BAVICHA KARIBUNI DODOMA:
Chama Cha Mapinduzi kinatarajia kufanya mkutano mkuu wake wa kikatiba mapema mwishoni mwa mwezi huu. Napenda kuchukua fursa hii kuwakumbusha wenzangu wa BAVICHA maneno yafuatayo."Ukiwa unapita kwenye mbuga kubwa yenye Nyoka na ukagongwa na Nyoka, haupaswi kushangaa kwani ulijua ile ni maskani ya Nyoka na ukapita. Ila ukikodi chumba kwenye hoteli kubwa ya nyota tano, ukajikuta umelalia Nyoka kitandani (hata Nyoka asipokugonga) utashituka na utashangaa kwani pale sio mahala pake."
Nimelazimika kutumia maneno hayo kwa kuwakumbusha vijana wenzangu wa Chama Cha Demodrasia na Maendeleo kuwa pindi mtakapo fika Dodoma na mkakuna na nyoka na akawagonga msilalame. Hampaswi kulalama kwasababu Dodoma ni maskani ya Nyoka na nyie mmefuateni tena kwa shari.
Nasema hivyo kwa sababu mmekuwa mabingwa wa vitisho kwa kuwatushia wakubwa nyau pasi kujua kuwa kwa kufanya hivyo mnaelekea katika njia ya kujipoteza na kuhatarisha amani ya nchi yetu, amani ambayo kila mzalendo anaapa kuilinda kwa gharama yeyote.
Niwakumbushe tuu kuwa akili za kushiwa changanya na za kwako, tumemsikia kiranja wenu Ole Sosopi akisema anakuja kuwakumbusha jinsi ya kutii sheria, na tunajiuliza ni sheria ipi CCM itakuwa inavunja kwa kikao chake cha kikatiba?Napenda kuwakumbusha Maneno ya Rais wetu Mtukufu John Pombe Magufuli alisema,‘‘Serikali ya Awamu ya Tano itaendelea kulinda kwa nguvu na uwezo wote Tunu hizi za Umoja na Amani. Hatutakuwa na simile kwa mtu au kikundi chochote ambacho kitataka kuvuruga umoja na amani yetu kwa misingi ya udini, rangi, ukabila, vyama au ukanda’’ mwisho wa kunukuu.
Rais wetu mtukufu ameapa kuilinda katiba na katika katiba amani ni tunu mhimu sana, na mtu awae yote atakae chazea amani yetu hakika atasahaurika katika kumbukumbu ya dunia hii. Amani yetu imesababisha tunapiga hatua, tunajenga uchumi wa kati na unaokuwa kwa kasi nzuri, tutakuwa watu wa ajabu sana kuwaona watu wachache wanataka kuchezea amani hii kwa kisingizio cha Demokrasia ili wapitishe agenda zao za kudhohofisha Serikali, hatutakubari hata kidogo.Na mtakapogongwa na nyoka msilaumu kwa sababu mmemfuateni wenyewe nyikani ambapo ni pahala pake.
Nitumieni fursa hii kuwakaribisha CHADEMA na BAVICHA Dodoma kuja kujifunza jinsi demokrasia iliyo huru inavyofanya kazi ndani ya Chama Cha Mapinduzi.Waje kujifunza jinsi wajumbe wa mkutano mkuu wanavyohoji Ilani yao inavyotekelezwa kwa vitendo.Waje wajifunze jinsi CCM inavyopokezana vijiti kwa viongozi wake.
Karibuni sana Dodoma kama mnakuja kujifunza ili mkawe mawakala wazuri huko kwenu ambako uongozi ni wa kurithi.Kama mtakuja kwa nia hiyo karibuni sana, ila kama mna nia Ovu hakika hamtavumilika na nyoka atawagonga kwani mmemfuateni wenyewe.Mwisho kumbukeni Amani ya nchi yetu ni mhimu sana, pindi mtakapofika Dodoma kwa lengo la kukifunza msikose kuhimiza amani na upendo kwa maendeleo ya Tanzania Madhubuti.
