Habari Wana jukwaa,Takribani miezi miwili imepita toka kampuni ya new habari ltd ilipowaondoa wafanyakazi wake kwa kuwapunguza kazi (retrenchment). Wakaahidiwa kuwa pesa zao za mishahara ya nyuma na stahiki za kupunguzwa kazi watalipwa ndani ya siku kumi na tano kadri ya barua walizopewa.Sasa ni miezi miwili na hakuna taarifa yeyote toka kwa CEO wa kampuni ndugu Bashe.Tunalileta Hilo jukwaani ili tuwasaidie Hawa ndugu zetu wapate stahiki zao.maana maisha yao ni ya shida kwa wale tulionao mtaani.