nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Mwandishi Wetu - Raia Mwema
MAKAMU Mwenyekiti wa UVCCM, Benno Mali
Ahojiwa polisi, risasi zajeruhi mwanafunzi wa CBE
MAKAMU Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), Benno Malisa, amehojiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi, Dar es Salaam kwa madai ya kutodhibiti bastola yake ambayo ilitumika kumjeruhi tumboni mwanafunzi wa Chuo cha Biashara (CBE) Dodoma, Raia Mwema imethibitisha.
Wiki iliyopita gazeti hili liliripoti kuwapo kwa tukio la kumfyatulia risasi mwanafunzi huyo, Emmanuel James Nyakiomo (30), eneo la Sinza, Mugabe, Dar es Salaam karibu na Hoteli ya City Style.
Uchunguzi zaidi wa gazeti hili sasa umebaini kuwa kesi kuhusu tukio hilo lililotokea Novemba 30, mwaka huu, ilifunguliwa kwa mara ya kwanza katika Kituo cha Polisi cha Urafiki, kwa taarifa UPR/RB/100664/11.
Hata hivyo, licha ya jalada kuhusu tukio hilo kufunguliwa kwa takriban mwezi mmoja sasa, kutokana na sababu zisizo wazi kesi hatua zaidi za mbele kuhusu tukio hilo zilisuasua kuchukuliwa na baadhi ya polisi.
Taarifa kuhusu jalada hilo la kesi zinaeleza kuwa gari iliyohusika katika tukio hilo ni aina ya Landcruiser, yenye rangi nyeupe ikiwa na namba za usajili T439BAW, linalodaiwa kutumiwa na Malisa.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, wakati wa tukio hilo Benno Malisa hakuwapo kwenye gari ambalo aliacha bastola yake na dereva aliitumia kuwafyatulia risasi vijana waliomhoji sababu ya kuwamwagia maji machafu.
Katika toleo lililopita la gazeti hili, yaliripotiwa maelezo ya mmoja wa watoa habari wetu akisema; "Baada ya vijana hao kupiga kelele za kwa nini wamemwagiwa maji machafu, dereva huyo ‘alipaki' gari na kuanza kuwafokea vijana hao na walipojibizana naye alifyatua risasi mbili hewani na baadaye moja kumlenga tumboni Emmanuel."
Tukio hilo ambalo lilitokea saa saba usiku wa Novemba 30, 2011, limetajwa kuibua maswali mengi, ikielezwa kuwa kulikuwa na juhudi za kuzuia wahusika kuchukuliwa hatua zinazostahili kwa mujibu wa sheria.
MAKAMU Mwenyekiti wa UVCCM, Benno Mali
Ahojiwa polisi, risasi zajeruhi mwanafunzi wa CBE
MAKAMU Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), Benno Malisa, amehojiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi, Dar es Salaam kwa madai ya kutodhibiti bastola yake ambayo ilitumika kumjeruhi tumboni mwanafunzi wa Chuo cha Biashara (CBE) Dodoma, Raia Mwema imethibitisha.
Wiki iliyopita gazeti hili liliripoti kuwapo kwa tukio la kumfyatulia risasi mwanafunzi huyo, Emmanuel James Nyakiomo (30), eneo la Sinza, Mugabe, Dar es Salaam karibu na Hoteli ya City Style.
Uchunguzi zaidi wa gazeti hili sasa umebaini kuwa kesi kuhusu tukio hilo lililotokea Novemba 30, mwaka huu, ilifunguliwa kwa mara ya kwanza katika Kituo cha Polisi cha Urafiki, kwa taarifa UPR/RB/100664/11.
Hata hivyo, licha ya jalada kuhusu tukio hilo kufunguliwa kwa takriban mwezi mmoja sasa, kutokana na sababu zisizo wazi kesi hatua zaidi za mbele kuhusu tukio hilo zilisuasua kuchukuliwa na baadhi ya polisi.
Taarifa kuhusu jalada hilo la kesi zinaeleza kuwa gari iliyohusika katika tukio hilo ni aina ya Landcruiser, yenye rangi nyeupe ikiwa na namba za usajili T439BAW, linalodaiwa kutumiwa na Malisa.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, wakati wa tukio hilo Benno Malisa hakuwapo kwenye gari ambalo aliacha bastola yake na dereva aliitumia kuwafyatulia risasi vijana waliomhoji sababu ya kuwamwagia maji machafu.
Katika toleo lililopita la gazeti hili, yaliripotiwa maelezo ya mmoja wa watoa habari wetu akisema; "Baada ya vijana hao kupiga kelele za kwa nini wamemwagiwa maji machafu, dereva huyo ‘alipaki' gari na kuanza kuwafokea vijana hao na walipojibizana naye alifyatua risasi mbili hewani na baadaye moja kumlenga tumboni Emmanuel."
Tukio hilo ambalo lilitokea saa saba usiku wa Novemba 30, 2011, limetajwa kuibua maswali mengi, ikielezwa kuwa kulikuwa na juhudi za kuzuia wahusika kuchukuliwa hatua zinazostahili kwa mujibu wa sheria.