hivi uzuri wa basi nini? nauli mwendo wa dereva au bodi ya gari hiyo kwa nje? au huduma azipatazo mtu ndani ya gari? nisaidieni kuelewa hili kabla sijajibu.
Rangi mama, rangi ya basi ndo kila kitu
dar mza panda MASTER CITY 40,000,= AU SUPER SAMI 40,000/=
mwendo mzuri na mabasi bado mapya,
green star wamebakiza jina na kugawa maji na pipi ila mabasi yamechoka, mwendo mdundo na nauli kubwa 45,000/= hayachelewi kukulaza njiani.
ukitaka mwendo mdundo kufika fasta panda ALLYZ, YAAN SAA MBILI UPO MWANZA .
Kwa basi za kawaida panda Zuberi 35,000 hadi 40,000 au princess shabaha 40000
na ukitaka kulala njiani panda SAI BABA au PRINCESS MURO au NAJMUNISA au BEST LINE
HAYA KAZI KWAKO MDAU
rangi ????????????????????? ya basi ndio kila kitu? dereva wake akiwa mlevi na anaendesha kwa mwendo wa ajbu kwako itakuwa sawa mkuu?
Mi na Yutong tofauti kabisa!Hayo mabasi ni mazuri kwa mwendo lakini seat zake zinaumiza mgongo hazina tofauti na za kosta.
Hayo mabasi ni mazuri kwa mwendo lakini seat zake zinaumiza mgongo hazina tofauti na za kosta.
Mi na Yutong tofauti kabisa!
hahahaa! we mtu sio mzuri kabisaaaa!!Precision
Msaada tutani..
Ni basi gani zuri luxury liendalo mwanza lenye huduma nzuri pamoja na mwendo mzuri (usiokuwa wa mbio)
Hili basi limenivutia ha ha haa!!Lakini hii bei inanipa utata mbona cheap sana ulipata ofa nini au wajuana na wauza tiketi counter??Basi zuri ni Fast Jet nauli buku 32 tu.. Sema dereva anakimbiza sana masaa mawili tu upo mwanza..
Sema jiandae hakuna pipi wala maji ya bure humo, kila kitu unanunua