BARUA YA WAZI KWA ROSTAM na LOWASSA:
Kwa niaba ya Watanzania wote wanaoipenda nchi yao, nawaamuru kusoma barua hii niiandikayo kwenu kupitia mtandao huu wa Great Thinkers. Kama hamtasoma humu naamini vibaraka wenu wata-print na kuwaletea muisome.
Tumefuatilia nyendo zenu kwa muda mrefu na kugundua kwamba ninyi na vibaraka wenu ndani na nje ya NEC ya CCM mmekuwa mkifanya hila na fitina kubwa dhidi ya wana wa nchi hii wanaopinga vitendo vyenu vya kifisadi.
Mmekuwa mkifanya vikao vingi vya kupanga njama za kuwachafua wanasiasa na watu wengine wanaoheshimika kama wapiganiaji wa kweli wa haki za Watanzania walio wengi ili kudumisha ukandamizaji wa wanyonge huku mkilinda maslahi yenu binafsi.
Lakini nimekasirishwa zaidi na kitendo chenu cha hivi karibuni cha kuwahonga wajumbe wa mkutano wa NEC ili wasaidie kutekeleza hila zenu za kutaka kumwondoa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Samwel Sitta, ili muendelee kuitafuna nchi bila usumbufu. Tuliwafuatilia kwa karibu sana kuanzia kule Zanzibar, tulikuwepo pale Hoteli ya Lamada, Dar es Salaam na baadaye Dodoma jinsi wapambe wenu wakiongozwa na Guninita mlivyokuwa mnatapanya pesa kwa wajumbe wapumbafu ili waisaliti nchi yao kwa hila zenu.
Tumerekodi majina na kauli za hao vibaraka wenu wote wa NEC ili tuzifanyie kazi baada ya kuona Idara ya Usalama wa Taifa iliyopaswa kufanya kazi hiyo imelala. Majibu mtayapata baada ya muda si mrefu kwani bado tuna kazi ya kuufahamisha umma wa Watanzania ili watambue jinsi mlivyo watu hatari!
Tunafahamu pia jinsi mnavyomtumia Kingunge Ngombale Mwiru kuupinga Waraka wa kanisa Katoliki kwa sababu umeanisha sifa za viongozi ambao watanzania wanawataka -- yaani viongozi waadilifu. Kwa kuwa nyie hamna sifa hizo mmeona waraka huo ni tishio kwa matamanio yenu ya kutaka kuwa madarakani. Tena wewe Lowassa nasikia eti unataka kuwa Rais baada ya Kikwete! Thubutu!
Tunawaamuru kuacha mara moja kuwapotosha Watanzania kwa kutumia magazeti yenu yanayoongozwa na vibaraka wenu katika kumwaga sumu mbaya kwa wananchi wetu.
Mmejifanya kuwa kimya kwenye vikao halali lakini ni wazungumzaji wazuri sana kwenye vikao vyenu vya siri mnavyovifanya hadi usiku wa manane.
Kwa barua hii, mtambue kwamba Watanzania mliowanyonya kwa muda mrefu sasa wameamka na wako tayari kurejesha UHURU wao ili waweze kumiliki kikamilifu raslimali lukuki za nchi yao walizojaliwa na Mungu. Tanzania ni nchi tajiri sana lakini ina watu maskini kupindukia kutokana na kuporwa raslimali zao na watu walafi msiotosheka kama ninyi na marafiki zenu wachache.
Ni matarajio yangu kwamba ujumbe huu utasaidia kuwarekebisha ili muache njama zote za kishenzi mnazopanga, ikiwa ni pamoja na kuthubutu kuwaharibia wapiganaji wetu hodari kama Samwel Sitta, Ole Sendeka, Dk Mwakyembe, Anne Kilango, Beatrice Shelukindo, Lucas Selelii, Godfrey Zambi, Fred Mpendazoe na wengine.
Nasema ole wemu!
Kwa niaba ya Watanzania wote wanaoipenda nchi yao, nawaamuru kusoma barua hii niiandikayo kwenu kupitia mtandao huu wa Great Thinkers. Kama hamtasoma humu naamini vibaraka wenu wata-print na kuwaletea muisome.
Tumefuatilia nyendo zenu kwa muda mrefu na kugundua kwamba ninyi na vibaraka wenu ndani na nje ya NEC ya CCM mmekuwa mkifanya hila na fitina kubwa dhidi ya wana wa nchi hii wanaopinga vitendo vyenu vya kifisadi.
Mmekuwa mkifanya vikao vingi vya kupanga njama za kuwachafua wanasiasa na watu wengine wanaoheshimika kama wapiganiaji wa kweli wa haki za Watanzania walio wengi ili kudumisha ukandamizaji wa wanyonge huku mkilinda maslahi yenu binafsi.
Lakini nimekasirishwa zaidi na kitendo chenu cha hivi karibuni cha kuwahonga wajumbe wa mkutano wa NEC ili wasaidie kutekeleza hila zenu za kutaka kumwondoa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Samwel Sitta, ili muendelee kuitafuna nchi bila usumbufu. Tuliwafuatilia kwa karibu sana kuanzia kule Zanzibar, tulikuwepo pale Hoteli ya Lamada, Dar es Salaam na baadaye Dodoma jinsi wapambe wenu wakiongozwa na Guninita mlivyokuwa mnatapanya pesa kwa wajumbe wapumbafu ili waisaliti nchi yao kwa hila zenu.
Tumerekodi majina na kauli za hao vibaraka wenu wote wa NEC ili tuzifanyie kazi baada ya kuona Idara ya Usalama wa Taifa iliyopaswa kufanya kazi hiyo imelala. Majibu mtayapata baada ya muda si mrefu kwani bado tuna kazi ya kuufahamisha umma wa Watanzania ili watambue jinsi mlivyo watu hatari!
Tunafahamu pia jinsi mnavyomtumia Kingunge Ngombale Mwiru kuupinga Waraka wa kanisa Katoliki kwa sababu umeanisha sifa za viongozi ambao watanzania wanawataka -- yaani viongozi waadilifu. Kwa kuwa nyie hamna sifa hizo mmeona waraka huo ni tishio kwa matamanio yenu ya kutaka kuwa madarakani. Tena wewe Lowassa nasikia eti unataka kuwa Rais baada ya Kikwete! Thubutu!
Tunawaamuru kuacha mara moja kuwapotosha Watanzania kwa kutumia magazeti yenu yanayoongozwa na vibaraka wenu katika kumwaga sumu mbaya kwa wananchi wetu.
Mmejifanya kuwa kimya kwenye vikao halali lakini ni wazungumzaji wazuri sana kwenye vikao vyenu vya siri mnavyovifanya hadi usiku wa manane.
Kwa barua hii, mtambue kwamba Watanzania mliowanyonya kwa muda mrefu sasa wameamka na wako tayari kurejesha UHURU wao ili waweze kumiliki kikamilifu raslimali lukuki za nchi yao walizojaliwa na Mungu. Tanzania ni nchi tajiri sana lakini ina watu maskini kupindukia kutokana na kuporwa raslimali zao na watu walafi msiotosheka kama ninyi na marafiki zenu wachache.
Ni matarajio yangu kwamba ujumbe huu utasaidia kuwarekebisha ili muache njama zote za kishenzi mnazopanga, ikiwa ni pamoja na kuthubutu kuwaharibia wapiganaji wetu hodari kama Samwel Sitta, Ole Sendeka, Dk Mwakyembe, Anne Kilango, Beatrice Shelukindo, Lucas Selelii, Godfrey Zambi, Fred Mpendazoe na wengine.
Nasema ole wemu!
Last edited: