Nimepata kumsikiliza waziri Bashe katika kujitahidi kujiinua kilimo nchini. Anabidii nzuri lakini nadhani anapaswa kupewa washauri wazuri wanaojua biashara ya kilimo
Binafsi nashauri yaanzishwe makampuni ya kilimo moja Kwa moja shambani,iwe ni ubia wa serikali na watu binafsi Kwa mfumo wa hisa, yakopeshwe fungu maalum na BOT kwa udhamini wa serikali,yapewe mpango kazi na yashindanishwe katika kuzalisha...yenyewe ya recruit vijana na kusimamia kilakitu wizara ibaki ku-deal na makampuni yaliyokuwa organized kiuongozi na siyo vijikundi vya vijana hatakama umewapeleka jkt sijui.
Inashtua kuskia waziri anasema kunavijana wamekosa nidhamu tumewafukuza kwenye mradi!!! Unapatawapi muda wa kushughulika na vijana na tabia zao wewe kama waziri??
Kilimo kimepitiaga misemo na bidii nyingi za serikali LAKINI hazifanikiwa kwakuwa serikali inajiweka front wakati yenyewe inatakiwa kuweka sera na mazingira Bora ya kilimo na masoko ikiwa nipamoja na kuanzisha makampuni ya kilimo ya wazawa.
Hatitaki kodi zetu za mabilioni zitumike kuanzisha biashara hasara za kutupotezea mabilioni mengine! Ajifunze TRC,ATCL,TTCL nakadhalika!! Serikali haitoweza kusimamia agriculture business on the ground Bali kusimamia makampuni Kwa kuingia ubia nayo.