CCM anamiliki kadi ya CCM haya ndio madai yao makubwa ya Bavicha Mwanza. Wanataka aachie ngazi kama atagoma wataitisha maandamano nchi nzima.
Inaonekana kila kiungo chako cha mwili kwa sasa kime"relax" baada ya kupata habari hizi,hongera sana mkuu!!
 
Wana-CHADEMA 'kufikiria' tu,kuwa DR Slaa ni 'mamluki',tafsiri yangu,ni kama vile maajabu ya wapenzi wa BASA,waandamane kuwa Messi ni mamluki afukuzwe!! Hata Bwana Mungu,atatulaani!
 
chadema wanazidi kutapatapa ovyo tu kila mmoja anakuja la na wazo lake...ukweli utabaki kuwa ukweli dr slaa ni pandikizi la ccm ndani ya chadema.

too bad,kumbe mlimpandikiza??

Sasa kama mlimpandikiza mwenzenu kanogewa sasa,,hatarudi tena huko,,na mbaya zaidi anakuja kuwaua nyinyi wenyewe wapandikizaji,,vipi chungu kumeza eeeh??

Hivi unajiskiaje umemtuma mjumbe wako huku ukitegemea atafanya kazi uliyomtuma na kumpa siri zako zote then huyo mjumbe katokomea moja kwa moja??mtasubiri sana na hamtaamini pale anapochukua nchi 2015,,
 
mimi ninayo shilingi hamsini ile ya zamani(ya noti),naweza kuitumia kwenye maduka ya ccm,fikiri kabla ya kusema,hatudanganywi na propaganda za marehemu watarajiwa(magamba)chali.


wamempandikiza slaa,sasa slaa kaota chadema moja kwa moja

wanalia na kusaga meno mafisadi
 
Chama tawala kinazidi kudhihirisha kushindwa kwake kuliongoza Taifa hili. Ndio maana kila kukicha wanakazana kupigana vijembe na Chadema. Wangekuwa hata na akili za kuazima wao wangeachana na makelele na upuuzi kama huu wa kadi,wangepiga kazi kuiletea nchi maendeleo na kuwajibika kwa dhati huku wakiwaacha Chadema waendelee na mikakati yao, mwisho wa siku wananchi wangeshawishika kuwapa tena nafasi kwa utendaji mzuri na uwajibikaji ikiwemo kuwaadabisha mafisadi na wale wote wanaokiuka miiko ya viongozi!! Vinginevyo wanazidi kujipalia mkaa wa moto,watanzania wa leo si mazuzu,useme kila kukicha upige domo kuzungumzia KADI,KADI,KADI huku hamna gamba lililojiuzulu,wanyama wetu bado wapo Qatar, watu wameficha manoti Uswisi wanakula bata hadi leo...............
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom