Ili CCM ife kifo cha ASILI, hakuna JIWE litaachwa kusimama juu ya JIWE lingine. Kwasababu NGUZO kubwa inayokiongoza chama hiki ni FITINA na RUSHWA tunazozishuhudia waziwazi sasa. Hili linatokana na mfumo wa kinafiki na mitandao/makundi waliojitengeneza wenyewe. Sasa kila kundi linajiona lipo juu na hakuna linalotaka kujishusha. Walianza kwa uchaguzi wa Urais, wakaingia kwenye chaguzi zao za ndani ambao sasa ndiyo SUMU yao kubwa waliojitengenezea.