Chama Cha Mapinduzi kinatarajia kufanya mkutano mkuu wake wa kikatiba mapema mwishoni mwa mwezi huu. Napenda kuchukua fursa hii kuwakumbusha wenzangu wa BAVICHA maneno yafuatayo."Ukiwa unapita kwenye mbuga kubwa yenye Nyoka na ukagongwa na Nyoka, haupaswi kushangaa kwani ulijua ile ni maskani ya Nyoka na ukapita. Ila ukikodi chumba kwenye hoteli kubwa ya nyota tano, ukajikuta umelalia Nyoka kitandani (hata Nyoka asipokugonga) utashituka na utashangaa kwani pale sio mahala pake."
Nimelazimika kutumia maneno hayo kwa kuwakumbusha vijana wenzangu wa Chama Cha Demodrasia na Maendeleo kuwa pindi mtakapo fika Dodoma na mkakuna na nyoka na akawagonga msilalame. Hampaswi kulalama kwasababu Dodoma ni maskani ya Nyoka na nyie mmefuateni tena kwa shari.
Nasema hivyo kwa sababu mmekuwa mabingwa wa vitisho kwa kuwatushia wakubwa nyau pasi kujua kuwa kwa kufanya hivyo mnaelekea katika njia ya kujipoteza na kuhatarisha amani ya nchi yetu, amani ambayo kila mzalendo anaapa kuilinda kwa gharama yeyote.
Niwakumbushe tuu kuwa akili za kushiwa changanya na za kwako, tumemsikia kiranja wenu Ole Sosopi akisema anakuja kuwakumbusha jinsi ya kutii sheria, na tunajiuliza ni sheria ipi CCM itakuwa inavunja kwa kikao chake cha kikatiba?Napenda kuwakumbusha Maneno ya Rais wetu Mtukufu John Pombe Magufuli alisema,‘‘Serikali ya Awamu ya Tano itaendelea kulinda kwa nguvu na uwezo wote Tunu hizi za Umoja na Amani. Hatutakuwa na simile kwa mtu au kikundi chochote ambacho kitataka kuvuruga umoja na amani yetu kwa misingi ya udini, rangi, ukabila, vyama au ukanda’’ mwisho wa kunukuu.
Rais wetu mtukufu ameapa kuilinda katiba na katika katiba amani ni tunu mhimu sana, na mtu awae yote atakae chazea amani yetu hakika atasahaurika katika kumbukumbu ya dunia hii. Amani yetu imesababisha tunapiga hatua, tunajenga uchumi wa kati na unaokuwa kwa kasi nzuri, tutakuwa watu wa ajabu sana kuwaona watu wachache wanataka kuchezea amani hii kwa kisingizio cha Demokrasia ili wapitishe agenda zao za kudhohofisha Serikali, hatutakubari hata kidogo.Na mtakapogongwa na nyoka msilaumu kwa sababu mmemfuateni wenyewe nyikani ambapo ni pahala pake.
Nitumieni fursa hii kuwakaribisha CHADEMA na BAVICHA Dodoma kuja kujifunza jinsi demokrasia iliyo huru inavyofanya kazi ndani ya Chama Cha Mapinduzi.Waje kujifunza jinsi wajumbe wa mkutano mkuu wanavyohoji Ilani yao inavyotekelezwa kwa vitendo.Waje wajifunze jinsi CCM inavyopokezana vijiti kwa viongozi wake.
Karibuni sana Dodoma kama mnakuja kujifunza ili mkawe mawakala wazuri huko kwenu ambako uongozi ni wa kurithi.Kama mtakuja kwa nia hiyo karibuni sana, ila kama mna nia Ovu hakika hamtavumilika na nyoka atawagonga kwani mmemfuateni wenyewe.Mwisho kumbukeni Amani ya nchi yetu ni mhimu sana, pindi mtakapofika Dodoma kwa lengo la kukifunza msikose kuhimiza amani na upendo kwa maendeleo ya Tanzania Madhubuti.