Basi la Dar Express lateketea kwa moto

Basi la Dar Express lateketea kwa moto

Mzee wa Shida

Member
Joined
Nov 29, 2014
Posts
66
Reaction score
5
KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Pwani, Jafari Ibrahimu amesema Basi la Dar Express lililokuwa likitokea Dar es Salaam kwenda Arusha, leo mchana limeteketea kwa moto eneo la Kwamakocho, Kijiji cha Kimange, wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani.

attachment.php


Kamanda Ibrahimu amesema kuwa abiria wote waliokuwemo ndani ya basi hilo wako salama.

Eneo la Kwamakocho lipo katikati ya eneo la Mandela na Mbwewe mkoani Tanga.

RPC Jafari Ibrahimu amesema chanzo cha moto huo bado hakijajulikana na akasema uchunguzi unaendelea.
 
Jamani hizi taarifa nimezisikia radio one lakini watu hawakuteketea.

Halafu Jf WhatsApp namba tupatiwe
 
Aisee, mauza uza bado yanaendelea. Usanii wa sticker za fire hausaidii, wanatulipisha Tshs 30,000 na bado hazifanyi kazi.
 
Aisee, mauza uza bado yanaendelea. Usanii wa sticker za fire hausaidii, wanatulipisha Tshs 30,000 na bado hazifanyi kazi.

ya ni kweli mkuu wanaacha kuangalia nyenzo zinazotakiwa kuzima moto kujua ni aina gani ya moto wa daraja gani unatakiwa uzimwe na carbondioxide au powder ssa utakuta nyenzo za mwanzoni awakagui na hakuna elimu za moto kwa abiria wala dereva wakati ajali za moto zinakua kwa kasi sana. Moto hatari uliosababishwa na mafuta ndio hatari sana unataka expert wa fire ndio auzime.stika hata uwe nazo milioni moja azizimi moto.
 
Uzuri wa gari hizo zote zinabima kubwa.
Sasa hapo mwenye gari miguu juu anasubiri alipwe kitu kipya.
Tatizo mali za abiria ndio watu huwa zinakula kwao
 
Aisee, mauza uza bado yanaendelea. Usanii wa sticker za fire hausaidii, wanatulipisha Tshs 30,000 na bado hazifanyi kazi.

Afwande Mpinga; Madereva wamegoma kwenda kusoma hao ndo maana magari yanaungua na mengine kupinduka. Tz ya leo ni majanga tuuu hakuna anayeweza kumshika huyu mchawi anaye tuloga.
Nashauri serekali hii sikivu iagize wataalam kutoka Thailand waje kuagua ka wale wa mvua.
 
Back
Top Bottom